< Первое послание к Коринфянам 1 >

1 Павел, зван Апостол Иисус Христов волею Божиею, и Сосфен брат,
Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
2 церкви Божией сущей в Коринфе, освященным о Христе Иисусе, званным святым, со всеми призывающими имя Господа нашего Иисуса Христа, во всяцем месте, тех же и нашем:
tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
3 благодать вам и мир от Бога Отца нашего и Господа Иисуса Христа.
Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4 Благодарю Бога моего всегда о вас, о благодати Божией данней вам о Христе Иисусе,
Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
5 яко во всем обогатистеся о Нем, во всяцем слове и всяцем разуме,
Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
6 якоже свидетелство Христово известися в вас:
kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
7 яко вам не лишитися ни во единем даровании, чающым откровения Господа нашего Иисуса Христа,
hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
8 Иже и утвердит вас даже до конца неповинных в день Господа нашего Иисуса Христа.
Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Верен Бог, Имже звани бысте во общение Сына Его Иисуса Христа, Господа нашего.
Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
10 Молю же вы, братие, именем Господа нашего Иисуса Христа, да тожде глаголете вси, и да не будут в вас распри, да будете же утверждени в томже разумении и в тойже мысли.
Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
11 Возвестися бо ми о вас, братие моя, (посланным) от Хлоиса, яко рвения в вас суть.
Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
12 Глаголю же се, яко кийждо вас глаголет: аз убо есмь Павлов, аз же Аполлосов, аз же Кифин, аз же Христов.
Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo,” mwingine: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo,”.
13 Еда разделися Христос, еда Павел распятся по вас? Или во имя Павлово крестистеся?
Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 Благодарю Бога, яко ни единаго от вас крестих, точию Криспа и Гаиа,
Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
15 да не кто речет, яко в мое имя крестих.
Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
16 Крестих же и Стефанинов дом: прочее не вем, аще кого иного крестих.
(Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
17 Не посла бо мене Христос крестити, но благовестити, не в премудрости слова, да не испразднится крест Христов.
Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
18 Слово бо крестное погибающым убо юродство есть, а спасаемым нам сила Божия есть.
Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
19 Писано бо есть: погублю премудрость премудрых, и разум разумных отвергу.
Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.”
20 Где премудр? Где книжник? Где совопросник века сего? Не обуи ли Бог премудрость мира сего? (aiōn g165)
Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
21 Понеже бо в премудрости Божией не разуме мир премудростию Бога, благоизволил Бог буйстовм проповеди спасти верующих.
Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
22 Понеже и Иудее знамения просят, и Еллини премудрости ищут:
Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
23 мы же проповедуем Христа распята, Иудеем убо соблазн, Еллином же безумие,
lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
24 самем же званным Иудеем же и Еллином Христа, Божию силу и Божию премудрость:
lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
25 зане буее Божие премудрее человек есть, и немощное Божие крепчае человек есть.
Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
26 Видите бо звание ваше, братие, яко не мнози премудри по плоти, не мнози сильни, не мнози благородни:
Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
27 но буяя мира избра Бог, да премудрыя посрамит, и немощная мира избра Бог, да посрамит крепкая:
Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
28 и худородная мира и уничиженная избра Бог, и не сущая, да сущая упразднит,
Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
29 яко да не похвалится всяка плоть пред Богом.
Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
30 Из Негоже вы есте о Христе Иисусе, Иже бысть нам премудрость от Бога, правда же и освящение и избавление,
Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
31 да, якоже пишется: хваляйся, о Господе да хвалится.
Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana.”

< Первое послание к Коринфянам 1 >