< 詩篇 147 >

1 主をほめたたえよ。われらの神をほめうたうことはよいことである。主は恵みふかい。さんびはふさわしいことである。
Msifuni Bwana. Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa, jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
2 主はエルサレムを築き、イスラエルの追いやられた者を集められる。
Bwana hujenga Yerusalemu, huwakusanya Israeli walio uhamishoni.
3 主は心の打ち砕かれた者をいやし、その傷を包まれる。
Anawaponya waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.
4 主はもろもろの星の数を定め、すべてそれに名を与えられる。
Huzihesabu nyota na huipa kila moja jina lake.
5 われらの主は大いなる神、力も豊かであって、その知恵ははかりがたい。
Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.
6 主はしえたげられた者をささえ、悪しき者を地に投げ捨てられる。
Bwana huwahifadhi wanyenyekevu lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.
7 主に感謝して歌え、琴にあわせてわれらの神をほめうたえ。
Mwimbieni Bwana kwa shukrani, mpigieni Mungu wetu kinubi.
8 主は雲をもって天をおおい、地のために雨を備え、もろもろの山に草をはえさせ、
Yeye huzifunika anga kwa mawingu, huinyeshea ardhi mvua, na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.
9 食物を獣に与え、また鳴く小がらすに与えられる。
Huwapa chakula mifugo na pia makinda ya kunguru yanapolia.
10 主は馬の力を喜ばれず、人の足をよみせられない。
Furaha yake haipo katika nguvu za farasi, wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.
11 主はおのれを恐れる者とそのいつくしみを望む者とをよみせられる。
Bwana hupendezwa na wale wamchao, wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.
12 エルサレムよ、主をほめたたえよ。シオンよ、あなたの神をほめたたえよ。
Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu, msifu Mungu wako, ee Sayuni,
13 主はあなたの門の貫の木を堅くし、あなたのうちにいる子らを祝福されるからである。
kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.
14 主はあなたの国境を安らかにし、最も良い麦をもってあなたを飽かせられる。
Huwapa amani mipakani mwenu na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
15 主はその戒めを地に下される。そのみ言葉はすみやかに走る。
Hutuma amri yake duniani, neno lake hukimbia kasi.
16 主は雪を羊の毛のように降らせ、霜を灰のようにまかれる。
Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
17 主は氷をパンくずのように投げうたれる。だれがその寒さに耐えることができましょうか。
Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
18 主はみ言葉を下してこれを溶かし、その風を吹かせられると、もろもろの水は流れる。
Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
19 主はそのみ言葉をヤコブに示し、そのもろもろの定めと、おきてとをイスラエルに示される。
Amemfunulia Yakobo neno lake, sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
20 主はいずれの国民をも、このようにはあしらわれなかった。彼らは主のもろもろのおきてを知らない。主をほめたたえよ。
Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote, hawazijui sheria zake. Msifuni Bwana.

< 詩篇 147 >