< 1 Nyakati 23 >

1 Daudi alipokuwa mzee aliyeshiba siku, akamfanya Solomoni mwanawe kuwa mfalme juu ya Israeli.
Therfor Dauid was eld and ful of daies, and ordeynede Salomon, his sone, kyng on Israel.
2 Pia akawakusanya pamoja viongozi wote wa Israeli, pamoja na makuhani na Walawi.
And he gaderide togidere alle the princes of Israel, and the preestis, and dekenes;
3 Walawi waliokuwa na umri wa miaka thelathini au zaidi walihesabiwa, nayo hesabu ya wanaume ilikuwa 38,000.
and the dekenes weren noumbrid fro twenti yeer and aboue, and eiyte and thretti thousynde of men weren foundun.
4 Daudi akasema, “Miongoni mwa hawa, 24,000 watasimamia kazi ya Hekalu la Bwana na 6,000 watakuwa maafisa na waamuzi,
And foure and twenty thousynde men weren chosun of hem, and weren departid in to the seruyce of the hows of the Lord; sotheli of souereyns, and iugis, sixe thousynde;
5 na 4,000 watakuwa mabawabu, na wengine 4,000 watamsifu Bwana kwa ala za uimbaji nilizotoa kwa ajili ya kusudi hilo.”
forsothe foure thousynde `porteris weren, and so many syngeris, syngynge to the Lord in orguns, whiche Dauid hadde maad for to synge.
6 Daudi akawagawa Walawi katika makundi kufuatana na wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.
And Dauid departide hem bi the whilis of the sones of Leuy, that is, of Gerson, and of Caath, and Merary.
7 Wana wa Wagershoni walikuwa wawili: Ladani na Shimei.
And the sones of Gerson weren Leedan and Semeye.
8 Wana wa Ladani walikuwa watatu: Yehieli wa kwanza, Zethamu na Yoeli.
The sones of Leedan weren thre, the prince Jehiel, and Ethan, and Johel.
9 Wana wa Shimei walikuwa watatu: Shelomothi, Hazieli na Harani. Hawa watatu walikuwa viongozi wa jamaa za Ladani.
The sones of Semei weren thre, Salamyth, and Oziel, and Aram; these weren the princes of the meynees of Leedan.
10 Nao wana wa Shimei walikuwa wanne: Yahathi, Zina, Yeushi na Beria.
Forsothe the sones of Semeye weren Leeth, and Ziza, and Yaus, and Baria, these foure weren the sones of Semei.
11 Yahathi alikuwa wa kwanza na Ziza wa pili, lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; kwa hiyo walihesabiwa kama jamaa moja, wakapewa wajibu kwa pamoja.
Sotheli Leeth was the formere, and Ziza the secounde; forsothe Yaus and Baria hadden not ful many sones, and therfor thei weren rikenyd in o meynee and oon hows.
12 Wana wa Kohathi walikuwa wanne: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.
The sones of Caath weren foure, Amram, and Ysaac, Ebron, and Oziel.
13 Wana wa Amramu walikuwa: Aroni na Mose. Aroni waliwekwa wakfu, yeye na wazao wake milele, wawe wakiweka wakfu vitu ambavyo ni vitakatifu mno, kutoa dhabihu mbele za Bwana, kuhudumu mbele zake na kutamka baraka katika Jina la Bwana milele.
The sones of Amram weren Aaron and Moyses; and Aaron was departid, that he schulde mynystre in the hooli thing of hooli thingis, he and hise sones with outen ende, and to brenne encense to the Lord bi his custom, and to blesse his name with outen ende.
14 Wana wa Mose mtu wa Mungu walihesabiwa kama sehemu ya kabila la Lawi.
Also the sones of Moyses, man of God, weren noumbrid in the lynage of Leuy.
15 Wana wa Mose walikuwa: Gershomu na Eliezeri.
The sones of Moises weren Gerson and Elieser.
16 Wazao wa Gershomu: Shebueli alikuwa wa kwanza.
The sones of Gerson; `Subuhel the firste.
17 Wazao wa Eliezeri: Rehabia alikuwa wa kwanza. Eliezeri alikuwa na mwana mmoja tu, lakini wana wa Rehabia walikuwa wengi sana.
Sotheli the sones of Eliezer weren Roboya the firste, and othere sones weren not to Eliezer; forsothe the sones of Roboia weren multipliede ful miche.
18 Wana wa Ishari: Shelomithi alikuwa wa kwanza.
The sones of Isaar; `Salumuth the firste.
