< II Samuela 20 >

1 Tedy się tam pojawił mąż niepobożny, którego zwano Seba, syn Bichry, mąż Jemini. Ten zatrąbił w trąbę, i rzekł: Nie mamy my działu w Dawidzie, ani mamy dziedzictwa w synu Isajego; wróć się każdy do namiotów swoich, o Izraelu!
Basi, kulikuwa na mtu mbaya sana aliyeitwa Sheba mwana wa Bikri, Mbenyamini, aliyekuwako huko. Akapiga tarumbeta na kupaza sauti, “Hatuna fungu katika Daudi, wala hatuna sehemu katika mwana wa Yese! Kila mtu aende hemani mwake, enyi Israeli!”
2 A tak odstąpili wszyscy mężowie Izraelscy od Dawida za Sebą, synem Bichry; ale mężowie Judzcy trzymali się króla swego, od Jordanu aż do Jeruzalemu.
Kwa hiyo watu wote wa Israeli wakamwacha Daudi na kumfuata Sheba mwana Bikri. Lakini watu wa Yuda wakawa karibu na mfalme wao katika safari yote kutoka Yordani mpaka Yerusalemu.
3 I przyszedł Dawid do domu swego w Jeruzalemie; a wziąwszy król dziesięć niewiast założnic, które był zostawił, aby strzegły domu, oddał je pod straż, i żywił je, ale do nich nie wchodził; i były pod strażą aż do dnia śmierci swojej, we wdowim stanie.
Daudi aliporudi katika jumba lake la kifalme huko Yerusalemu, aliwachukua wale masuria kumi aliokuwa amewaacha ili kuangalia jumba la kifalme na kuwaweka ndani ya nyumba chini ya ulinzi. Akawapa mahitaji yao lakini hakukutana nao kimwili. Waliwekwa kifungoni wakaishi kama wajane mpaka kifo chao.
4 Potem rzekł król do Amazy: Zbierz mi męże Judzkie za trzy dni; ty się też tu staw.
Ndipo mfalme akamwambia Amasa, “Waite watu wa Yuda waje kwangu katika muda wa siku tatu, nawe mwenyewe uwepo hapa.”
5 A tak poszedł Amaza, aby zebrał lud Judzki; lecz się zabawił nad czas naznaczony, który mu był naznaczył.
Lakini Amasa alipokwenda kuwaita Yuda, alichukua muda mrefu zaidi ya ule mfalme aliokuwa amemwekea.
6 I rzekł Dawid do Abisajego: Teraz gorzej nam uczyni Seba, syn Bichry, niż Absalom; przetoż ty weźmij sługi pana twego, a goń go, by snać nie znalazł sobie miast obronnych, i nie uszedł z oczu naszych.
Daudi akamwambia Abishai, “Sasa Sheba mwana wa Bikri atatuletea madhara zaidi kuliko alivyofanya Absalomu. Wachukue watu wa bwana wako na umfuatie, la sivyo atapata mji wenye ngome na kututoroka.”
7 Tedy wyszli z nim mężowie Joabowi, i Chertczycy i Feletczycy, i wszystko rycerstwo, a wyszli z Jeruzalemu w pogoń za Sebą, synem Bichry.
Hivyo watu wa Yoabu, na Wakerethi na Wapelethi, pamoja na wapiganaji mashujaa wote wakaondoka chini ya uongozi wa Abishai. Wakatoka Yerusalemu ili kumfuata Sheba mwana wa Bikri.
8 A gdy byli u wielkiego kamienia, który jest w Gabaon, tedy im Amaza zabieżał. A Joab miał przepasaną szatę swą, w której chodził, a na niej pas z mieczem przypasany do biódr swoich w pochwach swych, którego snadnie mógł dobyć, i zaś schować.
Wakati walikuwa kwenye mwamba mkubwa huko Gibeoni, Amasa alikuja kuwalaki. Yoabu alikuwa amevaa mavazi yake ya kijeshi; juu yake alifunga mkanda kwenye kiuno wenye upanga ndani ya ala. Alipokuwa akienda mbele, ule upanga ukaanguka kutoka kwenye ala.
9 I rzekł Joab do Amazy: Jakoż się masz, bracie mój? I ujął ręką prawą Joab Amazę za brodę, jakoby go całować miał.
Yoabu akamwambia Amasa, “U hali gani, ndugu yangu?” Kisha Yoabu akamshika Amasa ndevu kwa mkono wake wa kuume ili ambusu.
10 Ale Amaza nie postrzegł miecza, który był w ręce Joabowej: i przebił go nim pod piąte żebro, i wylał trzewa jego na ziemię, a tak za jadną raną umarł. A Joab i Abisaj, brat jego, szli w pogoń za Sebą, synem Bichry.
Amasa hakuona upanga uliokuwa mkononi mwa Yoabu, naye Yoabu akamchoma nao tumboni, nayo matumbo yake yakamwagika chini. Pasipo kuchomwa mara ya pili, Amasa akafa. Basi Yoabu na Abishai nduguye wakamfuatia Sheba mwana wa Bikri.
11 Tedy stanął jeden nad nim z sług Joabowych, i rzekł: Ktokolwiek jest życzliwy Joabowi, a ktokolwiek trzyma z Dawidem, niech idzie za Joabem.
Mmoja wa watu wa Yoabu akasimama kando ya Amasa, akasema, “Yeyote ampendaye Yoabu na yeyote aliye upande wa Daudi, na amfuate Yoabu!”
12 Lecz Amaza walał się w krwi w pośród drogi. A widząc on mąż, iż się zastanawiał wszystek lud nad nim, zwlekł Amazę z drogi na pole, i przyrzucił go szatą, gdyż widział, że ktokolwiek szedł mimo niego, zastanawiał się.
