< Exodus 40 >

1 locutusque est Dominus ad Mosen dicens
Kisha Yahweh akasema na Musa na kumwambia,
2 mense primo die prima mensis eriges tabernaculum testimonii
“Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka lazima wewe uandae hema la kukutania.
3 et pones in eo arcam dimittesque ante illam velum
Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake, na utaziba sanduku kwa pazia.
4 et inlata mensa pones super eam quae rite praecepta sunt candelabrum stabit cum lucernis suis
Utaleta ndani meza na kuandaa kwa mpangilio vitu vyake. Kisha utaleta kinara cha taa na kuandaa taa.
5 et altare aureum in quo adoletur incensum coram arca testimonii tentorium in introitu tabernaculi pones
Nawe utaweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba mbele ya sanduku la ushuhuda, na utaweka pazia katika mwingilio wa hema la kukutania.
6 et ante illud altare holocausti
Utaweka madhabahu kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa mbele ya mwingilio wa hema ya kukutania.
7 labrum inter altare et tabernaculum quod implebis aqua
Utaweka ile saani kubwa katikati ya hema la kukutania na madhabahu na utaweka maji ndani yake.
8 circumdabisque atrium tentoriis et ingressum eius
Uandae nyuani inayoizunguka, na utundike pazia katika mwingilio wa nyuani.
9 et adsumpto unctionis oleo ungues tabernaculum cum vasis suis ut sanctificentur
Lazima uchukuwe mafuta ya upako na upake hema la kukutania na kila kitu kilichopo ndani yake. Lazima uitenge na samani zake kwangu; kisha itakuwa takatifu.
10 altare holocausti et omnia vasa eius
Lazima upake mafuta madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa na vyombo vyake. Lazima utenge madhabhu kwa ajili yangu na itakuwa takatifu kwangu.
11 labrum cum basi sua omnia unctionis oleo consecrabis ut sint sancta sanctorum
Upake mafuta beseni la shaba na sakafu yake na uitenge kwa ajili yangu.
12 adplicabisque Aaron et filios eius ad fores tabernaculi testimonii et lotos aqua
Umlete Aruni na wanae kwa mwingilio wa hema la kukutania na uwaoshe wote kwa maji.
Utamfunika Aruni kwa mavazi yaliyo tengwa kwa ajili yangu, mpake mafuta na umtenge ili anitumikie kama kuhani.
Utawaleta wana wake na kuwafunika kwa nguo nzito.
15 indues sanctis vestibus ut ministrent mihi et unctio eorum in sacerdotium proficiat sempiternum
Utawapaka mafuta kama ulivyo mpaka baba yao ili wanitumikie kama makuhani. Upako wao utawafanya makuhani wa kudumu vizazi vyote vya watu wao.”
16 fecitque Moses omnia quae praeceperat Dominus
Hivi ndivyo Musa alivyo sema; alifuata yote Yahweh aliyo muamuru. Alifanya vitu vyote hivi.
17 igitur mense primo anni secundi in prima die mensis conlocatum est tabernaculum
Hivyo hema la kukutania liliandaliwa siku ya kwanza ya mwezi wa mwaka wa pili.
18 erexitque illud Moses et posuit tabulas ac bases et vectes statuitque columnas
Musa alianda hema la kukutania, akaeka sakafu zake sehemu yake, akaanda fremu zake, akashikisha chuma zake, na akaanda minara na nguzo zake.
19 et expandit tectum super tabernaculum inposito desuper operimento sicut Dominus imperarat
Alitandaza mfuniko juu ya hema la kukutania na kuweka hema juu yake, kama Yahweh alivyo muamuru.
20 posuit et testimonium in arca subditis infra vectibus et oraculum desuper
Alichukuwa amri za agano na kuweka kwenye sanduku. Pia aliweka nguzo kwenye sanduku na kuweka mfuniko wa kiti cha rehema.