19 Wana wa Hebroni walikuwa: Yeria alikuwa wa kwanza, wa pili Amaria, wa tatu Yahazieli, na wa nne Yekameamu.
The sones of Ebron; `Jerian the firste, Amarias the secounde, Jaziel the thridde, Jethamaan the fourthe.
20 Wana wa Uzieli walikuwa: Mika wa kwanza na Ishia wa pili.
The sones of Oziel; `Mycha the firste, Jesia the secounde.
21 Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Wana wa Mahli walikuwa: Eleazari na Kishi.
The sones of Merari weren Mooli and Musi. The sones of Mooli weren Eleazar, and Cys.
22 Eleazari akafa bila ya kuwa na wana: alikuwa na binti tu. Binamu zao, wana wa Kishi, wakawaoa.
Sotheli Eleazar was deed, and hadde not sones, but douytris; and the sones of Cys, the britheren of hem, weddiden hem.
23 Wana wa Mushi: Mahli, Ederi na Yeremothi; wote walikuwa watatu.
The sones of Musi weren thre, Mooli, and Heder, and Jerymuth.
24 Hawa walikuwa wazao wa Lawi kwa jamaa zao. Wakuu wa jamaa kama walivyoandikwa kwa majina yao na kuhesabiwa kila mmoja, yaani, wenye uwezo wa kufanya kazi kuanzia miaka ishirini au zaidi, waliohudumu katika Hekalu la Bwana.
These weren the sones of Leuy in her kynredis and meynees, prynces bi whilis, and noumbre of alle heedis, that diden the trauel of the seruyce of the hows of the Lord, fro twenti yeer and aboue.
25 Kwa maana Daudi alikuwa amesema, “Kwa vile Bwana, Mungu wa Israeli amewapa watu wake raha na amekuja kuishi Yerusalemu milele,
For Dauid seide, The Lord God of Israel hath youe reste to his puple, and a dwellyng in Jerusalem til in to with outen ende;
26 Walawi hawahitaji tena kubeba Maskani wala chombo chochote cha utumishi wake.”
and it schal not be the office of dekenes for to bere more the tabernacle, and alle vessels therof for to mynystre.
27 Kulingana na maagizo ya mwisho ya Daudi, Walawi waliohesabiwa ni wale wa kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi.
Also bi the laste comaundementis of Dauid the noumbre of the sones of Leuy schulen be rikened fro twenti yeer and aboue;
28 Wajibu wa Walawi ulikuwa kuwasaidia wazao wa Aroni kuhudumu katika Hekalu la Bwana: Kuwa wasimamizi wa nyua, vyumba vya pembeni, kutakasa vyombo vitakatifu na utendaji mwingine wowote katika nyumba ya Mungu.
and thei schulen be vndir the hond of the sones of Aaron in to the worschipe of the hows of the Lord, in porchis, and in chaumbris, and in the place of clensyng, and in the seyntuarie, and in alle werkis of the seruyce of the temple of the Lord.
29 Walikuwa wasimamizi wa mikate iliyowekwa mezani, unga kwa ajili ya sadaka za nafaka, mikate isiyotiwa chachu, uokaji na uchanganyaji, pamoja na vipimo vyote vya wingi na ukubwa.
Forsothe preestis schulen be ouer the looues of proposicioun, and to the sacrifice of flour, and to the pastis sodun in watir, and to the therf looues, and friyng panne, and to hoot flour, and to seenge, and ouer al weiyte and mesure.
30 Pia ulikuwa wajibu wao kila asubuhi kumshukuru na kumsifu Bwana. Iliwapasa pia kufanya hivyo jioni
Forsothe the dekenes schulen be, that thei stonde eerli, for to knowleche and synge to the Lord, and lijk maner at euentide,
31 na wakati wowote sadaka za kuteketezwa zilipotolewa kwa Bwana siku za Sabato na kwenye sikukuu za Mwezi Mwandamo na katika sikukuu nyingine zilizoamriwa. Iliwapasa kuhudumu mbele za Bwana mara kwa mara kwa idadi maalum na kwa namna waliyokuwa wamepewa maelekezo.
as wel in the offryng of brent sacrifices of the Lord, as in sabatis, and kalendis, and othere solempnytees, bi the noumbre and cerymonyes of eche thing contynueli bifor the Lord;
32 Hivyo Walawi wakafanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, katika Mahali Patakatifu chini ya uongozi wa ndugu zao wazao wa Aroni, kwa ajili ya utumishi katika Hekalu la Bwana.
and that thei kepe the obseruaunces of the tabernacle of the boond of pees of the Lord, and the custum of the seyntuarie, and the obseruaunce of the sones of Aaron, her britheren, that thei mynystre in the hows of the Lord.

< 1 Nyakati 23 >