< Salmi 109 >

1 Per il Capo de’ musici. Salmo di Davide. O Dio della mia lode, non tacere,
Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
2 perché la bocca dell’empio e la bocca di frode si sono aperte contro di me; hanno parlato contro di me con lingua bugiarda.
Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
3 M’hanno assediato con parole d’odio, e m’hanno fatto guerra senza cagione.
Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
4 Invece dell’amore che porto loro, mi sono avversari, ed io non faccio che pregare.
Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
5 Essi m’hanno reso male per bene, e odio per il mio amore.
Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
6 Costituisci un empio su di lui, si tenga alla sua destra un avversario.
Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
7 Quando sarà giudicato, esca condannato, e la sua preghiera gli sia imputata come peccato.
Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
8 Siano i suoi giorni pochi: un altro prenda il suo ufficio.
Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
9 Siano i suoi figliuoli orfani e la sua moglie vedova.
Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
10 I suoi figliuoli vadan vagando e accattino, e cerchino il pane lungi dalle loro case in rovina.
Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
11 Getti l’usuraio le sue reti su tutto ciò ch’egli ha, e gli stranieri faccian lor preda delle sue fatiche.
Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
12 Nessuno estenda a lui la sua benignità, e non vi sia chi abbia pietà de’ suoi orfani.
Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
13 La sua progenie sia distrutta; nella seconda generazione sia cancellato il loro nome!
Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
14 L’iniquità dei suoi padri sia ricordata dall’Eterno, e il peccato di sua madre non sia cancellato.
Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
15 Sian quei peccati del continuo davanti all’Eterno, e faccia egli sparire dalla terra la di lui memoria,
Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
16 perch’egli non si è ricordato d’usar benignità, ma ha perseguitato il misero, il povero, il tribolato di cuore per ucciderlo.
Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
17 Egli ha amato la maledizione, e questa gli è venuta addosso; non si è compiaciuto nella benedizione, ed essa si tien lungi da lui.
Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
18 S’è vestito di maledizione come della sua veste, ed essa è penetrata come acqua, dentro di lui, e come olio, nelle sue ossa.
Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
19 Siagli essa come un vestito di cui si cuopra, come una cintura di cui sia sempre cinto!
Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
20 Tal sia, da parte dell’Eterno, la ricompensa dei miei avversari, e di quelli che proferiscono del male contro l’anima mia.
Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
21 Ma tu, o Eterno, o Signore, opera in mio favore, per amor del tuo nome; poiché la tua misericordia è buona, liberami,
Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
22 perché io son misero e povero, e il mio cuore è piagato dentro di me.
Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
23 Io me ne vo come l’ombra quando s’allunga, sono cacciato via come la locusta.
Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
24 Le mie ginocchia vacillano per i miei digiuni, e la mia carne deperisce e dimagra.
Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
25 Son diventato un obbrobrio per loro; quando mi vedono, scuotono il capo.
Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
26 Aiutami, o Eterno, mio Dio, salvami secondo la tua benignità,
Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
27 e sappiano essi che questo è opera della tua mano, che sei tu, o Eterno, che l’hai fatto.
Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
28 Essi malediranno, ma tu benedirai; s’innalzeranno e resteran confusi, ma il tuo servitore si rallegrerà.
Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
29 I miei avversari saranno vestiti di vituperio e avvolti nella loro vergogna come in un mantello!
Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
30 Io celebrerò altamente l’Eterno con la mia bocca, lo loderò in mezzo alla moltitudine;
Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
31 poiché egli sta alla destra del povero per salvarlo da quelli che lo condannano a morte.
Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.

< Salmi 109 >