< Torati 3 >

1 Kisha tukageuka tukakwea kufuata njia iliyoelekea Bashani, Ogu mfalme wa Bashani akaondoka na jeshi lake lote kupigana na sisi huko Edrei.
And we turned and we went up [the] way of Bashan and he came forth Og [the] king of Bashan to meet us he and all people his for battle Edrei.
2 Bwana akaniambia, “Usimwogope kwa kuwa nimekwisha mkabidhi mikononi mwako pamoja na jeshi lake lote na nchi yake. Umfanyie sawasawa na ulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni.”
And he said Yahweh to me may not you fear him for in hand your I give him and all people his and land his and you will do to him just as you did to Sihon [the] king of the Amorite[s] who [was] dwelling in Heshbon.
3 Hivyo Bwana Mungu wetu pia akamweka Ogu mfalme wa Bashani pamoja na jeshi lake lote mikononi mwetu. Tuliwaangamiza wote, hakubakia hata mmoja.
And he gave Yahweh God our in hand our also Og [the] king of Bashan and all people his and we struck down him until not he had left to him a survivor.
4 Wakati huo tuliteka miji yake yote. Hakuna mji hata mmoja kati ya ile sitini ambao hatukuuteka, yaani eneo lote la Argobu, utawala wa Mfalme Ogu katika Bashani.
And we captured all cities his at the time that not it was a town which not we took from with them sixty citi[es] all [the] region of Argob [the] kingdom of Og in Bashan.
5 Miji yote hii ilijengewa ngome zenye kuta ndefu zenye malango na makomeo, pia kulikuwako na vijiji vingi ambavyo havikujengewa kuta.
All these [were] cities fortified wall high gates and bar[s] apart from [the] cities of the hamlet-dweller[s] many very.
6 Tuliwaangamiza kabisa, kama tulivyomfanyia Sihoni mfalme wa Heshboni, tukiangamiza kila mji, yaani wanaume, wanawake na watoto.
And we totally destroyed them just as we had done to Sihon [the] king of Heshbon we totally destroyed every city of men the women and the little one[s].
7 Lakini wanyama wote wa kufuga pamoja na nyara kutoka kwenye miji yao tulichukua vikawa vyetu.
And all the livestock and [the] booty of the cities we plundered for ourselves.
8 Hivyo kwa wakati huo tukachukua kutoka kwa wafalme hawa wawili wa Waamori nchi ya mashariki ya Yordani, kutoka Bonde la Arnoni mpaka kufika kwenye Mlima Hermoni.
And we took at the time that the land from [the] hand of [the] two [the] kings of the Amorite[s] who [were] on [the] other side of the Jordan from [the] wadi of Arnon to [the] mountain of Hermon.
9 (Wasidoni huuita mlima huo Sirioni, nao Waamori huuita Seniri.)
[the] Sidonians They call Hermon Sirion and the Amorite[s] they call it Senir.
10 Tuliteka miji yote kwenye uwanda wa juu, Gileadi yote, Bashani yote mpaka kufika Saleka na Edrei, miji ya utawala wa Ogu huko Bashani.
All - [the] cities of the plain and all Gilead and all Bashan to Salecah and Edrei [the] cities of [the] kingdom of Og in Bashan.
11 (Mfalme Ogu wa Bashani ndiye peke yake aliyesalia miongoni mwa mabaki ya Warefai. Kitanda chake kilikuwa cha chuma chenye urefu wa dhiraa tisa na upana wa dhiraa nne. Mpaka sasa kinaweza kuonekana katika mji wa Waamoni wa Raba.)
For only Og [the] king of Bashan he survived from [the] remnant of the Rephaites there! sarcophagus his [was] a sarcophagus of iron ¿ not [is] it in Rabbah of [the] people of Ammon [was] nine cubits length its and [was] four cubits breadth its by a cubit of a human.
12 Katika nchi tuliyoiteka wakati ule, niliwapa kabila la Reubeni na Gadi eneo lililoko kaskazini la Aroeri kando ya Bonde la Arnoni, na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.
And the land this we took possession of at the time that from Aroer which [was] at [the] wadi of Arnon and [the] half of [the] hill country of Gilead and cities its I gave to the Reubenite[s] and to the Gadite[s].
13 Kisha nusu ya kabila la Manase niliwapa sehemu ya Gileadi iliyobaki pamoja na Bashani yote, ambayo ilikuwa utawala wa Ogu. (Eneo lote la Argobu katika Bashani lilikuwa linajulikana kama nchi ya Warefai.
And [the] remainder of Gilead and all Bashan [the] kingdom of Og I gave to [the] half of [the] tribe of Manasseh all [the] region of Argob to all Bashan it it was called [the] land of [the] Rephaites.
14 Yairi, mzao wa kabila la Manase, alichukua eneo lote la nchi ya Argobu hadi kufikia mpaka wa Wageshuri na Wamaaka, ukaitwa kwa jina lake; kwa hiyo mpaka leo hii Bashani inaitwa Hawoth-Yairi.)
