< Psalmorum 107 >

1 alleluia confitemini Domino quoniam bonus quoniam in saeculum misericordia eius
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 dicant qui redempti sunt a Domino quos redemit de manu inimici de regionibus congregavit eos
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 a solis ortu et occasu et ab aquilone et mari
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 erraverunt in solitudine in inaquoso viam civitatis habitaculi non invenerunt
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 esurientes et sitientes anima eorum in ipsis defecit
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur et de necessitatibus eorum eripuit eos
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 et deduxit eos in viam rectam ut irent in civitatem habitationis
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 confiteantur Domino misericordiae eius et mirabilia eius filiis hominum
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 quia satiavit animam inanem et animam esurientem satiavit bonis
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 sedentes in tenebris et umbra mortis vinctos in mendicitate et ferro
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 quia exacerbaverunt eloquia Dei et consilium Altissimi inritaverunt
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 et humiliatum est in laboribus cor eorum infirmati sunt nec fuit qui adiuvaret
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur et de necessitatibus eorum liberavit eos
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 et eduxit eos de tenebris et umbra mortis et vincula eorum disrupit
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 confiteantur Domino misericordiae eius et mirabilia eius filiis hominum
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 quia contrivit portas aereas et vectes ferreos confregit
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 suscepit eos de via iniquitatis eorum propter iniustitias enim suas humiliati sunt
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 omnem escam abominata est anima eorum et adpropinquaverunt usque ad portas mortis
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur et de necessitatibus eorum liberavit eos
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 misit verbum suum et sanavit eos et eripuit eos de interitionibus eorum
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 confiteantur Domino misericordiae eius et mirabilia eius filiis hominum
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 et sacrificent sacrificium laudis et adnuntient opera eius in exultatione
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 qui descendunt mare in navibus facientes operationem in aquis multis
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 ipsi viderunt opera Domini et mirabilia eius in profundo
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 dixit et stetit spiritus procellae et exaltati sunt fluctus eius
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 ascendunt usque ad caelos et descendunt usque ad abyssos anima eorum in malis tabescebat
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 turbati sunt et moti sunt sicut ebrius et omnis sapientia eorum devorata est
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 et clamaverunt ad Dominum cum tribularentur et de necessitatibus eorum eduxit eos
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 et statuit procellam eius in auram et siluerunt fluctus eius
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 et laetati sunt quia siluerunt et deduxit eos in portum voluntatis eorum
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 confiteantur Domino misericordiae eius et mirabilia eius filiis hominum
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 exaltent eum in ecclesia plebis et in cathedra seniorum laudent eum
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 posuit flumina in desertum et exitus aquarum in sitim
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 terram fructiferam in salsuginem a malitia inhabitantium in ea
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 posuit desertum in stagna aquarum et terram sine aqua in exitus aquarum
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 et conlocavit illic esurientes et constituerunt civitatem habitationis
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 et seminaverunt agros et plantaverunt vineas et fecerunt fructum nativitatis
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 et benedixit eis et multiplicati sunt nimis et iumenta eorum non minoravit
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 et pauci facti sunt et vexati sunt a tribulatione malorum et dolore
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 effusa est contemptio super principes et errare fecit eos in invio et non in via
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 et adiuvit pauperem de inopia et posuit sicut oves familias
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 videbunt recti et laetabuntur et omnis iniquitas oppilabit os suum
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 quis sapiens et custodiet haec et intellegent misericordias Domini
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Psalmorum 107 >