< Psalmorum 135 >

1 alleluia laudate nomen Domini laudate servi Dominum
Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
2 qui statis in domo Domini in atriis domus Dei nostri
ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 laudate Dominum quia bonus Dominus psallite nomini eius quoniam suave
Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4 quoniam Iacob elegit sibi Dominus Israhel in possessionem sibi
Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5 quia ego cognovi quod magnus est Dominus et Deus noster prae omnibus diis
Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6 omnia quae voluit Dominus fecit in caelo et in terra in mare et in omnibus abyssis
Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7 educens nubes ab extremo terrae fulgora in pluviam fecit qui producit ventos de thesauris suis
Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8 qui percussit primogenita Aegypti ab homine usque ad pecus
Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9 emisit signa et prodigia in medio tui Aegypte in Pharaonem et in omnes servos eius
Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10 qui percussit gentes multas et occidit reges fortes
Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11 Seon regem Amorreorum et Og regem Basan et omnia regna Chanaan
Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12 et dedit terram eorum hereditatem hereditatem Israhel populo suo
Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
13 Domine nomen tuum in aeternum Domine memoriale tuum in generationem et generationem
Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
14 quia iudicabit Dominus populum suum et in servis suis deprecabitur
Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
15 simulacra gentium argentum et aurum opera manuum hominum
Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
16 os habent et non loquentur oculos habent et non videbunt
Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
17 aures habent et non audient neque enim est spiritus in ore eorum
zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
18 similes illis fiant qui faciunt ea et omnes qui sperant in eis
Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
19 domus Israhel benedicite Domino domus Aaron benedicite Domino
Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
20 domus Levi benedicite Domino qui timetis Dominum benedicite Domino
Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
21 benedictus Dominus ex Sion qui habitat in Hierusalem
Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.

< Psalmorum 135 >