< preritAH 16 >

1 paulo darbbIlustrAnagarayorupasthitobhavat tatra tImathiyanAmA ziSya eka AsIt; sa vizvAsinyA yihUdIyAyA yoSito garbbhajAtaH kintu tasya pitAnyadezIyalokaH|
Paulo pia alipokuja Derbe na Lystra; na tazama, pale palikuwepo na mwanafunzi aitwaye Timotheo, ni Kijana aliyezaliwa na mama wa Kiyahudi ambaye ni muumini na baba yake ni Mgiriki.
2 sa jano lustrA-ikaniyanagarasthAnAM bhrAtRNAM samIpepi sukhyAtimAn AsIt|
Watu wa Listra na Ikonia walimshudia vizuri.
3 paulastaM svasaGginaM karttuM matiM kRtvA taM gRhItvA taddezanivAsinAM yihUdIyAnAm anurodhAt tasya tvakchedaM kRtavAn yatastasya pitA bhinnadezIyaloka iti sarvvairajJAyata|
Paulo alimtaka ili asafiri naye, hivyo akamchukua na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi waliokuwako huko kwani wote walimjua kuwa baba yake ni Mgiriki.
4 tataH paraM te nagare nagare bhramitvA yirUzAlamasthaiH preritai rlokaprAcInaizca nirUpitaM yad vyavasthApatraM tadanusAreNAcarituM lokebhyastad dattavantaH|
Walipokuwa wakienda walipita kwenye miji na kutoa maagizo kwa makanisa ili kuyatii maagizo hayo yaliandikwa na mitume na wazee huko Yerusalemu.
5 tenaiva sarvve dharmmasamAjAH khrISTadharmme susthirAH santaH pratidinaM varddhitA abhavan|
Hivyo makanisa yakaimarishwa katika imani na walioamini wakaongezeka kwa idadi kila siku.
6 teSu phrugiyAgAlAtiyAdezamadhyena gateSu satsu pavitra AtmA tAn AziyAdeze kathAM prakAzayituM pratiSiddhavAn|
Paulo na mwenzake wakaenda Firigia na Galatia, kwani Roho wa Mungu aliwakataza kuhubiri neno huko kwenye jimbo la Asia.
7 tathA musiyAdeza upasthAya bithuniyAM gantuM tairudyoge kRte AtmA tAn nAnvamanyata|
Walipokaribia Misia, walijaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu akawakataza.
8 tasmAt te musiyAdezaM parityajya troyAnagaraM gatvA samupasthitAH|
Kwa hiyo wakapita Misia wakaja mpaka Mji wa Troa.
9 rAtrau paulaH svapne dRSTavAn eko mAkidaniyalokastiSThan vinayaM kRtvA tasmai kathayati, mAkidaniyAdezam AgatyAsmAn upakurvviti|
Maono yalimtokea Paulo usiku, kulikuwa na mtu wa Makedonia amesimama, akimwita na kusema “Njoni mtusaidie huku Makedonia”.
10 tasyetthaM svapnadarzanAt prabhustaddezIyalokAn prati susaMvAdaM pracArayitum asmAn AhUyatIti nizcitaM buddhvA vayaM tUrNaM mAkidaniyAdezaM gantum udyogam akurmma|
Paulo alipoona maono, mara tukajiandaa kwenda Makedonia, akijua kwamba Mungu alituita kwenda kuwahubiria injili.
11 tataH paraM vayaM troyAnagarAd prasthAya RjumArgeNa sAmathrAkiyopadvIpena gatvA pare'hani niyApalinagara upasthitAH|
Hivyo tukaondoka kutoka Troa, tukaenda moja kwa moja Samothrake, na siku iliyofuata tukafika mji wa Neapoli.
12 tasmAd gatvA mAkidaniyAntarvvartti romIyavasatisthAnaM yat philipInAmapradhAnanagaraM tatropasthAya katipayadinAni tatra sthitavantaH|
Kutoka hapo tukaenda Filipi ambao ni moja ya mji wa Makedonia, mji muhimu katika wilaya na utawala wa Kirumi na tukakaa siku kadhaa.
13 vizrAmavAre nagarAd bahi rgatvA nadItaTe yatra prArthanAcAra AsIt tatropavizya samAgatA nArIH prati kathAM prAcArayAma|
Siku ya Sabato, tulikwenda nje ya lango kwa njia ya mto, sehemu ambayo tulidhania kutakuwa na mahali pa kufanyia maombi. Tulikaa chini na kuongea na akinamama waliokuja pamoja.
14 tataH thuyAtIrAnagarIyA dhUSarAmbaravikrAyiNI ludiyAnAmikA yA IzvarasevikA yoSit zrotrINAM madhya AsIt tayA pauloktavAkyAni yad gRhyante tadarthaM prabhustasyA manodvAraM muktavAn|
Mwanamke mmoja aitwaye Lidia, muuzaji wa zambarau, kutoka katika mji wa Tiatira, mwenye kumwabudu Mungu, alitusikiliza. Bwana alimfungua moyo wake na kuweka maanani maneno yaliyosemwa na Paulo.
