< ヨブ 記 5 >

1 試みに呼んでみよ、だれかあなたに答える者があるか。どの聖者にあなたは頼もうとするのか。
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
2 確かに、憤りは愚かな者を殺し、ねたみはあさはかな者を死なせる。
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
3 わたしは愚かな者の根を張るのを見た、しかしわたしは、にわかにそのすみかをのろった。
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
4 その子らは安きを得ず、町の門でしえたげられても、これを救う者がない。
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
5 その収穫は飢えた人が食べ、いばらの中からさえ、これを奪う。また、かわいた者はその財産をあえぎ求める。
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
6 苦しみは、ちりから起るものでなく、悩みは土から生じるものでない。
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
7 人が生れて悩みを受けるのは、火の子が上に飛ぶにひとしい。
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
8 しかし、わたしであるならば、神に求め、神に、わたしの事をまかせる。
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
9 彼は大いなる事をされるかたで、測り知れない、その不思議なみわざは数えがたい。
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
10 彼は地に雨を降らせ、野に水を送られる。
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
11 彼は低い者を高くあげ、悲しむ者を引き上げて、安全にされる。
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
12 彼は悪賢い者の計りごとを敗られる。それで何事もその手になし遂げることはできない。
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
13 彼は賢い者を、彼ら自身の悪巧みによって捕え、曲った者の計りごとをくつがえされる。
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
14 彼らは昼も、やみに会い、真昼にも、夜のように手探りする。
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
15 彼は貧しい者を彼らの口のつるぎから救い、また強い者の手から救われる。
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
16 それゆえ乏しい者に望みがあり、不義はその口を閉じる。
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
17 見よ、神に戒められる人はさいわいだ。それゆえ全能者の懲しめを軽んじてはならない。
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
18 彼は傷つけ、また包み、撃ち、またその手をもっていやされる。
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
19 彼はあなたを六つの悩みから救い、七つのうちでも、災はあなたに触れることがない。
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
20 ききんの時には、あなたをあがなって、死を免れさせ、いくさの時には、つるぎの力を免れさせられる。
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
21 あなたは舌をもってむち打たれる時にも、おおい隠され、滅びが来る時でも、恐れることはない。
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
22 あなたは滅びと、ききんとを笑い、地の獣をも恐れることはない。
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
23 あなたは野の石と契約を結び、野の獣はあなたと和らぐからである。
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
24 あなたは自分の天幕の安全なことを知り、自分の家畜のおりを見回っても、欠けた物がなく、
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
25 また、あなたの子孫の多くなり、そのすえが地の草のようになるのを知るであろう。
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
26 あなたは高齢に達して墓に入る、あたかも麦束をその季節になって打ち場に運びあげるようになるであろう。
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
27 見よ、われわれの尋ねきわめた所はこのとおりだ。あなたはこれを聞いて、みずから知るがよい」。
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< ヨブ 記 5 >