Amasa alikuwa akigaagaa katika damu yake katikati ya barabara; mtu mmoja akaona kwamba vikosi vyote vilikuwa vinasimama pale. Huyo mtu alipotambua kwamba kila aliyefika pale Amasa alipokuwa alisimama, alimburuta Amasa kutoka barabarani mpaka kwenye shamba na kutupia nguo juu yake.
13 A gdy był zwleczony z drogi, bieżał każdy mąż za Joabem, goniąc Sebę, syna Bichry.
Baada ya Amasa kuondolewa kutoka barabarani, watu wote walienda pamoja na Yoabu kumfuatia Sheba mwana wa Bikri.
14 Który już był przeszedł przez wszystkie pokolenia Izraelskie, aż do Abel i Betmaacha, ze wszystkimi Berymczykami, którzy się też byli zebrali, a szli za nim.
Sheba akapita katika makabila yote ya Israeli hadi Abel-Beth-Maaka na kupitia eneo lote la Waberi ambao walijikusanya pamoja na kumfuata.
15 A gdy się tam ściągnęli, oblegli go w Abeli Betmaacha, i usypali szańce przeciw miastu, tak iż stali przed murem, a wszystek lud, który był z Joabem, usiłował obalić mury.
Vikosi vyote vya Yoabu vikaja na kumhusuru Sheba mwana wa Bikri huko Abel-Beth-Maaka. Wakauzingira mji kwa kuweka vikosi vya askari, ili kukabiliana na ngome ya mji. Walipokuwa wanagongagonga ukuta ili kuubomoa na kuuangusha chini,
16 Wtem zawołała z miasta niektóra niewiasta mądra: Słuchajcie, słuchajcie! rzeczcie proszę do Joaba: Przystąp sam, a rozmówię się z tobą.
mwanamke mmoja mwenye busara akaita kutoka ndani ya mji, akisema, “Sikilizeni! Sikilizeni! Mwambieni Yoabu aje hapa ili niweze kuzungumza naye.”
17 Który gdy do niej przystąpił, rzekła mu ona niewiasta: Tyżeś jest Joab? I odpowiedział: Jestem. Tedy mu rzekła: Słuchaj słów służebnicy twojej; i odpowiedział: Słucham.
Yoabu alikwenda mbele yake, akamuuliza, “Wewe ni Yoabu?” Akamjibu, “Ndiye mimi.” Yule mwanamke akamwambia, “Sikiliza kile mtumishi wako atakachokuambia.” Akamwambia, “Ninasikiliza.”
18 Przetoż rzekła, mówiąc: Powiadano przedtem, mówiąc: Koniecznie pytać się będą w Abelu, a tak się wszystko sprawi.
Huyo mwanamke akaendelea kusema, “Zamani za kale walikuwa wakisema, ‘Wakaulize ushauri huko Abeli,’ hivyo kulimaliza lile shauri.
19 Jam jest jedno miasto z spokojnych i wiernych w Izraelu, a ty szukasz, abyś zatracił miasto i matkę w Izraelu; przeczże chcesz zburzyć dziedzictwo Pańskie?
Sisi ni watu wa amani na waaminifu katika Israeli. Wewe unajaribu kuharibu mji ambao ni mama katika Israeli. Kwa nini unataka kumeza urithi wa Bwana?”
20 I odpowiedział jej Joab, mówiąc: Niedaj, niedaj mi tego Boże, abym miał podwrócić i zburzyć je.
Yoabu akajibu, “Hilo liwe mbali nami. Hilo liwe mbali nami kumeza au kuharibu.
21 Nie takci się rzecz ma. Ale mąż z góry Efraim, imieniem Seba, syn Bichry, podniósł rękę swą przeciw królowi Dawidowi; wydajcież go samego, a odciągnę od miasta. Zatem rzekła niewiasta do Jaoba: Oto głowę jego zrzucą do ciebie z muru.
Hivyo sivyo ilivyo. Mtu mmoja jina lake Sheba mwana wa Bikri, kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ameinua mkono wake dhidi ya mfalme, dhidi ya Daudi. Nikabidhini mtu huyu mmoja, nami nitajiondoa katika mji huu.” Huyu mwanamke akamwambia Yoabu, “Kichwa chake mtatupiwa kupitia juu ya ukuta.”
22 A tak sprawiła to ona niewiasta u wszystkigo ludu mądrością swoją, że ściąwszy głowę Sebie, synowi Bichry, zrzucili ją do Jaoaba; który zatrąbił w trąbę, i rozeszli się wszyscy od miasta, każdy do namiotów swoich; Joab się też wrócił do króla do Jeruzalemu.
Ndipo huyo mwanamke akaenda kwa watu wote akiwa na ushauri wake wa busara, nao wakakata kichwa cha Sheba mwana wa Bikri na kumtupia Yoabu. Kwa hiyo Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wake wakatawanyika kutoka mjini, kila mmoja akirejea nyumbani kwake. Naye Yoabu akarudi kwa mfalme huko Yerusalemu.
23 I był Joab hetmanem nad wszystkiem wojskiem Izraelskiem, a Banajas, syn Jojady, nad Chretczykami i nad Feletczykami.
Yoabu alikuwa jemadari wa jeshi lote la Israeli; Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu ya Wakerethi na Wapelethi;
24 Adoram był poborcą, a Jozafat, syn Ahiluda, kanclerzem.
Adoramu alikuwa kiongozi wa wale waliofanya kazi ya kulazimishwa; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
25 Seja pisarzem, a Sadok i Abijatar byli kapłanami.
Sheva alikuwa mwandishi; Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani;
26 Hira także Jairtczyk był książęciem u Dawida.
na Ira, Myairi, alikuwa kuhani wa Daudi.

< II Samuela 20 >