< 箴言 知恵の泉 1 >

1 ダビデの子、イスラエルの王ソロモンの箴言。
Mithali za Solomoni mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:
2 これは人に知恵と教訓とを知らせ、悟りの言葉をさとらせ、
Kwa kupata hekima na nidhamu; kwa kufahamu maneno ya busara;
3 賢い行いと、正義と公正と公平の教訓をうけさせ、
kwa kujipatia nidhamu na busara, kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;
4 思慮のない者に悟りを与え、若い者に知識と慎みを得させるためである。
huwapa busara wajinga, maarifa na akili kwa vijana;
5 賢い者はこれを聞いて学に進み、さとい者は指導を得る。
wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao, wenye kupambanua na wapate mwongozo;
6 人はこれによって箴言と、たとえと、賢い者の言葉と、そのなぞとを悟る。
kwa kufahamu mithali na mifano, misemo na vitendawili vya wenye hekima.
7 主を恐れることは知識のはじめである、愚かな者は知恵と教訓を軽んじる。
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha maarifa, lakini wapumbavu hudharau hekima na adabu.
8 わが子よ、あなたは父の教訓を聞き、母の教を捨ててはならない。
Mwanangu, sikiliza mwongozo wa baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
9 それらは、あなたの頭の麗しい冠となり、あなたの首の飾りとなるからである。
Hayo yatakuwa taji la maua la neema kichwani pako, na mkufu wa kuipamba shingo yako.
10 わが子よ、悪者があなたを誘っても、それに従ってはならない。
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
11 彼らがあなたに向かって、「一緒に来なさい。われわれは待ち伏せして、人の血を流し、罪のない者を、ゆえなく伏してねらい、
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
12 陰府のように、彼らを生きたままで、のみ尽し、健やかな者を、墓に下る者のようにしよう。 (Sheol h7585)
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni. (Sheol h7585)
13 われわれは、さまざまの尊い貨財を得、奪い取った物で、われわれの家を満たそう。
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
14 あなたもわれわれの仲間に加わりなさい、われわれは共に一つの金袋を持とう」と言っても、
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
15 わが子よ、彼らの仲間になってはならない、あなたの足をとどめて、彼らの道に行ってはならない。
Mwanangu, usiandamane nao. Usiweke mguu wako katika njia zao,
16 彼らの足は悪に走り、血を流すことに速いからだ。
kwa kuwa miguu yao hukimbilia kwenye dhambi, ni wepesi kumwaga damu.
17 すべて鳥の目の前で網を張るのは、むだである。
Tazama ni jinsi gani ilivyo kazi bure kutandaza wavu wakati ndege wote wanakuona!
18 彼らは自分の血を待ち伏せし、自分の命を伏してねらうのだ。
Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!
19 すべて利をむさぼる者の道はこのようなものである。これはその持ち主の命を取り去るのだ。
Huu ndio mwisho wa wote ambao wanajipatia mali kwa hila; huuondoa uhai wa wale wenye mali.
20 知恵は、ちまたに呼ばわり、市場にその声をあげ、
Hekima huita kwa sauti kuu barabarani, hupaza sauti yake kwenye viwanja vikubwa;
21 城壁の頂で叫び、町の門の入口で語る。
kwenye makutano ya barabara za mji zenye makelele mengi hupaza sauti, kwenye malango ya mji hutoa hotuba yake:
22 「思慮のない者たちよ、あなたがたは、いつまで思慮のないことを好むのか。あざける者は、いつまで、あざけり楽しみ、愚かな者は、いつまで、知識を憎むのか。
“Enyi wajinga, mtangʼangʼania ujinga wenu hadi lini? Mpaka lini wenye mizaha watafurahia mizaha, na wapumbavu kuchukia maarifa?
23 わたしの戒めに心をとめよ、見よ、わたしは自分の思いを、あなたがたに告げ、わたしの言葉を、あなたがたに知らせる。
Kama mngekuwa mmeitikia karipio langu, ningekuwa nimemimina roho yangu kwenu na kuwafahamisha maneno yangu.
24 わたしは呼んだが、あなたがたは聞くことを拒み、手を伸べたが、顧みる者はなく、
Lakini kwa kuwa mlinikataa nilipowaita na hakuna yeyote aliyekubali niliponyoosha mkono wangu,
25 かえって、あなたがたはわたしのすべての勧めを捨て、わたしの戒めを受けなかったので、
kwa kuwa mliyapuuza mashauri yangu yote na hamkukubali karipio langu,
26 わたしもまた、あなたがたが災にあう時に、笑い、あなたがたが恐慌にあう時、あざけるであろう。
mimi nami nitawacheka katika maafa yenu, nitawadhihaki wakati janga litawapata:
27 これは恐慌が、あらしのようにあなたがたに臨み、災が、つむじ風のように臨み、悩みと悲しみとが、あなたがたに臨む時である。
wakati janga litawapata kama tufani, wakati maafa yatawazoa kama upepo wa kisulisuli, wakati dhiki na taabu zitawalemea.
28 その時、彼らはわたしを呼ぶであろう、しかし、わたしは答えない。ひたすら、わたしを求めるであろう、しかし、わたしに会えない。
“Ndipo watakaponiita lakini sitawajibu; watanitafuta lakini hawatanipata.
29 彼らは知識を憎み、主を恐れることを選ばず、
Kwa kuwa walichukia maarifa, wala hawakuchagua kumcha Bwana,
30 わたしの勧めに従わず、すべての戒めを軽んじたゆえ、
kwa kuwa hawakukubali mashauri yangu, na kukataa maonyo yangu,
31 自分の行いの実を食らい、自分の計りごとに飽きる。
watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa matunda ya hila zao.
32 思慮のない者の不従順はおのれを殺し、愚かな者の安楽はおのれを滅ぼす。
Kwa kuwa ukaidi wa wajinga utawaua, nako kuridhika kwa wajinga kutawaangamiza.
33 しかし、わたしに聞き従う者は安らかに住まい、災に会う恐れもなく、安全である」。
Lakini yeyote anisikilizaye ataishi kwa usalama, atatulia, bila kuwa na hofu ya madhara.”

< 箴言 知恵の泉 1 >