< Matendo 28 >

1 Baada ya kufika nchi kavu salama, ndipo tukafahamu kwamba jina la kile kisiwa ni Malta.
得救以後,那時纔知道這島名叫默里達。
2 Wenyeji wa kile kisiwa wakatufanyia ukarimu usio wa kawaida. Waliwasha moto na kutukaribisha sisi sote kwa sababu mvua ilikuwa inanyesha na kulikuwa na baridi.
土人待我們非常友善,因為當時正在下雨,天又寒冷,他們就生起一堆火來款待我們眾人。
3 Paulo alikuwa amekusanya mzigo wa kuni na alipokuwa anaweka kwenye moto kwa ajili ya joto, nyoka mwenye sumu akatoka humo na kujisokotea mkononi mwake.
保祿拾了一捆柴,放在火堆上;有一條毒蛇,因熱而出,纏住了他的手。
4 Wale wenyeji wa kile kisiwa walipomwona yule nyoka akiningʼinia mkononi mwa Paulo, wakaambiana, “Huyu mtu lazima awe ni muuaji, ingawa ameokoka kutoka baharini, haki haijamwacha aishi.”
土人一見毒蛇在保祿手上懸著,就彼此說:「這人必定是個兇手,雖然他從海裏得了救,天理仍不容他活著。」
5 Lakini Paulo akamkungʼutia yule nyoka ndani ya moto wala yeye hakupata madhara yoyote.
保祿竟把那毒蛇抖在火裏,一點也沒有受害;
6 Watu walikuwa wanangoja avimbe au aanguke ghafula na kufa. Lakini baada ya kungoja kwa muda mrefu na kuona kwamba hakuna chochote kisicho cha kawaida kilichomtokea, wakabadili mawazo yao na kuanza kusema kwamba yeye ni mungu.
他們等待保祿發腫,或者突然跌倒死去;但等了好久,見沒有一點不對的地方在他身上發生,就轉念說他是個神。
7 Basi karibu na sehemu ile, palikuwa na shamba kubwa la mtu mmoja kiongozi wa kile kisiwa, aliyeitwa Publio. Alitupokea na akatuhudumia kwa ukarimu mkubwa kwa muda wa siku tatu.
離那地方不遠,有一塊田園,是島上的首領名叫頗里約的;他收留我們,款待了我們三天,很是厚道。
8 Baba yake Publio alikuwa mgonjwa kitandani, akiwa anaumwa homa na kuhara damu. Paulo akaingia ndani ili kumwona na baada ya maombi, akaweka mikono juu yake na kumponya.
適馮頗里約的父親臥病,患熱病和痢疾;保祿就到他那裏,祈禱以後,給他覆手,治好了他。
9 Jambo hili lilipotukia, watu wote wa kisiwa kile waliokuwa wagonjwa wakaja, nao wakaponywa.
這樣一來,島上其餘有病的人也都前來,也全被治好了。
10 Wakatupa heshima nyingi, nasi tulipokuwa tayari kusafiri kwa njia ya bahari, wakapakia melini vitu vyote tulivyokuwa tunavihitaji.
他們處處表示十分尊敬我們;當我們開船的時候,還給我們放上急需品。
11 Miezi mitatu baadaye tukaanza safari kwa meli iliyokuwa imetia nanga kwenye kisiwa hicho kwa ajili ya majira ya baridi. Hii ilikuwa meli ya Iskanderia yenye alama ya miungu pacha waitwao Kasta na Poluksi.
有隻用「雕斯雇黎」作標幟的亞歷山大里亞船,在那島上過冬:過了三個月,我們便乘這船航行。
12 Kituo chetu cha kwanza kilikuwa Sirakusa na tukakaa huko siku tatu.
我們在息辣谷撒靠了岸,停留了三天;
13 Kisha tukangʼoa nanga, tukafika Regio. Siku iliyofuata, upepo mkali wa kusi ukavuma, na siku ya pili yake tukafika Puteoli.
從這裏繞道前行,到了勒基雍。過了一夜,吹起了南風,次日我們就到了頗提約里;
14 Huko tukawakuta ndugu, nasi tukakaribishwa tukae nao kwa siku saba. Hivyo tukaendelea na safari mpaka Rumi.
在那裏我們遇見了弟兄們,他們請我們在那裏住了七天;以後,我們便往羅馬去了。
15 Ndugu wa huko Rumi waliposikia habari zetu, walikuja mpaka Soko la Apio na mahali paitwapo Mikahawa Mitatu kutulaki. Paulo alipowaona, alimshukuru Mungu akatiwa moyo.
