< Послание к Римлянам 15 >

1 Должни есмы мы сильнии немощи немощных носити, и не себе угождати:
Sisi tulio imara katika imani tunapaswa kuwasaidia wale walio dhaifu wayakabili matatizo yao. Tusijipendelee sisi wenyewe tu.
2 кииждо же вас ближнему да угождает во благое к созиданию.
Kila mmoja wetu anapaswa kumpendeza jirani yake kwa wema ili huyo apate kujijenga katika imani.
3 Ибо и Христос не Себе угоди, но якоже есть писано: поношения поносящих Тебе нападоша на Мя.
Maana Kristo hakujipendelea mwenyewe; ila alikuwa kama yasemavyo Maandiko: “Kashfa zote walizokutolea wewe zimenipata mimi.”
4 Елика бо преднаписана быша, в наше наказание преднаписашася, да терпением и утешением Писаний упование имамы.
Maana yote yalioandikwa yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi ili kutokana na saburi na faraja tupewayo na Maandiko hayo Matakatifu tupate kuwa na matumaini.
5 Бог же терпения и утешения да даст вам тожде мудрствовати друг ко другу о Христе Иисусе,
Mungu aliye msingi wa saburi na faraja yote, awajalieni ninyi kuwa na msimamo mmoja kufuatana na mfano wake Kristo Yesu,
6 да единодушно едиными усты славите Бога и Отца Господа нашего Иисуса Христа.
ili ninyi nyote, kwa nia moja na sauti moja, mumtukuze Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
7 Темже приемлите друг друга, якоже и Христос прият вас во славу Божию.
Basi, karibishaneni kwa ajili ya utukufu wa Mungu kama naye Kristo alivyowakaribisheni.
8 Глаголю же Христа Иисуса служителя бывша обрезания по истине Божией, во еже утвердити обетования отцев.
Maana, nawaambieni Kristo aliwatumikia Wayahudi apate kuonyesha uaminifu wa Mungu, na zile ahadi Mungu alizowapa babu zetu zipate kutimia;
9 А языком по милости, прославити Бога, якоже есть писано: сего ради исповемся Тебе во языцех, Господи, и имени Твоему пою.
ili nao watu wa mataifa mengine wapate kumtukuza Mungu kwa sababu ya huruma yake. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu hiyo, nitakusifu miongoni mwa watu wa mataifa. Nitaziimba sifa za jina lako.”
10 И паки глаголет: возвеселитеся, языцы, с людьми Его.
Tena Maandiko yasema: “Furahini, enyi watu wa mataifa; furahini pamoja na watu wake.”
11 И паки: хвалите Господа, вси языцы, и похвалите Его, вси людие.
Na tena: “Enyi mataifa yote, msifuni Bwana; enyi watu wote, msifuni.”
12 И паки Исаиа глаголет: будет корень Иессеов, и востаяй владети над языки: на Того языцы уповают.
Tena Isaya asema: “Atatokea mtu katika ukoo wa Yese, naye atawatawala watu wa mataifa; nao watamtumainia.”
13 Бог же упования да исполнит вас всякия радости и мира в вере, избыточествовати вам во уповании, силою Духа Святаго.
Basi, Mungu aliye msingi wa matumaini, awajazeni furaha yote na amani kutokana na imani yenu; tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
14 Извещен же есмь, братие моя, и сам аз о вас, яко и сами вы полни есте благости, исполнени всякаго разума, могуще и иныя научити:
Ndugu zangu, mimi binafsi nina hakika kwamba ninyi pia mmejaa wema, elimu yote, na mnaweza kushauriana ninyi kwa ninyi.
15 дерзее же писах вам, братие моя, от части, яко воспоминая вам, за благодать данную ми от Бога,
Lakini nimewaandikia hapa na pale katika barua hii bila woga, nipate kuwakumbusheni juu ya mambo fulani. Nimefanya hivyo kwa sababu ya neema aliyonijalia Mungu
16 во еже быти ми служителю Иисус Христову во языцех, священнодействующу благовествование Божие, да будет приношение еже от язык благоприятно и освященно Духом Святым.
ya kuwa mtumishi wa Yesu Kristo kwa watu wa mataifa. Ni jukumu langu la kikuhani kuihubiri Habari Njema ya Mungu ili watu wa mataifa mengine wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, dhabihu iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.
17 Имам убо похвалу о Христе Иисусе в тех, яже к Богу:
Kwa hiyo, nikiwa nimeungana na Kristo Yesu, naweza kujivunia huduma yangu kwa ajili ya Mungu.