Jair [the] son of Manasseh he took all [the] region of Argob to [the] border of the Geshurite[s] and the Maacathite[s] and he called them on own name his Bashan [the] villages of Jair until the day this.
15 Nikampa Makiri nchi ya Gileadi.
And to Makir I gave Gilead.
16 Lakini niliwapa Wareubeni na Wagadi eneo kuanzia Gileadi hadi Bonde la Arnoni (katikati ya bonde ulikuwa ndio mpaka), kuelekea mpaka Mto Yaboki, ambao ndio mpaka wa Waamoni.
And to the Reubenite[s] and to the Gadite[s] I gave from Gilead and to [the] wadi of Arnon [the] middle of the wadi and a border and to Jabbok the wadi [is] [the] border of [the] people of Ammon.
17 Kwa upande wa magharibi mpaka wao ulikuwa Yordani katika Araba, toka ziwa Galilaya hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), kwenye miteremko ya Pisga upande wa mashariki.
And the Arabah and the Jordan and a border from Kinnereth and to [the] sea of the Arabah [the] Sea of Salt under [the] slopes of Pisgah east-ward.
18 Wakati huo nilikuamuru: “Bwana Mungu wako amekupa nchi hii uimiliki. Lakini ni lazima wanaume wenu wote wenye uwezo, wakiwa wamejiandaa tayari kwa vita, wavuke ngʼambo wakiwatangulia ndugu zako Waisraeli.
And I commanded you at the time that saying Yahweh God your he has given to you the land this to take possession of it equipped you will pass over before countrymen your [the] people of Israel O all [the] sons of strength.
19 Lakini wake zenu, watoto wenu na mifugo yenu (kwani najua mnayo mifugo mingi) wanaweza kukaa katika miji niliyowapa,
Only wives your and little one[s] your and livestock your I know that livestock much [belongs] to you they will remain in cities your which I have given to you.
20 mpaka hapo Bwana atakapowapa ndugu zenu kupumzika kama alivyowapa ninyi, wao pia wamiliki ile nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, ngʼambo ya Yordani. Baada ya hapo, kila mmoja wenu anaweza kurudi kwenye milki niliyowapa.”
Until that he will give rest Yahweh - to countrymen your like you and they will take possession of also they the land which Yahweh God your [is] about to give to them on [the] other side of the Jordan and you will return everyone to possession his which I have given to you.
21 Wakati huo nilimwamuru Yoshua, “Umejionea kwa macho yako mwenyewe yale yote ambayo Bwana Mungu wenu amewafanyia wafalme hawa wawili. Bwana atazifanyia falme zote huko mnakokwenda vivyo hivyo.
And Joshua I commanded at the time that saying eyes your [are] the [ones which] have seen all that he did Yahweh God your to [the] two the kings these thus he will do Yahweh to all the kingdoms where you [are] about to pass over there.
22 Msiwaogope, Bwana Mungu wenu atapigana kwa ajili yenu.”
Not you must fear them for Yahweh God your he [is] the [one who] will fight for you.
23 Wakati huo nilimsihi Bwana:
And I sought favor to Yahweh at the time that saying.
24 “Ee Bwana Mwenyezi, umemwonyesha mtumishi wako ukuu wako na mkono wako wenye uweza. Kwa kuwa ni mungu yupi aliye mbinguni au duniani anayeweza kufanya kazi na matendo makuu kama ufanyayo wewe?
O Lord Yahweh you you have begun to show servant your greatness your and hand your strong that who? [is] God in the heavens and on the earth who he will do like works your and like mighty deeds your.
25 Acha niende nikaione hiyo nchi nzuri ngʼambo ya Yordani, ile nchi nzuri ya vilima na Lebanoni.”
Let me pass over please so I may see the land good which [is] on [the] other side of the Jordan the hill country good this and Lebanon.
26 Lakini kwa sababu yenu Bwana alinikasirikia na hakutaka kunisikiliza. Bwana aliniambia, “Hilo latosha; usiseme nami jambo hili tena.
And he was furious Yahweh with me on account of you and not he listened to me and he said Yahweh to me enough for you may not you repeat to speak to me again in the matter this.
27 Kwea juu ya kilele cha Pisga uangalie magharibi, kaskazini, kusini na mashariki. Iangalie hiyo nchi kwa macho yako, kwa vile wewe hutavuka Yordani.
Go up - [the] top of Pisgah and lift up eyes your west-ward and north-ward and south-ward and east-ward and see with own eyes your that not you will pass over the Jordan this.
28 Lakini mwagize Yoshua, mtie moyo na umtie nguvu, kwa kuwa yeye atawaongoza watu hawa hadi ngʼambo na kuwarithisha nchi utakayoiona.”
And commission Joshua and encourage him and strengthen him for he he will pass over before the people this and he he will give as an inheritance them the land which you will see.
29 Kwa hiyo tulikaa kwenye bonde karibu na Beth-Peori.
And we remained in the valley opposite to Beth Peor.

< Torati 3 >