15 ataH sA yoSit saparivArA majjitA satI vinayaM kRtvA kathitavatI, yuSmAkaM vicArAd yadi prabhau vizvAsinI jAtAhaM tarhi mama gRham Agatya tiSThata| itthaM sA yatnenAsmAn asthApayat|
Baada ya kubatizwa, yeye na nyumba yake yote, alitusihi akisema “kama mmeniona kuwa mimi ni mwaminifu katika Bwana, basi nawasihi muingie na kukaa kwangu”. Akatusihi sana.
16 yasyA gaNanayA tadadhipatInAM bahudhanopArjanaM jAtaM tAdRzI gaNakabhUtagrastA kAcana dAsI prArthanAsthAnagamanakAla AgatyAsmAn sAkSAt kRtavatI|
Ikawa kwamba, tulipokuwa tunaenda mahali pa kuomba, msichana mmoja aliyekuwa na pepo la utambuzi akakutana nasi. Alimletea bwana wake faida nyingi kwa kubashiri.
17 sAsmAkaM paulasya ca pazcAd etya proccaiH kathAmimAM kathitavatI, manuSyA ete sarvvoparisthasyezvarasya sevakAH santo'smAn prati paritrANasya mArgaM prakAzayanti|
Mwanamke huyu alimfuata Paulo pamoja na sisi, akipiga kelele na kusema “Hawa wanaume ni watumishi wa Mungu aliye Mkuu, wanaowatangazia ninyi habari ya wokovu”.
18 sA kanyA bahudinAni tAdRzam akarot tasmAt paulo duHkhitaH san mukhaM parAvartya taM bhUtamavadad, ahaM yIzukhrISTasya nAmnA tvAmAjJApayAmi tvamasyA bahirgaccha; tenaiva tatkSaNAt sa bhUtastasyA bahirgataH|
Alifanya hivyo kwa siku nyingi, lakini Paulo akiwa amekasirishwa na tendo hilo, aligeuka nyuma na kumwambia pepo, “Nakuamuru kwa Jina la Yesu umtoke ndani yake.” Naye akatoka na kumwacha mara moja.
19 tataH sveSAM lAbhasya pratyAzA viphalA jAteti vilokya tasyAH prabhavaH paulaM sIlaJca dhRtvAkRSya vicArasthAne'dhipatInAM samIpam Anayan|
Mabwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limeondoka, waliwakamata Paulo na Sila na kuwaburuza sokoni mbele ya wenye mamlaka.
20 tataH zAsakAnAM nikaTaM nItvA romilokA vayam asmAkaM yad vyavaharaNaM grahItum AcarituJca niSiddhaM,
Walipowafikisha kwa mahakimu, walisema, “Hawa wanaume ni Wayahudi na wanasababisha ghasia kubwa katika mji wetu.
21 ime yihUdIyalokAH santopi tadeva zikSayitvA nagare'smAkam atIva kalahaM kurvvanti,
Wanafundisha mambo ambayo siyo sheria sisi kuyapokea wala kuyafuata kama Warumi.”
22 iti kathite sati lokanivahastayoH prAtikUlyenodatiSThat tathA zAsakAstayo rvastrANi chitvA vetrAghAtaM karttum AjJApayan|
Umati ukawainukia kinyume Paulo na Sila, mahakimu wakararua nguo zao na kuwavua na kuamuru wachapwe viboko
23 aparaM te tau bahu prahAryya tvametau kArAM nItvA sAvadhAnaM rakSayeti kArArakSakam Adizan|
Baada ya kuwachapa viboko vingi, waliwatupa gerezani na kumuamuru askari wa gereza kuwalinda vyema.
24 ittham AjJAM prApya sa tAvabhyantarasthakArAM nItvA pAdeSu pAdapAzIbhi rbaddhvA sthApitAvAn|
Baada ya kupokea amri hiyo, askari wa gereza aliwatupa katika chumba cha ndani ya gereza na kuwafunga miguu yao kwenye sehemu alipowahifadhi.
25 atha nizIthasamaye paulasIlAvIzvaramuddizya prAthanAM gAnaJca kRtavantau, kArAsthitA lokAzca tadazRNvan
Wakati wa usiku wa manane, Paulo na Sila wakawa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu, huku wafungwa wengine wakiwasikiliza,
26 tadAkasmAt mahAn bhUmikampo'bhavat tena bhittimUlena saha kArA kampitAbhUt tatkSaNAt sarvvANi dvArANi muktAni jAtAni sarvveSAM bandhanAni ca muktAni|
Ghafla kukatokea tetemeko kuu na misingi ya gereza ikatikiswa, milango ya gereza ikafunguka, na minyororo ya wafungwa wote ikalegezwa.
