< 詩篇 85 >

1 聖歌隊の指揮者によってうたわせたコラの子の歌 主よ、あなたはみ国にめぐみを示し、ヤコブの繁栄を回復されました。
Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2 あなたはその民の不義をゆるし、彼らの罪をことごとくおおわれました。 (セラ)
Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
3 あなたはすべての怒りを捨て、激しい憤りを遠ざけられました。
Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4 われらの救の神よ、われらを回復し、われらに対するあなたの憤りをおやめください。
Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
5 あなたはとこしえにわれらを怒り、よろずよまで、あなたの怒りを延ばされるのですか。
Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
6 あなたの民が、あなたによって喜びを得るため、われらを再び生かされないのですか。
Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
7 主よ、あなたのいつくしみをわれらに示し、あなたの救をわれらに与えてください。
Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
8 わたしは主なる神の語られることを聞きましょう。主はその民、その聖徒、ならびにその心を主に向ける者に、平和を語られるからです。
Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
9 まことに、その救は神を恐れる者に近く、その栄光はわれらの国にとどまるでしょう。
Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
10 いつくしみと、まこととは共に会い、義と平和とは互に口づけし、
Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
11 まことは地からはえ、義は天から見おろすでしょう。
Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
12 主が良い物を与えられるので、われらの国はその産物を出し、
Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
13 義は主のみ前に行き、その足跡を道とするでしょう。
Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.

< 詩篇 85 >