< Salmi 104 >

1 BENEDICI, anima mia, il Signore; O Signore Iddio mio, tu sei sommamente grande; Tu sei vestito di gloria e di magnificenza.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
2 Egli si ammanta di luce come di una vesta; Egli tende il cielo come una cortina.
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
3 Egli fa i palchi delle sue sale nelle acque; Egli pone le nuvole [per] suo carro: Egli passeggia sopra le ale del vento.
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
4 Egli fa i venti suoi Angeli, E il fuoco divampante suoi ministri.
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
5 Egli ha fondata la terra sulle sue basi; Giammai in perpetuo non sarà smossa.
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
6 Tu l'avevi [già] coperta dell'abisso, come d'una vesta; Le acque si erano fermate sopra i monti.
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
7 Esse fuggirono per lo tuo sgridare; Si affrettarono per la voce del tuo tuono;
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
8 Erano salite sopra i monti; [ma] discesero nelle valli, Al luogo che tu hai loro costituito.
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
9 Tu hai [loro] posto un termine, il qual non trapasseranno; [E] non torneranno a coprir la terra.
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
10 [Egli è quel] che manda le fonti per le valli, Onde [esse] corrono fra i monti;
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
11 Abbeverano tutte le bestie della campagna; Gli asini salvatichi spengono la lor sete [con esse].
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
12 Presso a quelle si riparano gli uccelli del cielo; Fanno sentir di mezzo alle frondi le [lor] voci.
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
13 Egli adacqua i monti dalle sue stanze sovrane; La terra è saziata del frutto delle sue opere.
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
14 Egli fa germogliar l'erba per le bestie; E l'erbaggio per lo servigio dell'uomo, Facendo uscire della terra il pane.
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
15 Egli rallegra il cuor dell'uomo col vino, Egli fa risplender la faccia coll'olio, E sostenta il cuor dell'uomo col pane.
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
16 Gli alberi del Signore [ne] son saziati; I cedri del Libano ch'egli ha piantati;
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
17 Dove gli uccelli si annidano; Gli abeti, [che son] la stanza della cicogna.
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
18 Gli alti monti [sono] per li cavriuoli; Le rocce [sono] il ricetto de' conigli.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
19 Egli ha fatta la luna per le stagioni; Il sole conosce il suo occaso.
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
20 Tu mandi le tenebre, ed e' si fa notte, Nella quale tutte le fiere delle selve vanno attorno.
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
21 I leoncelli rugghiano dietro alla preda, E per chiedere a Dio il lor pasto.
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
22 [Ma, tosto ch]'è levato il sole, si raccolgono, E giacciono ne' lor ricetti.
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
23 Allora l'uomo esce alla sua opera, Ed al suo lavoro, infino alla sera.
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
24 Quanto grandi sono, o Signore, le tue opere! Tu le hai tutte fatte con sapienza; La terra è piena de' tuoi beni.
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
25 Ecco, il mar grande ed ampio: Quivi son rettili senza numero, Amimali piccoli e grandi.
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
26 Quivi nuotano le navi, E il Leviatan che tu hai formato per ischerzare in esso.
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
27 Tutti [gli animali] sperano in te, Che tu dii loro il lor cibo al suo tempo.
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
28 [Se] tu [lo] dài loro, [lo] ricolgono; [Se] tu apri la tua mano, son saziati di beni.
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
29 [Se] tu nascondi la tua faccia, sono smarriti; [Se] tu ritiri il fiato loro, trapassano, E ritornano nella lor polvere.
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
30 [Se] tu rimandi il tuo spirito son creati; E tu rinnuovi la faccia della terra.
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
31 Sia la gloria del Signore in eterno; Rallegrisi il Signore nelle sue opere;
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
32 Il quale se riguarda verso la terra, ella trema; Se tocca i monti, essi fumano.
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
33 Io canterò al Signore, mentre viverò; Io salmeggerò all'Iddio mio, tanto che io durerò.
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
34 Il mio ragionamento gli sarà piacevole, Io mi rallegrerò nel Signore.
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
35 Vengano meno i peccatori d'in su la terra, E gli empi non sieno più. Anima mia, benedici il Signore. Alleluia.
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.

< Salmi 104 >