27 ataeva kArArakSako nidrAto jAgaritvA kArAyA dvArANi muktAni dRSTvA bandilokAH palAyitA ityanumAya koSAt khaGgaM bahiH kRtvAtmaghAtaM karttum udyataH|
Mlinzi wa Gereza aliamka kutoka usingizini na akaona milango yote ya gereza imefunguliwa; hivyo akachukua upanga wake maana alitaka kujiua kwa sababu alifikiri wafungwa wote walikwishatoroka,
28 kintu paulaH proccaistamAhUya kathitavAn pazya vayaM sarvve'trAsmahe, tvaM nijaprANahiMsAM mAkArSIH|
Lakini, Paulo akapiga kelele kwa sauti kuu, akisema “usijidhuru kwa sababu wote tuko mahali hapa”.
29 tadA pradIpam Anetum uktvA sa kampamAnaH san ullampyAbhyantaram Agatya paulasIlayoH pAdeSu patitavAn|
Mlinzi wa gereza aliomba taa ziletwe na akaingia ndani ya gereza kwa haraka, akitetemeka na kuogopa, akawaangukia Paulo na Sila,
30 pazcAt sa tau bahirAnIya pRSTavAn he mahecchau paritrANaM prAptuM mayA kiM karttavyaM?
na kuwatoa nje ya gereza na kusema, “Waheshimiwa, nifanye nini ili nipate kuokoka?”
31 pazcAt tau svagRhamAnIya tayoH sammukhe khAdyadravyANi sthApitavAn tathA sa svayaM tadIyAH sarvve parivArAzcezvare vizvasantaH sAnanditA abhavan|
Nao wakamwambia, “Mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.”
32 tasmai tasya gRhasthitasarvvalokebhyazca prabhoH kathAM kathitavantau|
Walinena neno la Bwana kwake, pamoja na watu wote wa nyumbani kwake,
33 tathA rAtrestasminneva daNDe sa tau gRhItvA tayoH prahArANAM kSatAni prakSAlitavAn tataH sa svayaM tasya sarvve parijanAzca majjitA abhavan|
Mlinzi wa gereza aliwachukua usiku ule na kuwaosha sehemu walizoumia, yeye pamoja na watu wa nyumbani mwake wakabatizwa mara.
34 pazcAt tau svagRhamAnIya tayoH sammukhe khAdyadravyANi sthApitavAn tathA sa svayaM tadIyAH sarvve parivArAzcezvare vizvasantaH sAnanditA abhavan|
Akawaleta Paulo na Sila nyumbani kwake na kuwatengea chakula. Naye akawa na furaha kuu pamoja na watu wa nyumbani mwake kwa sababu walimwamini Mungu.
35 dina upasthite tau lokau mocayeti kathAM kathayituM zAsakAH padAtigaNaM preSitavantaH|
Ilipokuwa mchana, mahakimu walituma ujumbe kwa yule mlinzi wa gereza wakisema, “Waruhusu wale watu waende”,
36 tataH kArArakSakaH paulAya tAM vArttAM kathitavAn yuvAM tyAjayituM zAsakA lokAna preSitavanta idAnIM yuvAM bahi rbhUtvA kuzalena pratiSThetAM|
Mlinzi wa gereza akamjulisha Paulo juu ya maneno hayo ya kuwa, “Mahakimu walituma ujumbe niruhusu mwondoke: hivyo tokeni nje na mwende kwa amani.”
37 kintu paulastAn avadat romilokayorAvayoH kamapi doSam na nizcitya sarvveSAM samakSam AvAM kazayA tADayitvA kArAyAM baddhavanta idAnIM kimAvAM guptaM vistrakSyanti? tanna bhaviSyati, svayamAgatyAvAM bahiH kRtvA nayantu|
Lakini Paulo akawaambia, “Walitupiga hadharani, watu ambao ni Warumi bila kutuhukumu na waliamua kututupa gerezani; halafu sasa wanataka kututoa kwa siri? Hapana, haitawezekana, wao wenyewe waje kututoa mahali hapa”.
38 tadA padAtibhiH zAsakebhya etadvArttAyAM kathitAyAM tau romilokAviti kathAM zrutvA te bhItAH
Walinzi wakawajulisha mahakimu juu ya maneno hayo, mahakimu wakaogopa sana pale walipojua kuwa Paulo na Sila ni Warumi.
39 santastayoH sannidhimAgatya vinayam akurvvan aparaM bahiH kRtvA nagarAt prasthAtuM prArthitavantaH|
Mahakimu wakaja na kuwasihi watoke, na walipowatoa nje ya gereza, waliwaomba Paulo na Sila watoke nje ya mji wao.
40 tatastau kArAyA nirgatya ludiyAyA gRhaM gatavantau tatra bhrAtRgaNaM sAkSAtkRtya tAn sAntvayitvA tasmAt sthAnAt prasthitau|
Kwa hiyo Paulo na Sila wakatoka nje ya gereza wakaja nyumbani kwa Lidia. Paulo na Sila walipowaona ndugu, waliwatia moyo na kisha kuondoka katika mji huo.

< preritAH 16 >