< Ezekieli 32 >

1 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema:
Aa ie amy androm-baloha’ ty volam-paha-folo-ro’ ambi’ i taom-paha-folo-roe-ambiy, le niheo amako ty tsara’ Iehovà manao ty hoe:
2 “Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie: “‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa, wewe ni kama joka kubwa baharini, unayevuruga maji kwa miguu yako na kuchafua vijito.
O ana’ondatio, ampionjono bekom-pandalàñe t’i Parò mpanjaka’ i Mitsraime le ano ty hoe, Hambañe ami’ty liona tora’e añivo’ o kilakila’ ndatio irehe, naho manahake ty trozoñe an-driak’ ao, ie nitsititiak’ amo saka’oo, naho nitsoborè’o am-pandia o ranoo, vaho linoto’o o fitsiritsioha’eo.
3 “‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu nitautupa wavu wangu juu yako, nao watakukokota katika wavu wangu.
Aa hoe ty nafè’Iehovà Talè: Ami’ty firimboñam-pifokoañe maro le halafiko ama’o ty harato, vaho hampionjoneñe an-karatoko boak’ ao.
4 Nitakutupa nchi kavu na kukuvurumisha uwanjani. Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako na wanyama wote wa nchi watajishibisha nyama yako.
Le hafetsako an-tamboho eo, naho havokovokoko an-kivoke eo, hampivotraheko ama’o o voron-dikerañeo, vaho ho vontsiñeko ama’o iaby ze kila bibi’ ty tane toy.
5 Nitatawanya nyama yako juu ya milima na kujaza mabonde kwa mabaki yako.
Le hapoko amo haboañeo ty nofo’o, naho ho liporeko ami’ty haleora’o o vavataneo.
6 Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka njia yote hadi milimani, nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.
Ho tondrahako amo lio’o midoandoañeo i tane ilañoa’oy, pak’ am-bohitse ey; vaho ihe ty hibanara’ o sakao.
7 Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu na kuzitia nyota zake giza; nitalifunika jua kwa wingu, nao mwezi hautatoa nuru yake.
Aa ie nampimongoreko, ho kolopofako i likerañey naho hanoeko maieñe o vasia’eo; ho saroñeko rahoñe i àndroy, vaho tsy hañomey ty hazavà’e i volañey.
8 Mianga yote itoayo nuru angani nitaitia giza juu yako; nitaleta giza juu ya nchi yako, asema Bwana Mwenyezi.
Hampimoromoroñeko ze hene hazavàñe mireandreañe an-dikerañe ey ty ama’o, vaho hapoko an-tane’o ao ty ieñe, hoe t’Iehovà Talè.
9 Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa, nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi ambazo haujapata kuzijua.
Hampilonjereko ty arofo’ ondaty maro, ie hafetsako amo kilakila’ ndatio ty firotsaha’o, amo fifeheañe mboe tsy fohi’oo.
10 Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie, wafalme wao watatetemeka kwa hofu kwa ajili yako nitakapotikisa upanga wangu mbele yao. Siku ya anguko lako kila mmoja wao atatetemeka kila dakika kwa ajili ya maisha yake.
Vaho hampilatsàko ty rofòko maro, hampangebahebaheñe ty ama’o o mpanjaka’eo, ie ahelahelako aolo’ iareo eo ty fibarako, ie hitolom-pihondrahondra, songa hirombak’ aiñe, amy andro hikorovoha’oy.
11 “‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja dhidi yako.
Aa hoe ty nafè’ Iehovà Talè: Hiambotrak’ ama’areo ty fibaram-panjaka’ i Bavele.
12 Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka kwa panga za watu mashujaa, taifa katili kuliko mataifa yote. Watakivunjavunja kiburi cha Misri, nayo makundi yake yote ya wajeuri yatashindwa.
Ty fibara’ o fanalolahio ty hampihotrako ondati’oo; songa lahitsiay amo kilakila’ ndatio; Ho rotsahe’ iareo ty firengevoha’ i Mitsraime, vaho kila haitoañe i valobohò’ey.
13 Nitaangamiza mifugo yake yote wanaojilisha kando ya maji mengi, hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu wala kwato za mnyama hazitayachafua tena.
Ho fonga zamaneko o hare’eo boak’ amo rano’e maroo; le lia’e tsy ho lotoem-pandia’ ondaty ndra hòtrom-biby.
14 Kisha nitafanya maji yake yatulie na kufanya vijito vyake vitiririke kama mafuta, asema Bwana Mwenyezi.
hampidreteko o saka’eo, hampitsiritsioheko hoe menake o toraha’eo, hoe t’Iehovà Talè.
15 Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa na kuiondolea nchi kila kitu kilichomo ndani yake, nitakapowapiga wote waishio humo, ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’
Ie hampangoakoaheko ty tane’ i Mitsraime, ho tavaneñe añe ty havokara’ i taney, naho lafaeko iaby o mpimoneñeo, le ho fohi’ iereo te Izaho Iehovà.
