< Jozuego 17 >

1 Padł też los pokoleniu Manasesowemu (bo on jest pierworodny Józefów.) Machyrowi pierworodnemu Manasesowemu, ojcu Galaada, przeto, że był mężem walecznym, i dostał mu się Galaad i Basan.
Huu ndio mgawo wa kabila la Manase kama mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, yaani kwa ajili ya Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase. Makiri alikuwa baba wa Wagileadi, ambao walipokea Gileadi na Bashani kwa sababu Wamakiri walikuwa askari wakuu.
2 Dostało się też innym synom Manasesowym według domów ich, synom Abiezer, i synom Helek, i synom Esryjel, i synom Sychem, i synom Hefer, i synom Semida. Cić są synowie Manasesowi, syna Józefowego, mężczyzny według domów ich.
Kwa hiyo mgawo huu ulikuwa kwa ajili ya watu wa Manase waliokuwa wamebaki, ambao ni koo za Abiezeri, Heleki, Asirieli, Shekemu, Heferi na Shemida. Hawa ndio wanaume wale wengine wa uzao wa Manase mwana wa Yosefu kwa koo zao.
3 Ale Salfaad, syn Heferów, syna Galaadowego, syna Machyrowego, syna Manasesowego, nie miał synów, jedno córki, a te imiona córek jego: Machla, i Noa, Hegla, Melcha, i Tersa.
Basi Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase hakuwa na wana waume ila mabinti tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.
4 Te przyszedłszy przed Eleazara kapłana, i przed Jozuego, syna Nunowego, i przed książęta, rzekły: Pan rozkazał Mojżeszowi, aby nam dał dziedzictwo w pośród braci naszych; i dał im Jozue według rozkazania Pańskiego dziedzictwo w pośrodku braci ojca ich.
Wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi, wakasema: “Bwana alimwagiza Mose atupatie urithi miongoni mwa ndugu zetu.” Kwa hiyo Yoshua akawapa urithi pamoja na ndugu wa baba yao, kufuatana na agizo la Bwana.
5 I przypadło sznurów na Manasesa dziesięć, oprócz ziemi Galaad i Basan, które były za Jordanem.
Fungu la Manase lilikuwa na sehemu kumi za nchi, licha ya Gileadi na Bashani mashariki mwa Yordani,
6 Albowiem córki Manasesowe otrzymały dziedzictwo między syny jego, a ziemia Galaad dostała się drugim synom Manasesowym.
kwa sababu wale binti za kabila la Manase walipokea urithi miongoni mwa wana wa kiume. Nchi ya Gileadi ilikuwa mali ya wazao wa Manase waliobaki.
7 I była granica Manasesowa od Aser do Machmatat, które jest przeciwko Sychem, a idzie granica ta po prawej stronie do mieszkających w En Tafua.
Eneo la Manase lilienea kuanzia Asheri hadi Mikmeta mashariki mwa Shekemu. Mpaka ule ulielekea upande wa kusini kutoka pale kujumuisha watu walioishi En-Tapua.
8 (Manasesowa była ziemia Tafua; ale Tafua przy granicy Manasesowej była synów Efraimowych.)
(Nchi ya Tapua ilikuwa mali ya Manase, lakini Tapua yenyewe iliyo mpakani mwa nchi ya Manase ilikuwa ya Waefraimu.)
9 I bieży ta granica do potoku Kana na południe tegoż potoku; a miasta Efraimitów są między miasty Manasesowemi; ale granica Manasesowa idzie od północy onego potoku, a kończy się u morza.
Kisha mpaka ule uliendelea kuelekea kusini hadi Bonde la Kana. Kulikuwepo miji ya Efraimu iliyokuwa miongoni mwa miji ya Manase, lakini mpaka wa Manase ulikuwa upande wa kaskazini wa lile bonde na kuishia kwenye bahari.
10 Na południe był dział Efraimów, a na północy Manasesów, a morze jest granica jego; a w pokoleniu Aser schodzą się na północy, a w Isaschar na wschód słońca.
