< preritAH 26 >

1 tata AgrippaH paulam avAdIt, nijAM kathAM kathayituM tubhyam anumati rdIyate| tasmAt paulaH karaM prasAryya svasmin uttaram avAdIt|
Basi, Agripa akamwambia Paulo, “Unaruhusiwa kujitetea.” Hapo Paulo alinyosha mkono wake akajitetea hivi:
2 he AgripparAja yatkAraNAdahaM yihUdIyairapavAdito 'bhavaM tasya vRttAntam adya bhavataH sAkSAn nivedayitumanumatoham idaM svIyaM paramaM bhAgyaM manye;
“Mfalme Agripa, ninajiona mwenye bahati leo kujitetea mbele yako kuhusu yale mashtaka yote ambayo Wayahudi walikuwa wamesema juu yangu.
3 yato yihUdIyalokAnAM madhye yA yA rItiH sUkSmavicArAzca santi teSu bhavAn vijJatamaH; ataeva prArthaye dhairyyamavalambya mama nivedanaM zRNotu|
Hasa kwa vile wewe mwenyewe ni mtaalamu wa desturi za Wayahudi na migogoro yao, ninakuomba basi unisikilize kwa uvumilivu.
4 ahaM yirUzAlamnagare svadezIyalokAnAM madhye tiSThan A yauvanakAlAd yadrUpam AcaritavAn tad yihUdIyalokAH sarvve vidanti|
“Wayahudi wanajua habari za maisha yangu tangu utoto, jinsi nilivyoishi tangu mwanzo kati ya taifa langu huko Yerusalemu.
5 asmAkaM sarvvebhyaH zuddhatamaM yat phirUzIyamataM tadavalambI bhUtvAhaM kAlaM yApitavAn ye janA A bAlyakAlAn mAM jAnAnti te etAdRzaM sAkSyaM yadi dadAti tarhi dAtuM zaknuvanti|
Wananifahamu kwa muda mrefu, na wanaweza kushuhudia, kama wakipenda, kwamba tangu mwanzo niliishi kama mmoja wa kikundi chenye siasa kali zaidi katika dini yetu, yaani kikundi cha Mafarisayo.
6 kintu he AgripparAja Izvaro'smAkaM pUrvvapuruSANAM nikaTe yad aGgIkRtavAn tasya pratyAzAhetoraham idAnIM vicArasthAne daNDAyamAnosmi|
Na sasa niko hapa nihukumiwe kwa sababu ninaitumainia ile ahadi ambayo Mungu aliwaahidia babu zetu.
7 tasyAGgIkArasya phalaM prAptum asmAkaM dvAdazavaMzA divAnizaM mahAyatnAd IzvarasevanaM kRtvA yAM pratyAzAM kurvvanti tasyAH pratyAzAyA hetorahaM yihUdIyairapavAdito'bhavam|
Ahadi hiyo ndiyo ileile inayotumainiwa na makabila kumi na mawili ya taifa letu, wakimtumikia Mungu kwa dhati mchana na usiku. Mheshimiwa mfalme, Wayahudi wananishtaki kwa sababu ya tumaini hilo!
8 Izvaro mRtAn utthApayiSyatIti vAkyaM yuSmAkaM nikaTe'sambhavaM kuto bhavet?
Kwa nini ninyi mnaona shida sana kuamini kwamba Mungu huwafufua wafu?
9 nAsaratIyayIzo rnAmno viruddhaM nAnAprakArapratikUlAcaraNam ucitam ityahaM manasi yathArthaM vijJAya
Kwa kweli mimi mwenyewe niliamini kwamba ni wajibu wangu kufanya mambo mengi kulipinga jina la Yesu wa Nazareti.
10 yirUzAlamanagare tadakaravaM phalataH pradhAnayAjakasya nikaTAt kSamatAM prApya bahUn pavitralokAn kArAyAM baddhavAn vizeSatasteSAM hananasamaye teSAM viruddhAM nijAM sammatiM prakAzitavAn|
Mambo hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Mimi binafsi, nikiwa nimepewa mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu, nilipata kuwatia gerezani wengi wa watu wa Mungu. Nao walipohukumiwa kuuawa, nilipiga kura ya kukubali.
