< Ezekieli 9 >

1 Kisha nikamsikia akiita kwa sauti kubwa akisema, “Walete wasimamizi wa mji hapa, kila mmoja akiwa na silaha mkononi mwake.”
Then he called in mine ears with a loud voice, saying: 'Cause ye them that have charge over the city to draw near, every man with his destroying weapon in his hand.'
2 Nami nikaona watu sita wakija toka upande wa lango la juu, linalotazama kaskazini kila mmoja na silaha za kuangamiza mkononi mwake. Pamoja nao alikuwepo mtu aliyekuwa amevaa mavazi ya kitani safi, naye alikuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande mmoja. Wakaingia ndani ya Hekalu wakasimama pembeni mwa madhabahu ya shaba.
And, behold, six men came from the way of the upper gate, which lieth toward the north, every man with his weapon of destruction in his hand; and one man in the midst of them clothed in linen, with a writer's inkhorn on his side. And they went in, and stood beside the brazen altar.
3 Basi utukufu wa Mungu wa Israeli ukaondoka hapo juu ya makerubi, ulikokuwa umekaa, ukaenda kwenye kizingiti cha Hekalu. Ndipo Bwana akamwita yule mtu aliyevaa kitani safi aliyekuwa na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja,
And the glory of the God of Israel was gone up from the cherub, whereupon it was, to the threshold of the house; and He called to the man clothed in linen, who had the writer's inkhorn on his side.
4 akamwambia, “Pita katika mji wote wa Yerusalemu ukaweke alama juu ya vipaji vya nyuso za wale watu wanaohuzunika na kuomboleza kwa sababu ya machukizo yote yanayotendeka katika mji huu.”
And the LORD said unto him: 'Go through the midst of the city, through the midst of Jerusalem, and set a mark upon the foreheads of the men that sigh and that cry for all the abominations that are done in the midst thereof.'
5 Nikiwa ninasikia, akawaambia wale wengine, “Mfuateni anapopita katika mji wote mkiua, pasipo huruma wala masikitiko.
And to the others He said in my hearing: 'Go ye through the city after him, and smite; let not your eye spare, neither have ye pity;
6 Waueni wazee, vijana wa kiume na wa kike, wanawake na watoto, lakini msimguse mtu yeyote mwenye alama. Anzieni katika mahali pangu patakatifu.” Kwa hiyo wakaanza na wale wazee waliokuwa mbele ya Hekalu.
slay utterly the old man, the young man and the maiden, and little children and women; but come not near any man upon whom is the mark; and begin at My sanctuary.' Then they began at the elders that were before the house.
7 Ndipo akawaambia, “Linajisini Hekalu na mkazijaze kumbi zake maiti za wale waliouawa. Nendeni!” Kwa hiyo wakaenda wakaanza kuua watu mjini kote.
And He said unto them: 'Defile the house, and fill the courts with the slain; go ye forth.' And they went forth, and smote in the city.
8 Wakati walikuwa wakiwaua watu, nami nilikuwa nimeachwa peke yangu, nikaanguka kifudifudi, nikapiga kelele nikisema, “Ee Bwana Mwenyezi! Je, utaangamiza mabaki yote ya Israeli, katika kumwagwa huku kwa ghadhabu yako juu ya Yerusalemu?”
And it came to pass, while they were smiting, and I was left, that I fell upon my face, and cried, and said: 'Ah Lord GOD! wilt Thou destroy all the residue of Israel in Thy pouring out of Thy fury upon Jerusalem?'
9 Bwana akanijibu, “Dhambi ya nyumba ya Israeli na Yuda imekuwa kubwa mno kupita kiasi, nchi imejaa umwagaji damu na mjini kumejaa udhalimu. Kwani wamesema, ‘Bwana ameiacha nchi, Bwana hauoni.’
Then said He unto me: 'The iniquity of the house of Israel and Judah is exceeding great, and the land is full of blood, and the city full of wresting of judgment; for they say: The LORD hath forsaken the land, and the LORD seeth not.
10 Kwa hiyo sitawahurumia wala kuwaachilia lakini nitaleta juu ya vichwa vyao, yale waliyoyatenda.”
And as for Me also, Mine eye shall not spare, neither will I have pity, but I will bring their way upon their head.'
11 Ndipo mtu yule aliyekuwa amevaa nguo ya kitani safi na vifaa vya mwandishi akiwa amevishikilia upande wake mmoja, akarudi na kutoa taarifa akisema, “Nimefanya kama ulivyoniagiza.”
And, behold, the man clothed in linen, who had the inkhorn on his side, reported, saying: 'I have done according to all that Thou hast commanded me.'

< Ezekieli 9 >