21 cumque intulisset arcam in tabernaculum adpendit ante eam velum ut expleret Domini iussionem
Aliichukuwa sanduku na kuweka ndani ya hema la kukutania. Aliandaa pazia ili lizibe sanduku la ushuhuda, kama Yahweh alivyo muamuru.
22 posuit et mensam in tabernaculo testimonii ad plagam septentrionalem extra velum
Alieka meza kwenye hema la kukutania, kwa upande wa kaskazini mwa hema la kukutania, nje ya pazia.
23 ordinatis coram propositionis panibus sicut praeceperat Dominus Mosi
Alieka mkate kwa mpangilio katika meza ya Yahweh, kama Yahweh alivyo amuru.
24 posuit et candelabrum in tabernaculum testimonii e regione mensae in parte australi
Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania, upande wa pili wa meza, kusini mwa hema la kukutani.
25 locatis per ordinem lucernis iuxta praeceptum Domini
Aliwasha taa mbele za Yahweh, kama Yahweh alivyo muamuru.
26 posuit et altare aureum sub tecto testimonii contra velum
Aliweka madhabahu ya dhahabu ya uvumba ndani ya hema la kukutania mbele ya pazia.
27 et adolevit super eo incensum aromatum sicut iusserat Dominus
Alichoma uvumba wa manukato hapo, kama Yahweh alivyo muamuru.
28 posuit et tentorium in introitu tabernaculi
Alitundika pazia katika hema ya kukutania.
29 et altare holocausti in vestibulo testimonii offerens in eo holocaustum et sacrificia ut Dominus imperarat
Aliweka madhabahu ya sadaka ya kuteketeza katika hema ya kukutania. Aliitolea sadaka ya kuteketeza na sadaka ya unga, kama Yahweh alivyo muamuru.
30 labrum quoque statuit inter tabernaculum testimonii et altare implens illud aqua
Aliweka beseni katikati ya hema ya kukutunia na madhabahu, na maji ya kuoshea.
31 laveruntque Moses et Aaron ac filii eius manus suas et pedes
Musa, Aruni, na wanae waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni
32 cum ingrederentur tectum foederis et accederent ad altare sicut praeceperat Dominus
muda wowote walipoenda kwenye hema ya kukutania na muda wowote walipoenda kwenye madhabahu. Walijisafisha, kama Yahweh alivyo muamuru Musa.
33 erexit et atrium per gyrum tabernaculi et altaris ducto in introitu eius tentorio postquam cuncta perfecta sunt
Musa alianda nyuani nyuma ya hema ya kukutania na madhabahu. Alianda pazia katika mwingilio wa nyuani. Katika hili, Musa alimaliza kazi.
34 operuit nubes tabernaculum testimonii et gloria Domini implevit illud
Kisha wingu likafunika hema ya kukutania, na utukufu wa Yahweh ukafunika hema ya kukutania.
35 nec poterat Moses ingredi tectum foederis nube operiente omnia et maiestate Domini coruscante quia cuncta nubes operuerat
Musa hakuweza kuingia hema ya kukutania kwasababu wingu lilikuwa juu yake, na kwasababu utukufu wa Yahweh ulijaza hema ya kukutania.
36 si quando nubes tabernaculum deserebat proficiscebantur filii Israhel per turmas suas
Muda wowote wingu lilipo chukuliwa juu kutoka hema ya kukutania, watu wa Israeli waliendelea na safari yao.
37 si pendebat desuper manebant in eodem loco
Lakini kama wingu haliku nyanyuka juu kutoka hema ya kukutania, kisha basi watu hawaku safiri. Walibaki hadi siku lilipo nyanyuliwa juu.
38 nubes quippe Domini incubabat per diem tabernaculo et ignis in nocte videntibus populis Israhel per cunctas mansiones suas
Kwa kuwa wingu la Yahweh lilikuwa juu ya hema ya kukutania mchana, na moto wake ulikuwa juu yake usiku, wazi kwa watu wote wa Israeli kipindi chote cha safari yao.

< Exodus 40 >