< مکاشفهٔ یوحنا 19 >

و بعد از آن شنیدم چون آوازی بلند ازگروهی کثیر در آسمان که می‌گفتند: «هللویاه! نجات و جلال و اکرام و قوت از آن خدای ما است، ۱ 1
Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
زیرا که احکام او راست و عدل است، چونکه داوری نمود بر فاحشه بزرگ که جهان را به زنای خود فاسد می‌گردانید و انتقام خون بندگان خود را از دست او کشید.» ۲ 2
kwa maana hukumu zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”
و بار دیگر گفتند: «هللویاه، و دودش تاابدالاباد بالا می‌رود!» (aiōn g165) ۳ 3
Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn g165)
و آن بیست و چهار پیر و چهار حیوان به روی درافتاده، خدایی را که بر تخت نشسته است سجده نمودند و گفتند: «آمین، هللویاه!» ۴ 4
Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: “Amen, Haleluya!”
و آوازی از تخت بیرون آمده، گفت: «حمدنمایید خدای ما را‌ای تمامی بندگان او وترسندگان او چه کبیر و چه صغیر.» ۵ 5
Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: “Msifuni Mungu wetu, ninyi watumishi wake wote, ninyi nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa!”
و شنیدم چون آواز جمعی کثیر و چون آوازآبهای فراوان و چون آواز رعدهای شدید که می‌گفتند: «هللویاه، زیرا خداوند خدای ما قادرمطلق، سلطنت گرفته است. ۶ 6
Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.
شادی و وجدنماییم و او را تمجید کنیم زیرا که نکاح بره رسیده است و عروس او خود را حاضر ساخته است. ۷ 7
Tufurahi, tushangilie na kumpa utukufu! Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia na bibi arusi wake amejiweka tayari.
وبه او داده شد که به کتان، پاک و روشن خود رابپوشاند، زیرا که آن کتان عدالتهای مقدسین است.» ۸ 8
Akapewa kitani safi, nyeupe inayongʼaa, ili avae.” (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)
و مرا گفت: «بنویس: خوشابحال آنانی که به بزم نکاح بره دعوت شده‌اند.» و نیز مرا گفت که «این است کلام راست خدا.» ۹ 9
Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”
و نزد پایهایش افتادم تا او را سجده کنم. اوبه من گفت: «زنهار چنین نکنی زیرا که من با توهمخدمت هستم و با برادرانت که شهادت عیسی را دارند. خدا را سجده کن زیرا که شهادت عیسی روح نبوت است.» ۱۰ 10
Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”
و دیدم آسمان را گشوده و ناگاه اسبی سفیدکه سوارش امین و حق نام دارد و به عدل داوری وجنگ می‌نماید، ۱۱ 11
Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita.
و چشمانش چون شعله آتش و بر سرش افسرهای بسیار و اسمی مرقوم داردکه جز خودش هیچ‌کس آن را نمی داند. ۱۲ 12
Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe.
وجامه‌ای خون آلود دربر دارد و نام او را «کلمه خدا» می‌خوانند. ۱۳ 13
Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.”
و لشکرهایی که درآسمانند، بر اسبهای سفید و به کتان سفید و پاک ملبس از عقب او می‌آمدند. ۱۴ 14
Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri.
و از دهانش شمشیری تیز بیرون می‌آید تا به آن امت‌ها را بزندو آنها را به عصای آهنین حکمرانی خواهد نمودو او چرخشت خمر غضب و خشم خدای قادرمطلق را زیر پای خود می‌افشرد. ۱۵ 15
Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi.
و بر لباس وران او نامی مرقوم است یعنی «پادشاه پادشاهان ورب‌الارباب». ۱۶ 16
Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
و دیدم فرشته‌ای را در آفتاب ایستاده که به آواز بلند تمامی مرغانی را که در آسمان پروازمی کنند، ندا کرده، می‌گوید: «بیایید و بجهت ضیافت عظیم خدا فراهم شوید. ۱۷ 17
Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu,
تا بخورید گوشت پادشاهان و گوشت سپه سالاران و گوشت جباران و گوشت اسبها و سواران آنها و گوشت همگان را، چه آزاد و چه غلام، چه صغیر و چه کبیر.» ۱۸ 18
ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”
و دیدم وحش و پادشاهان زمین ولشکرهای ایشان را که جمع شده بودند تا بااسب‌سوار و لشکر او جنگ کنند. ۱۹ 19
Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake.
و وحش گرفتار شد و نبی کاذب با وی که پیش او معجزات ظاهر می‌کرد تا به آنها آنانی را که نشان وحش رادارند و صورت او را می‌پرستند، گمراه کند. این هر دو، زنده به دریاچه آتش افروخته شده به کبریت انداخته شدند. (Limnē Pyr g3041 g4442) ۲۰ 20
Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr g3041 g4442)
و باقیان به شمشیری که از دهان اسب‌سوار بیرون می‌آمد کشته شدند وتمامی مرغان از گوشت ایشان سیر گردیدند. ۲۱ 21
Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.

< مکاشفهٔ یوحنا 19 >