弟兄們聽到我們的消息後,便從羅馬來到阿丕約市場和三館迎接我們;保祿見了他們,就感謝天主,而獲得勇氣。
16 Tulipofika Rumi, Paulo aliruhusiwa kuishi peke yake akiwa na askari wa kumlinda.
我們進了羅馬,保祿獲准與看守他的士兵獨居一處。
17 Siku tatu baadaye Paulo akawaita pamoja viongozi wa Kiyahudi. Walipokwisha kukusanyika akawaambia, “Ndugu zangu, ingawa sikufanya jambo lolote dhidi ya watu wetu au dhidi ya desturi za baba zetu, lakini nilikamatwa huko Yerusalemu nikakabidhiwa kwa Warumi.
過了三天,保祿便召集猶太人的首領;待他們來齊了,就向他們說:「諸位仁人弟兄!論到我,我雖沒有行什麼反對民族,或祖先規例的事,卻被鎖押了,從耶路撒冷被交到羅馬人手裏。
18 Wao walipokwisha kunihoji, wakataka kuniachia huru kwa sababu hawakuona kosa lolote nililolifanya linalostahili adhabu ya kifo.
他們審問了我,在我身上沒有找到該死的罪案,就想釋放我;
19 Lakini Wayahudi walipopinga uamuzi huo, nililazimika kukata rufaa kwa Kaisari, ingawa sikuwa na lalamiko lolote juu ya taifa langu.
但猶太人反對,我不得已,只好向凱撒上訴,並不是我有什麼事要控告我的人民。
20 Basi hii ndiyo sababu nimewatumania, ili niseme nanyi. Kwa kuwa ni kwa ajili ya tumaini la Israeli nimefungwa kwa minyororo.”
為這個緣故,我纔請你們來見面談話。我原是為了以色列所希望的事,纔帶上了這條鎖鏈。」
21 Wakamjibu, “Hatujapokea barua zozote kutoka Uyahudi zinazokuhusu, wala hapana ndugu yeyote aliyekuja hapa ambaye ametoa taarifa au kuzungumza jambo lolote baya juu yako.
他們向他說:「我們沒有從猶太接到關於你的書信,弟兄們中也沒有一個人來報告,或說你有什麼不好;
22 Lakini tungependa kusikia kutoka kwako unalofikiri kwa sababu tunajua kwamba kila mahali watu wanazungumza mabaya kuhusu jamii hii.”
不過我們願意從你本人聽聽你的意見,因為關於這個教門,我們知道它到處受人反對。」
23 Baada ya kupanga siku ya kuonana naye, watu wengi wakaja kuanzia asubuhi hadi jioni akawaeleza na kutangaza kuhusu Ufalme wa Mungu akijaribu kuwahadithia juu ya Yesu kutoka Sheria ya Mose na kutoka Manabii.
他們既與保祿約定了日子,就有更多的人到寓所來見他;他就從早到晚,給他們講解,為天主的國作證,引徵梅瑟法律和先知書,勸導他們信服耶穌。
24 Baadhi wakasadiki yale aliyosema, lakini wengine hawakuamini.
有的人因他所說的話而相信了,有的卻不相信;
25 Hivyo hawakukubaliana, nao walipokuwa wanaondoka, Paulo akatoa kauli moja zaidi: “Roho Mtakatifu alinena kweli na baba zenu aliposema mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu kwa kinywa cha nabii Isaya kwamba:
他們彼此不合,便散去了。散去之前,保祿曾說了這段話:「聖神藉依撒意亞先知向你們祖先說的正對。
26 “‘Nenda kwa watu hawa na useme, “Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa; na pia mtatazama, lakini hamtaona.”
他說:『你去對這民族說:你們聽是聽,但不了解;看是看,卻不明白,
27 Kwa kuwa mioyo ya watu hawa imekuwa migumu; hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba macho yao. Wasije wakaona kwa macho yao, na wakasikiliza kwa masikio yao, wakaelewa kwa mioyo yao, na kugeuka nami nikawaponya.’
因為這民族的心遲鈍,耳朵難以聽見;他們閉了自己的眼睛,免得眼睛看見,耳朵聽見,心裏了解而悔改,而要我醫好他們。』
28 “Basi na ijulikane kwenu kwamba, huu wokovu wa Mungu umepelekwa kwa watu wa Mataifa, nao watasikiliza.” [
所以,你們要知道:
29 Naye akiisha kusema maneno haya, Wayahudi wakaondoka wakiwa na hoja nyingi miongoni mwao.]
天主的這個救恩已送給了外邦人,他們將要聽從。」
30 Kwa miaka miwili mizima Paulo alikaa huko kwa nyumba aliyokuwa amepanga. Akawakaribisha wote waliokwenda kumwona.
保祿在自己賃的房子裏,住了整整兩年;凡來見他的,他都接待。
31 Akahubiri Ufalme wa Mungu na kufundisha mambo yale yaliyomhusu Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri wote na bila kizuizi chochote.
他宣講天主的國,教授主耶穌基督的事,都非常自由,沒有人禁止。

< Matendo 28 >