< Pāvila 1. Vēstule Korintiešiem 11 >

1 Dzenaties man pakaļ, tā kā es Kristum.
Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.
2 Un es jūs slavēju, brāļi, ka jūs visās lietās mani pieminat un turat tās mācības, kā jums tās esmu mācījis.
Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.
3 Bet es gribu, ka jūs zināt, ka ikkatra vīra galva ir Kristus, bet sievas galva ir vīrs, bet Kristus galva ir Dievs.
Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.
4 Ikviens vīrs, kas Dievu lūgdams vai mācīdams apsegu tur uz galvas, apkauno savu galvu.
Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.
5 Bet ikviena sieva ar neapsegtu galvu Dievu lūgdama vai mācīdama, apkauno savu galvu. Jo tas tikpat, tā kā tā būtu apcirpta.
Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.
6 Jo ja sieva neapsedzās, tad lai tā arī top apcirpta. Bet kad nu tas sievai par kaunu, ka tā ir apcirpta jeb plikgalve, tad lai tā apsedzās.
Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.
7 Bet vīram nebūs galvu apsegt, jo viņš ir Dieva ģīmis un gods; bet sieva ir vīra gods.
Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.
8 Jo vīrs nav no sievas, bet sieva no vīra.
Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.
9 Un vīrs arī nav radīts sievas dēļ, bet sieva vīra dēļ.
Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.
10 Tāpēc sievai būs valdnieka zīmi galvā turēt eņģeļu dēļ.
Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.
11 Tomēr nedz vīrs ir bez sievas, nedz sieva bez vīra iekš Tā Kunga.
Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.
12 Jo tā kā sieva ir no vīra, tāpat arī vīrs ir caur sievu; bet viss tas ir no Dieva.
Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.
13 Spriežat paši, vai pieklājās, ka sieva Dievu lūdz neapsegta?
Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?
14 Jeb vai pati daba jums nemāca, ka tas vīram par negodu, kad tam gari mati,
Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?
15 Bet ja sievai gari mati: tad tas viņai par godu; jo mati viņai doti par apsegu.
Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.
16 Bet ja kāds grib par to tiepties: mums tāda ieraduma nav, nedz Dieva draudzēm.
Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.
17 Es jūs pamācu un to nevaru uzteikt, ka jūs sanākat ne par svētību, bet par nesvētību.
Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.
18 Jo pirmā kārtā, kad jūs sanākat draudzē, es dzirdu, ka šķelšanās ir jūsu starpā, un pa daļai to gan ticu.
Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.
19 Jo šķelšanām gan vajag būt jūsu starpā, lai tie pastāvīgie jūsu starpā top zināmi.
Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.
20 Kad nu jūs sanākat kopā, tad tā nenotiek, kā pieklājās baudīt Tā Kunga mielastu.
Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,
21 Jo pie mielasta ikviens steidzās paņemt savu paša ēdienu un cits paliek neēdis un cits ir pilns.
kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.
22 Jo vai tad jums nav māju, kur varat ēst un dzert? Jeb vai jūs Dieva draudzi nicinājiet un tos apkaunojiet, kam nav nekā? Ko lai jums saku? Vai lai jūs teicu? Šinī lietā es jūs neteicu.
Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!
23 Jo no Tā Kunga es to esmu dabūjis, ko atkal jums esmu mācījis, ka Tas Kungs Jēzus tanī naktī, kad Tas kļuva nodots, to maizi ņēma,
Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,
24 Un pateicies pārlauza un sacīja: ņemiet, ēdiet, tā ir Mana miesa, kas par jums top lauzta; to dariet Mani pieminēdami.
naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”
25 Tāpat arī to biķeri, pēc tā vakarēdiena, sacīdams: Šis biķeris ir tā jaunā derība iekš Manām asinīm. To dariet, cikkārt jūs to dzeriet, Mani pieminēdami.
Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”
26 Jo cikkārt jūs no šīs maizes ēdat un no šī biķera dzerat, tad pasludinājiet Tā Kunga nāvi, tiekams Tas nāk.
Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.
27 Tad nu, kas necienīgi ēd šo maizi, vai dzer Tā Kunga biķeri, tas būs noziedzīgs pie Tā Kunga miesas un asinīm.
Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.
28 Bet lai cilvēks pats izmeklējās, un tā lai viņš ēd no šīs maizes un dzer no šī biķera.
Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.
29 Jo kas necienīgi ēd un dzer, tas ēd un dzer sev pašam sodu, neizšķirdams Tā Kunga miesu.
Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.
30 Tādēļ jūsu starpā daudz ir vāji un neveseli, un daudz ir aizmiguši (garīgi, iekš draudzes).
Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.
31 Jo ja mēs paši sevi tiesātu, tad netaptu tiesāti.
Lakini kama tungejichunguza wenyewe tusingehukumiwa.
32 Bet kad mēs topam tiesāti, tad no Tā Kunga topam pārmācīti, lai ar pasauli netopam pazudināti.
Tunapohukumiwa na Bwana, tunaadibishwa ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33 Tad nu, mani brāļi, kad jūs sanākat pie mielasta, tad gaidiet cits uz citu.
Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo pamoja ili kula, mngojane.
34 Bet ja kas ir izsalcis, tas lai ēd mājās, lai jūs nesanākat par sodu. To citu es mācīšu, kad es nākšu.
Kama mtu akiwa na njaa, ale nyumbani kwake ili mkutanapo pamoja msije mkahukumiwa. Nami nitakapokuja nitawapa maelekezo zaidi.

< Pāvila 1. Vēstule Korintiešiem 11 >