Nchi ya kusini ilikuwa ya Efraimu, na ile iliyokuwa upande wa kaskazini ilikuwa ya Manase. Eneo la Manase lilifika bahari na ikapakana na Asheri upande wa kaskazini, na Isakari upande wa mashariki.
11 I dostało się Manasesowi w pokoleniu Isaschar i w Aser, Betsan i miasteczka jego, i Jeblaam i miasteczka jego; przytem mieszkający w Dor i miasteczka ich, także mieszkający w Endor i miasteczka ich; i mieszkający też w Tanach i miasteczka ich, i mieszkający w Magiedda i miasteczka ich; trzy powiaty.
Katika Isakari na Asheri Manase alikuwa na miji pia: Beth-Shani, Ibleamu na watu wa Dori, Endori, Taanaki na Megido, pamoja na vijiji vyote vinavyohusika na miji hiyo (ya tatu katika orodha ni Nafothi).
12 Ale nie mogli synowi Manasesowi wypędzić z onych miast obywateli; przetoż począł Chananejczyk mieszkać w onej ziemi.
Lakini Wamanase hawakuweza kuimiliki miji hii, kwa kuwa Wakanaani walikazana kuishi katika maeneo hayo.
13 A gdy się zmocnili synowie Izraelscy, uczynili Chananejczyka hołdownikiem: ale go nie wygnali do szczętu.
Hata hivyo, Waisraeli walivyoendelea kupata nguvu waliwatumikisha Wakanaani na kuwatia katika kazi za kulazimishwa, lakini hawakuwafukuza kabisa.
14 Tedy rzekli synowie Józefowi do Jozuego, mówiąc: Przeczżeś nam dał w dziedzictwo los jeden, i sznur jeden? a myśmy lud wielki i dotąd błogosławił nam Pan.
Watu wa Yosefu wakamwambia Yoshua, “Kwa nini umetupa sisi mgawo mmoja tu na sehemu moja tu kuwa urithi? Sisi tu watu wengi sana, na Bwana ametubariki kwa wingi.”
15 I rzekł do nich Jozue: Jeźliś jest ludem wielkiem, idźże do lasu, a wysiecz sobie tam miejsca w ziemi Ferezejskiej, i Refaimskiej, jeźlić ciasna góra Efraimowa.
Yoshua akajibu, “Kama ninyi ni wengi sana, na kama nchi ya vilima ya Efraimu ni ndogo sana kwenu, pandeni msituni mkafyeke eneo kwa ajili yenu wenyewe huko kwenye nchi ya Waperizi na Warefai.”
16 Któremu odpowiedzieli synowie Józefowi: Nie dosyć nam na tej górze; do tego wozy żelazne są u wszystkich Chananejczyków, którzy mieszkają w ziemi nadolnej, i u tych, którzy mieszkają w Betsan i w miasteczkach jego, także u tych, którzy mieszkają w dolinie Jezreel.
Watu wa Yosefu wakajibu, “Hiyo nchi ya vilima haitutoshi, nao Wakanaani wote wanaoishi katika tambarare wanayo magari ya vita ya chuma, wote wa Beth-Shani na miji yake, na wale walio katika Bonde la Yezreeli.”
17 RZekł tedy Jozue do domu Józefowego, do Efraima i do Manasesa, mówiąc: Ludeś ty wielki, i moc twoja wielka, nie będziesz miał tylko losu jednego.
Lakini Yoshua akanena na nyumba ya Yosefu, yaani Efraimu na Manase: “Ninyi ni wengi sana na wenye nguvu sana. Hamtakuwa na mgawo mmoja tu,
18 Ale górę będziesz miał; a iż tam jest las, tedy go wyrąbiesz, i będziesz miał granice jego; bo wypędzisz Chananejczyka, choć ma wozy żelazne i choć jest potężny.
bali pia nchi hii ya kilima yenye msitu. Ifyekeni, nayo mipaka yake itakuwa yenu umbali mtakaoweza kufika. Ingawa Wakanaani wana magari ya chuma, nao wana nguvu, mwaweza kuwafukuza humo.”

< Jozuego 17 >