< Proverbi 14 >

1 La donna savia edifica la sua casa, ma la stolta l’abbatte con le proprie mani.
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Chi cammina nella rettitudine teme l’Eterno, ma chi è pervertito nelle sue vie lo sprezza.
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
3 Nella bocca dello stolto germoglia la superbia, ma le labbra dei savi son la loro custodia.
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
4 Dove mancano i buoi è vuoto il granaio, ma l’abbondanza della raccolta sta nella forza del bove.
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
5 Il testimonio fedele non mentisce, ma il testimonio falso spaccia menzogne.
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
6 Il beffardo cerca la sapienza e non la trova, ma per l’uomo intelligente la scienza è cosa facile.
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
7 Vattene lungi dallo stolto; sulle sue labbra certo non hai trovato scienza.
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
8 La sapienza dell’uomo accorto sta nel discernere la propria strada, ma la follia degli stolti non è che inganno.
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
9 Gli insensati si burlano delle colpe commesse, ma il favore dell’Eterno sta fra gli uomini retti.
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
10 Il cuore conosce la sua propria amarezza, e alla sua gioia non può prender parte un estraneo.
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
11 La casa degli empi sarà distrutta, ma la tenda degli uomini retti fiorirà.
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
12 V’è tal via che all’uomo par diritta, ma finisce col menare alla morte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
13 Anche ridendo, il cuore può esser triste; e l’allegrezza può finire in dolore.
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
14 Lo sviato di cuore avrà la ricompensa dal suo modo di vivere, e l’uomo dabbene, quella delle opere sue.
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
15 Lo scemo crede tutto quel che si dice, ma l’uomo prudente bada ai suoi passi.
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
16 Il savio teme, ed evita il male; ma lo stolto è arrogante e presuntuoso.
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
17 Chi è pronto all’ira commette follie, e l’uomo pien di malizia diventa odioso.
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
18 Gli scemi ereditano stoltezza, ma i prudenti s’incoronano di scienza.
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
19 I malvagi si chinano dinanzi ai buoni, e gli empi alle porte de’ giusti.
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
20 Il povero è odiato anche dal suo compagno, ma gli amici del ricco son molti.
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
21 Chi sprezza il prossimo pecca, ma beato chi ha pietà dei miseri!
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
22 Quelli che meditano il male non son forse traviati? ma quelli che meditano il bene trovan grazia e fedeltà.
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
23 In ogni fatica v’è profitto, ma il chiacchierare mena all’indigenza.
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
24 La corona de’ savi è la loro ricchezza, ma la follia degli stolti non è che follia.
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
25 Il testimonio verace salva delle vite, ma chi spaccia bugie non fa che ingannare.
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
26 V’è una gran sicurezza nel timor dell’Eterno; Egli sarà un rifugio per i figli di chi lo teme.
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
27 Il timor dell’Eterno è fonte di vita e fa schivare le insidie della morte.
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
28 La moltitudine del popolo è la gloria del re, ma la scarsezza de’ sudditi è la rovina del principe.
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
29 Chi è lento all’ira ha un gran buon senso, ma chi è pronto ad andare in collera mostra la sua follia.
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
30 Un cuor calmo è la vita del corpo, ma l’invidia è la carie dell’ossa.
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
31 Chi opprime il povero oltraggia Colui che l’ha fatto, ma chi ha pietà del bisognoso, l’onora.
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
32 L’empio è travolto dalla sua sventura, ma il giusto spera anche nella morte.
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
33 La sapienza riposa nel cuore dell’uomo intelligente, ma in mezzo agli stolti si fa tosto conoscere.
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
34 La giustizia innalza una nazione, ma il peccato è la vergogna dei popoli.
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
35 Il favore del re è per il servo prudente, ma la sua ira è per chi gli fa onta.
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< Proverbi 14 >