16 “Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”
Izay i bekom-pandalàñey le ho saboe’ iereo; ho saboe’ o anak’ ampela’ o kilakila’ ndatio, vaho ho bekoe’ iereo amy Mitsraime naho amo valobohò’e iabio, hoe t’Iehovà Talè.
17 Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema:
Ie amy androm-paha-folo-lim’ ambi’ i volañeiy amy taom-paha-folo-roe ambiy, le niheo amako ty tsara’ Iehovà, manao ty hoe:
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. (questioned)
O ana’ ondatio, mibekoa amy valobohò’ i Mitsraimey le afe­tsaho ambane, mb’an-tsikeo­keoke mb’eo, ie naho o anak’ampela’ o fifeheañe maozatseo, hitraofa’e amo migodañe an-koboñeo.
19 Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa!
Ia ty andikoara’o ami’ty hamontramontra’o? Mizotsoa irehe, hampipololorañe amo tsy nisavareñeo.
20 Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote.
Hikorovok’ añivo’ o zinamam-pibarao iereo; natolotse amy meso-lavay; endeso mb’etoy re naho ze hene ondati’ e.
21 Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’ (Sheol h7585)
Hisaontsy ama’e naho amo mpañolots’ azeo ty maozatse amo fanalolahy boak’ an-Tsikeokeokeo ami’ty hoe: fa nigodañe ao iereo, mitsalalampatse amo tsy nisavareñeo, vinonom-pibara. (Sheol h7585)
22 “Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga.
Ao ty Asore naho o mpirai-lia’e iabio; miarikoboñe aze o kibori’eo; kila zamañe, tsiningorom-pibara;
23 Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.
an-tsikeokeo’ i koboñey o kibori’ iareoo. Mandre mañohoke o kibori’eo o mpirai-lia’eo. Fonga mifitak’ ao o lahin-defo’eo. Fa zinamañ’an-kotakotak’ ao, ie nañembañ’ ondaty an-tane o veloñeo.
24 “Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. (questioned)
Ao t’i Elame rekets’ o fonga lahin-defo’eo miarikoboñe i kibori’ey. Songa vinono, nampikorovohem-pibara, nigodañe ambane tane ao o tsy nisavareñeo. Nampirevendreveñe’ iereo ondaty an-tanen-kaveloñeo, f’ie mitrao-kasalarañe amo nigodañe an-koboñeo henaneo.
25 Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.
Nandranjiam-pandreañe t’i Elame añivo’ o navetrakeo rekets’ i valobohò’ey. Fonga mañohok’ aze eo o kibori’eo, songa tsy nisavareñe, linihim-pibara ty amy fangebahebaha’ iareo ondaty an-tanen-kaveloñey. Aa le vavè’ iareo ty hameñarañe mindre amo mizotso an-koboñeo, ie napok’ an-teñateña’ o nikoromakeo.
26 “Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai.
Ao t’i Meseke Tobale vaho o valo­bohò’eo; sindre arikatohe’ o ki­bori’eo, songa tsy nisavareñe, zinamam-pibara ie nampivorombelo’ ondaty an-tanen-kaveloñe ao.
27 Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
Toe tsy hitrao-pandreañ’ amo fanalolahy nitsingoritritse amo tsy nisavareñeoo iereo, o nigodañe an-Tsikeokeok’ ao rekets’ o fialia’ eoo naho miondam-pibara ambane’ o añambone’eo, ie amo taola’eo o hakeo’eo ami’ty nampitsololoha’ iareo ondaty an-tane o veloñeo. (Sheol h7585)
28 “Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.
Hete! ho folaheñe an-teñateña’ o tsy nisavareñeo irehe vaho hipololotse amo zinamam-pibarao.
29 “Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.
Ao t’i Edome, naho o mpan­jaka’eo, vaho o roandria’eo; songa mandre amo binaibaim-pibarao rekets’ o haozara’eo; hitrao-pitsa­lalampatse amo tsy nisavareñeo, o fa nigodañe an-koboñeo.
30 “Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.
Ao ka o roandria’ tavaratseo, ie iaby, naho ze hene nte-Tsidone, ze fa nigodañe mañambane añe mitraok’ amo zinamañeo naho ami’ty fangebaheba’ iareo, salatse iereo amo haozara’eo; mandre ami’ty tsy fisavara’ iereo ao rekets’ o zinamam-pibarao, mivave o fisalara’eo mindre amo migodañe mb’an-koboñeo.
31 “Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.
Hahaisake iareo t’i Parò ie hampitsiñeñe amy valobohò’ey; eka, i Parò naho o fonga lia-rai’eo songa binaibaim-pibara, hoe t’Iehovà Talè.
32 Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”
Amy te nitsitsifeko an-tanen-kaveloñe ao ty fangetraketraha’e, le handre añivo’ o tsy nisavareñeo amo zinevom-pibarao t’i Parò naho i valobohò’ey, hoe t’Iehovà Talè.

< Ezekieli 32 >