18 не смею бо глаголати что, ихже не содея Христос мною, в послушание языков, словом и делом,
Sithubutu kusema kitu kingine chochote isipokuwa tu kile ambacho Kristo Yesu amekifanya kwa kunitumia mimi ili watu wa mataifa wapate kutii. Amefanya hivyo kwa maneno na vitendo,
19 в силе знамений и чудес, силою Духа Божия, якоже ми от Иерусалима и окрест даже до Иллирика исполнити благовествование Христово.
kwa nguvu ya miujiza na maajabu, na kwa nguvu ya Roho wa Mungu. Basi, kwa kusafiri kila mahali, tangu kule Yerusalemu mpaka Iluriko, nimeihubiri kikamilifu Habari Njema ya Kristo.
20 Сице же потщахся благовестити, не идеже именовася Христос, да не на чужем основании созижду,
Nia yangu imekuwa daima kuihubiri Habari Njema popote pale ambapo jina la Kristo halijapata kusikika, nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine.
21 но якоже есть писано: имже не возвестися о Нем, узрят, и иже не слышаша, уразумеют.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Watu wote ambao hawakuambiwa habari zote wataona; nao wale ambao hawajapata kusikia, wataelewa.”
22 Темже и возбранен бых многажды приити к вам.
Kwa sababu hiyo nilizuiwa mara nyingi kuja kwenu.
23 Ныне же ктому места не имыи в странах сих, желание же имый приити к вам от многих лет,
Lakini maadam sasa nimemaliza kazi yangu pande hizi, na kwa kuwa kwa miaka mingi nimekuwa na nia kubwa ya kuja kwenu,
24 яко аще поиду во Испанию, прииду к вам. Уповаю бо мимогрядый видети вас и вами проводитися тамо, аще вас прежде от части насыщуся.
natumaini kufanya hivyo sasa. Ningependa kuwaoneni nikiwa safarini kwenda Spania na kupata msaada wenu kwa safari hiyo baada ya kufurahia kuwa kwa muda pamoja nanyi.
25 Ныне же гряду во Иерусалим, служяй святым,
Lakini, kwa sasa nakwenda kuwahudumia watu wa Mungu kule Yerusalem.
26 благоволиша бо Македониа и Ахаиа общение некое сотворити к нищым святым живущым во Иерусалиме.
Maana makanisa ya Makedonia na Akaya yemeamua kutoka mchango wao kuwasaidia watu wa Mungu walio maskini huko Yerusalem.
27 Благоволиша бо, и должни им суть. Аще бо в духовных их причастницы быша языцы, должни суть и в плотских послужити им.
Wao wenyewe wameamua kufanya hivyo; lakini, kwa kweli, hilo ni jukumu lao kwa hao. Maana, ikiwa watu wa mataifa mengine wameshiriki baraka za kiroho za Wayahudi, wanapaswa nao pia kuwahudumia Wayahudi katika mahitaji yao ya kidunia.
28 Сие убо скончав, и запечатлев им плод сей, поиду вами во Испанию:
Nitakapokwisha tekeleza kazi hiyo na kuwakabidhi mchango huo uliokusanywa kwa ajili yao, nitawatembeleeni ninyi nikiwa safarini kwenda Spania.
29 вем же, яко грядый к вам, во исполнении благословения благовестия Христова прииду.
Najua ya kuwa nikija kwenu nitawaletea wingi wa baraka za Kristo.
30 Молю же вы, братие, Господем нашим Иисус Христом и любовию Духа, споспешствуите ми в молитвах о мне к Богу,
Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo, na kwa ajili ya upendo uletwao na Roho, mniunge mkono kwa kuniombea kwa Mungu.
31 да избавлюся от противляющихся во Иудеи, и да служба моя, яже во Иерусалиме, благоприятна будет святым.
Ombeni nipate kutoka salama miongoni mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, nayo huduma yangu huko Yerusalem ipate kukubaliwa na watu wa Mungu walioko huko.
32 Да с радостию прииду к вам волею Божиею и упокоюся с вами.
Hivyo, Mungu akipenda, nitaweza kuja kwenu na moyo wa furaha, nikapumzike pamoja nanyi.
33 Бог же мира со всеми вами. Аминь.
Mungu aliye chanzo cha amani na awe nanyi nyote! Amina!

< Послание к Римлянам 15 >