< 1 Wathesalonike 5 >

1 Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
Über Zeit und Zeitumstände, Brüder, ist nicht Not, euch zu schreiben;
2 kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
Ihr wißt ja selbst genau, daß der Tag des Herrn kommen wird wie ein Dieb in der Nacht.
3 Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
Denn wenn sie sagen: Es ist Friede, ist keine Gefahr, so steht plötzlich das Verderben vor der Tür, wie die Wehen vor dem Weib, das gebären soll; und sie können nicht entfliehen.
4 Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
Ihr aber, Brüder, seid nicht in Finsternis, so daß euch der Tag wie der Dieb überfalle.
5 Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
Ihr alle seid ja Kinder des Lichts und Kinder des Tags; wir sind nicht von der Nacht, noch von der Finsternis.
6 Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
So laßt uns denn nicht schlafen, wie die anderen, sondern wachen und nüchtern sein.
7 Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
Denn die da schlafen, schlafen in der Nacht, und die da trunken sind, sind trunken in der Nacht.
8 Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
Wir aber, die wir vom Tage sind, wollen nüchtern sein, mit dem Panzer des Glaubens und der Liebe angetan, und mit dem Helm der Hoffnung zur Seligkeit.
9 Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Denn Gott hat uns nicht gesetzt zum Zorn, sondern zur Erlangung der Seligkeit durch unseren Herrn Jesus Christus, Der für uns gestorben ist.
10 Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
Auf daß wir, ob wir wachen oder schlafen, zugleich mit Ihm leben sollen.
11 Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
Darum ermahnt einander und erbaue einer den anderen, wie ihr denn auch tut.
12 Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
Wir bitten euch aber, Brüder, daß ihr sorgt für die, welche an euch arbeiten und euch vorstehen in dem Herrn und euch vermahnen.
13 Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
Und haltet sie hoch in eurer Liebe, um ihres Werkes willen. Haltet Frieden untereinander.
14 Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
Wir ermahnen euch aber, liebe Brüder, weiset zurecht die Unordentlichen, tröstet die Kleinmütigen, nehmt euch der Schwachen an, seid langmütig gegen alle.
15 Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
Seht darauf, daß keiner Böses mit Bösem vergelte, sondern jagt allezeit dem Guten nach, beides, untereinander und gegen jedermann.
16 Furahini siku zote;
Seid allezeit frohen Mutes.
17 ombeni bila kukoma;
Betet ohne Unterlaß.
18 shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
Seid dankbar in allen Dingen, denn das ist der Wille Gottes in Christus Jesus an euch.
19 Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
Den Geist dämpfet nicht.
20 msiyadharau maneno ya unabii.
Mißachtet nicht Weissagungen,
21 Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
Sondern prüft alles, das Gute behaltet!
22 Jiepusheni na uovu wa kila namna.
Meidet allen bösen Schein.
23 Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
Er aber, der Gott des Friedens, heilige euch durch und durch, und Geist, Seele und Leib möge an euch völlig unsträflich erhalten werden für die Zukunft unseres Herrn Jesus Christus.
24 Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
Treu ist Er, Der euch ruft, und wird es auch vollbringen.
25 Ndugu, tuombeeni.
Brüder, betet für uns!
26 Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
Grüßet alle Brüder mit dem heiligen Kuß.
27 Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
Ich beschwöre euch bei dem Herrn, daß ihr diesen Brief alle heiligen Brüder lesen lasset.
28 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.
Die Gnade unseres Herrn Jesu Christi sei mit euch! Amen.

< 1 Wathesalonike 5 >