11 vAraM vAraM bhajanabhavaneSu tebhyo daNDaM pradattavAn balAt taM dharmmaM nindayitavAMzca punazca tAn prati mahAkrodhAd unmattaH san videzIyanagarANi yAvat tAn tADitavAn|
Mara nyingi niliwafanya waadhibiwe katika masunagogi yote nikiwashurutisha waikane imani yao. Hasira yangu kwao ilikuwa kubwa hata nikawasaka mpaka miji ya mbali.
12 itthaM pradhAnayAjakasya samIpAt zaktim AjJApatraJca labdhvA dammeSaknagaraM gatavAn|
“Kwa mujibu huohuo, nilikwenda Damasko wakati mmoja, nikiwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa makuhani wakuu.
13 tadAhaM he rAjan mArgamadhye madhyAhnakAle mama madIyasaGginAM lokAnAJca catasRSu dikSu gagaNAt prakAzamAnAM bhAskaratopi tejasvatIM dIptiM dRSTavAn|
Mheshimiwa, wakati nilipokuwa njiani, saa sita mchana, niliona mwanga mkubwa kuliko wa jua ukiangaza kutoka mbinguni, ukanizunguka mimi na wale wasafiri wenzangu.
14 tasmAd asmAsu sarvveSu bhUmau patiteSu satsu he zaula hai zaula kuto mAM tADayasi? kaNTakAnAM mukhe pAdAhananaM tava duHsAdhyam ibrIyabhASayA gadita etAdRza ekaH zabdo mayA zrutaH|
Sisi sote tulianguka chini, nami nikasikia sauti ikiniambia kwa Kiebrania: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa? Unajiumiza bure kama punda anayepiga teke fimbo ya bwana wake.
15 tadAhaM pRSTavAn he prabho ko bhavAn? tataH sa kathitavAn yaM yIzuM tvaM tADayasi sohaM,
Mimi nikauliza: Ni nani wewe Bwana? Naye Bwana akajibu: Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
16 kintu samuttiSTha tvaM yad dRSTavAn itaH punaJca yadyat tvAM darzayiSyAmi teSAM sarvveSAM kAryyANAM tvAM sAkSiNaM mama sevakaJca karttum darzanam adAm|
Haidhuru, inuka sasa; simama wima. Nimekutokea ili nikuweke rasmi kuwa mtumishi wangu. Utawathibitishia watu wengine mambo uliyoyaona leo na yale ambayo bado nitakuonyesha.
17 vizeSato yihUdIyalokebhyo bhinnajAtIyebhyazca tvAM manonItaM kRtvA teSAM yathA pApamocanaM bhavati
Nitakuokoa na watu wa Israeli na watu wa mataifa mengine ambao mimi ninakutuma kwao.
18 yathA te mayi vizvasya pavitrIkRtAnAM madhye bhAgaM prApnuvanti tadabhiprAyeNa teSAM jJAnacakSUMSi prasannAni karttuM tathAndhakArAd dIptiM prati zaitAnAdhikArAcca IzvaraM prati matIH parAvarttayituM teSAM samIpaM tvAM preSyAmi|
Utayafumbua macho yao na kuwawezesha watoke gizani na kuingia katika mwanga; watoke katika utawala wa Shetani, wamgeukie Mungu; ili kwa kuamini, wapate kusamehewa dhambi na kuchukua nafasi yao kati ya wale ambao wamepata kuwa watu wa Mungu.
19 he AgripparAja etAdRzaM svargIyapratyAdezaM agrAhyam akRtvAhaM
“Hivyo, mfalme Agripa, sikuweza kuwa mkaidi kwa maono hilo la mbinguni.
20 prathamato dammeSaknagare tato yirUzAlami sarvvasmin yihUdIyadeze anyeSu dezeSu ca yena lokA matiM parAvarttya IzvaraM prati parAvarttayante, manaHparAvarttanayogyAni karmmANi ca kurvvanti tAdRzam upadezaM pracAritavAn|
Ila nilianza kuhubiri kwanza kwa watu wa Damasko, halafu kwa wale wa Yerusalemu na nchi yote ya Yudea, na pia kwa watu wa mataifa mengine. Niliwahimiza wamgeukie Mungu na kuonyesha kwa vitendo kwamba wamebadilisha mioyo yao.
