< حزقیال 9 >

و او به آواز بلند به گوش من ندا کرده، گفت: «وکلای شهر را نزدیک بیاور و هرکس آلت خراب کننده خود را در دست خود بدارد.» ۱ 1
Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
و اینک شش مرد از راه دروازه بالایی که بطرف شمال متوجه است آمدند و هرکس تبرخود را در دستش داشت. و در میان ایشان یک مرد ملبس شده به کتان بود و دوات کاتب درکمرش. و ایشان داخل شده، نزد مذبح برنجین ایستادند. ۲ 2
Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
و جلال خدای اسرائیل از روی آن کروبی که بالای آن بود به آستانه خانه برآمد و به آن مردی که به کتان ملبس بود و دوات کاتب را درکمر داشت خطاب کرد. ۳ 3
Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
و خداوند به او گفت: «از میان شهر یعنی از میان اورشلیم بگذر و برپیشانی کسانی که به‌سبب همه رجاساتی که در آن کرده می‌شود آه و ناله می‌کنند نشانی بگذار. ۴ 4
akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
و به آنان به سمع من گفت که در عقب او از شهربگذرید و هلاک سازید و چشمان شما شفقت نکند و ترحم منمایید. ۵ 5
Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
پیران و جوانان و دختران و اطفال و زنان را تمام به قتل رسانید، اما به هرکسی‌که این نشان را دارد نزدیک مشوید و ازقدس من شروع کنید.» پس از مردان پیری که پیش خانه بودند شروع کردند. ۶ 6
Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
و به ایشان فرمود: «خانه را نجس سازید وصحنها را از کشتگان پر ساخته، بیرون آیید.» پس بیرون آمدند و در شهر به کشتن شروع کردند. ۷ 7
Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
وچون ایشان می‌کشتند و من باقی‌مانده بودم به روی خود در‌افتاده، استغاثه نمودم و گفتم: «آه‌ای خداوند یهوه آیا چون غضب خود را براورشلیم می‌ریزی تمامی بقیه اسرائیل را هلاک خواهی ساخت؟» ۸ 8
Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
او مرا جواب داد: «گناه خاندان اسرائیل و یهودا بی‌نهایت عظیم است وزمین از خون مملو و شهر از ستم پر است. زیرامی گویند: خداوند زمین را ترک کرده است وخداوند نمی بیند. ۹ 9
Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
پس چشم من نیز شفقت نخواهد کرد و من رحمت نخواهم فرمود، بلکه رفتار ایشان را بر سر ایشان خواهم آورد.» ۱۰ 10
Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
واینک آن مردی که به کتان ملبس بود و دوات را درکمر داشت، جواب داد و گفت: «به نهجی که مراامر فرمودی عمل نمودم.» ۱۱ 11
Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”

< حزقیال 9 >