< Numeri 1 >

1 IL Signore parlò ancora a Mosè, nel deserto di Sinai, nel Tabernacolo della convenenza, nel primo giorno del secondo mese, nell'anno secondo da che [i figliuoli d'Israele] furono usciti fuor del paese di Egitto, dicendo:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 Levate la somma di tutta la raunanza de' figliuoli d'Israele, secondo le lor nazioni, [e] le famiglie de' padri loro, contando per nome, a testa a testa, ogni maschio,
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 di età da vent'anni in su, tutti coloro che possono andare alla guerra in Israele; annoverateli, tu, ed Aaronne, per le loro schiere.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 E siavi con voi un uomo di ciascuna tribù, che sia capo della sua casa paterna.
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 E questi [sono] i nomi di coloro che saranno presenti con voi: Di Ruben, Elisur, figliuolo di Sedeur;
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 Di Simeone, Selumiel, figliuolo di Surisaddai;
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 Di Giuda, Naasson, figliuolo di Amminadab;
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 D'Issacar, Natanael, figliuolo di Suar;
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 Di Zabulon, Eliab, figliuolo di Helon;
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 De' figliuoli di Giuseppe: di Efraim, Elisama, figliuoli di Ammiud; di Manasse, Gamliel, figliuolo di Pedasur;
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 Di Beniamino, Abidan, figliuolo di Ghidoni;
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 Di Dan, Ahiezer, figliuolo di Ammisaddai;
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 Di Aser, Paghiel, figliuolo di Ocran;
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 Di Gad, Eliasaf, figliuolo di Deuel;
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 Di Neftali, Ahira, figliuolo di Enan.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Costoro [erano] quelli che si chiamavano alla raunanza, principali delle tribù loro paterne, e capi delle migliaia d'Israele.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Mosè adunque ed Aaronne presero seco questi uomini, ch'erano stati nominati per li nomi [loro].
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 E, a' calendi del secondo mese, adunarono tutta la raunanza; e le generazioni [de' figliuoli d'Israele] furono descritte per le lor nazioni, e per le famiglie loro paterne, contandoli per nome dall'età di vent'anni in su, a testa a testa.
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 Come il Signore avea comandato a Mosè, egli li annoverò nel deserto di Sinai.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 E delle generazioni de' figliuoli di Ruben, primogenito d'Israele, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome, a testa a testa, d'infra tutti i maschi, dall'età di vent'anni in su, tutti quelli che potevano andare alla guerra;
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 gli annoverati della tribù di Ruben [furono] quarantaseimila cinquecento.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Delle generazioni de' figliuoli di Simeone, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome, a testa a testa, d'infra tutti i maschi, dall'età di vent'anni in su, tutti quelli che potevano andare alla guerra;
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 gli annoverati della tribù di Simeone [furono] cinquantanovemila trecento.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Delle generazioni de' figliuoli di Gad, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 gli annoverati della tribù di Gad [furono] quarantacinquemila seicencinquanta.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Delle generazioni de' figliuoli di Giuda, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 gli annoverati della tribù di Giuda [furono] settantaquattromila seicento.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Delle generazioni de' figliuoli d'Issacar, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 gli annoverati della tribù d'Issacar [furono] cinquantaquattromila quattrocento.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Delle generazioni de' figliuoli di Zabulon, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 gli annoverati della tribù di Zabulon [furono] cinquantasettemila quattrocento.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 De' figliuoli di Giuseppe; delle generazioni de' figliuoli di Efraim, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 gli annoverati della tribù di Efraim [furono] quarantamila cinquecento.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Delle generazioni de' figliuoli di Manasse, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 gli annoverati della tribù di Manasse [furono] trentaduemila dugento.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Delle generazioni de' figliuoli di Beniaminio, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 gli annoverati della tribù di Beniamino [furono] trentacinquemila quattrocento.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Delle generazioni de' figliuoli di Dan, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 gli annoverati della tribù di Dan [furono] sessantaduemila settecento.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Delle generazioni de' figliuoli di Aser, per le lor nazioni, e famiglie paterne; contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 gli annoverati della tribù di Aser [furono] quarantunmila cinquecento.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Delle generazioni de' figliuoli di Neftali, per le lor nazioni, e famiglie paterne, contati per nome tutti quelli che potevano andare alla guerra, dall'età di vent'anni in su;
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 gli annoverati della tribù di Neftali [furono] cinquantatremila quattrocento.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Questi [furono] gli annoverati, i quali Mosè ed Aaronne annoverarono, insieme co' principali d'Israele, [ch'] erano dodici uomini, uno per familglia paterna.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 Così, tutti gli annoverati d'infra i figliuoli d'Israele, per le lor famiglie paterne, dall'età di vent'anni in su, che potevano andare alla guerra,
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 furono seicentotremila cinquecencinquanta.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Ma i Leviti non furono annoverati fra loro secondo la lor tribù paterna;
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 perciocchè il Signore avea detto a Mosè:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 Sol non annoverar la tribù di Levi, e non levarne la somma per mezzo i figliuoli d'Iraele.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Ma ordina i Leviti sopra il Tabernacolo della Testimonianza, e sopra tutti i suoi arredi; e sopra tutte le cose ad esso [appartenenti]; e portino essi il Tabernacolo e tutti i suoi arredi; e facciano i servigi di esso, e accampinvisi attorno.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 E quando il Tabernacolo si dipartirà, mettanlo giù i Leviti; quando altresì si accamperà, rizzinlo i Leviti; e se alcuno straniere vi si appressa, sia fatto morire.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 Or accampinsi i figliuoli d'Israele, ciascuno nel suo quartiere, e ciascuno presso alla sua bandiera, per le loro schiere.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Ma accampinsi i Leviti intorno al Tabernacolo della Testimonianza; acciocchè non vi sia ira contro alla raunanza de' figliuoli d'Israele; e facciano i Leviti la funzione del Tabernacolo della Testimonianza.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 E i figliuoli d'Israele fecero interamente come il Signore avea comandato.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Numeri 1 >