21 etatkAraNAd yihUdIyA madhyemandiraM mAM dhRtvA hantum udyatAH|
Kwa sababu hiyo, Wayahudi walinikamata nikiwa Hekaluni, wakajaribu kuniua.
22 tathApi khrISTo duHkhaM bhuktvA sarvveSAM pUrvvaM zmazAnAd utthAya nijadezIyAnAM bhinnadezIyAnAJca samIpe dIptiM prakAzayiSyati
Lakini Mungu alinisaidia; na hivyo mpaka siku ya leo nimesimama imara nikitoa ushuhuda kwa wote, wakubwa na wadogo. Ninayosema ni yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia;
23 bhaviSyadvAdigaNo mUsAzca bhAvikAryyasya yadidaM pramANam adaduretad vinAnyAM kathAM na kathayitvA IzvarAd anugrahaM labdhvA mahatAM kSudrANAJca sarvveSAM samIpe pramANaM dattvAdya yAvat tiSThAmi|
yaani ilimpasa Kristo ateseke na kuwa wa kwanza kufufuka kutoka wafu, ili atangaze kwamba mwanga wa ukombozi unawaangazia sasa watu wote, Wayahudi na pia watu wa mataifa mengine.”
24 tasyamAM kathAM nizamya phISTa uccaiH svareNa kathitavAn he paula tvam unmattosi bahuvidyAbhyAsena tvaM hatajJAno jAtaH|
Paulo alipofika hapa katika kujitetea kwake, Festo alisema kwa sauti kubwa, “Paulo! Una wazimu! Kusoma kwako kwingi kunakutia wazimu!”
25 sa uktavAn he mahAmahima phISTa nAham unmattaH kintu satyaM vivecanIyaJca vAkyaM prastaumi|
Lakini Paulo akasema, “Sina wazimu mheshimiwa Festo: Ninachosema ni ukweli mtupu.
26 yasya sAkSAd akSobhaH san kathAM kathayAmi sa rAjA tadvRttAntaM jAnAti tasya samIpe kimapi guptaM neti mayA nizcitaM budhyate yatastad vijane na kRtaM|
Wewe Mfalme unayafahamu mambo haya, kwa hiyo ninaweza kuongea bila uoga mbele yako. Sina mashaka kwamba matukio hayo yanajulikana kwako maana jambo hili halikutendeka mafichoni.
27 he AgripparAja bhavAn kiM bhaviSyadvAdigaNoktAni vAkyAni pratyeti? bhavAn pratyeti tadahaM jAnAmi|
Mfalme Agripa, je, una imani na manabii? Najua kwamba unaamini.”
28 tata AgrippaH paulam abhihitavAn tvaM pravRttiM janayitvA prAyeNa mAmapi khrISTIyaM karoSi|
Agripa akamjibu Paulo, “Kidogo tu utanifanya Mkristo!”
29 tataH so'vAdIt bhavAn ye ye lokAzca mama kathAm adya zRNvanti prAyeNa iti nahi kintvetat zRGkhalabandhanaM vinA sarvvathA te sarvve mAdRzA bhavantvitIzvasya samIpe prArthaye'ham|
Paulo akamjibu, “Namwomba Mungu kwamba, kwa muda mfupi au mrefu, si wewe tu bali wote wanaonisikia leo wapate kuwa kama nilivyo mimi, lakini bila hii minyororo.”
30 etasyAM kathAyAM kathitAyAM sa rAjA so'dhipati rbarNIkI sabhAsthA lokAzca tasmAd utthAya
Hapo mfalme Agripa, mkuu wa mkoa, Bernike na wale wote waliokuwa pamoja nao, walisimama.
31 gopane parasparaM vivicya kathitavanta eSa jano bandhanArhaM prANahananArhaM vA kimapi karmma nAkarot|
Walipokwisha ondoka, waliambiana, “Mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo au kifungo.”
32 tata AgrippaH phISTam avadat, yadyeSa mAnuSaH kaisarasya nikaTe vicArito bhavituM na prArthayiSyat tarhi mukto bhavitum azakSyat|
Naye Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeweza kufunguliwa kama asingalikuwa amekata rufani kwa Kaisari.”

< preritAH 26 >