< Rodzaju 48 >

1 To gdy się stało, dano znać Józefowi: Oto, ojciec twój zachorzał; który wziąwszy dwóch synów swoich z sobą, Manasesa i Efraima, jechał do niego.
Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye.
2 I powiedziano Jakóbowi, mówiąc: Oto, syn twój Józef idzie do ciebie. A Izrael pokrzepiwszy się, usiadł na łożu.
Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani.
3 I rzekł Jakób do Józefa: Bóg wszechmogący ukazał mi się w Luzie, w ziemi Chananejskiej, i błogosławił mi.
Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki,
4 A mówił do mnie: Oto, ja rozrodzę cię, i rozmnożę cię, i wywiodę z ciebie wielki naród; a dam ziemię tę nasieniu twemu po tobie w dziedzictwo wieczne.
naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’
5 Przetoż teraz dwaj synowie twoi, którzyć się urodzili w ziemi Egipskiej, pierwej niżem ja tu do ciebie przyszedł do Egiptu, moi są, Efraim i Manases; jako Ruben i Symeon moi będą.
“Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu.
6 Ale dzieci twoje, które po tych spłodzisz, twoje będą; imieniem braci swojej będą zwani w osiadłościach swych.
Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao.
7 A gdym się wracał z Padan, umarła mi Rachel w ziemi Chananejskiej w drodze, gdym jeszcze był jakoby na milę od Efraty, i pogrzebłem ją tam przy drodze ku Efracie; a toć jest Betlehem.
Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu).
8 A ujrzawszy Izrael syny Józefowe, rzekł: Czyi to są?
Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?”
9 Tedy odpowiedział Józef ojcu swemu: Synowie to moi, które mi tu dał Bóg; a on rzekł: Przywiedź je proszę do mnie, abym im błogosławił.
Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.” Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.”
10 A oczy Izraelowe ociężały były dla starości, i nie mógł dojrzeć: i przywiódł je do niego, które Jakób pocałował i obłapił.
Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia.
11 Zatem rzekł Izrael do Józefa: Oglądać więcej oblicza twego nie spodziewałem się, a oto, dał mi Bóg widzieć i nasienie twoje.
Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.”
12 Tedy Józef odwiódł je od łona jego, i pokłonił się obliczem swem aż do ziemi.
Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi.
13 A wziąwszy Józef obydwu, postawił Efraima po prawej ręce swojej, a po lewej Izraelowej; a Manasesa po lewej ręce swojej a po prawej Izraelowej, i przywiódł je do niego.
Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao.
14 A wyciągnąwszy Izrael prawicę swoję, włożył ją na głowę Efraima, który był młodszy, lewicę zaś swoję na głowę Manasesa, umyślnie przełożywszy ręce swoje, choć Mananses był pierworodny.
Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza.
15 I błogosławił Józefowi, mówią: Bóg, przed którego obliczem chodzili ojcowie moi, Abraham i Izaak, Bóg który mię żywił od młodości mojej aż do dnia tego;
Ndipo akambariki Yosefu akisema, “Mungu ambaye baba zangu Abrahamu na Isaki walimtii, Mungu ambaye amekuwa mchungaji wa maisha yangu yote mpaka leo hii,
16 Anioł, który mię wyrwał ze wszystkiego złego, niech błogosławi dzieciom tym, a niech będą nazywani od imienia mego, i od imienia ojców moich, Abrahama i Izaaka, a jako ryby niech się rozmnożą na ziemi.
Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote, yeye na awabariki vijana hawa. Na waitwe kwa jina langu na kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki, wao na waongezeke kwa wingi katika dunia.”
17 A obaczywszy Józef, iż włożył ojciec jego rękę prawą swoję na głowę Efraimowę, nie miło mu było; i ujął rękę ojca swego, aby ją przeniósł z głowy Efraimowej na głowę Manasesowę.
Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase.
18 I rzekł Józef do ojca swego: Nie tak, ojcze mój; albowiem ten jest pierworodny, włóżże prawicę swoję na głowę jego.
Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.”
19 Ale się zbraniał ojciec jego, i rzekł: Wiemci synu miły, wiem; i tenci się stanie w lud wielki, tenci też urośnie; a wszakże brat jego młodszy urośnie nadeń, a z nasienia jego wyjdzie mnóstwo narodów.
Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.”
20 Błogosławił im tedy dnia onego, mówiąc: Przez cię będzie błogosławił Izrael, mówiąc: Niech cię wystawi Bóg jako Efraima, i jako Manasesa; a tak przełożył Efraima nad Manasesa.
Akawabarikia siku ile na kusema, “Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii: ‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’” Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase.
21 Potem rzekł Izrael do Józefa: Oto, ja umieram, a Bóg będzie z wami, i przywróci was do ziemi ojców waszych.
Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu.
22 Oto, ja dawam ci część jednę mimo bracią twoję, którejm nabył z ręki Amorejczyków mieczem moim, i łukiem moim.
Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

< Rodzaju 48 >