< Wagalatia 1 >

1 Paulo mtume: si mtume wa wanadamu wala aliyetumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo na Mungu Baba aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu;
Paul, an apostle, —not from men, nor through man, but through Jesus Christ, and God the Father who raised him from among the dead,
2 na ndugu wote walio pamoja nami: Kwa makanisa ya Galatia:
And all the brethren with me; —unto the assemblies of Galatia:
3 Neema iwe nanyi na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo,
Favour unto you and peace, from God our Father, and Lord Jesus Christ, —
4 aliyejitoa kwa ajili ya dhambi zetu ili apate kutuokoa katika ulimwengu huu wa sasa ulio mbaya, sawasawa na mapenzi yake yeye aliye Mungu na Baba yetu. (aiōn g165)
Who gave himself for our sins, that he might deliver us out of the present evil age, according to the will of our God and Father, — (aiōn g165)
5 Utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
Unto whom be the glory unto the ages of ages: Amen! (aiōn g165)
6 Nashangaa kwamba mnamwacha upesi hivyo yeye aliyewaita kwa neema ya Kristo na kuifuata Injili nyingine,
I marvel that, thus quickly, ye are moving away from him that called you in the favour of Christ, unto a different glad-message, —
7 ambayo kwa kweli si Injili kamwe, ila kwa dhahiri kuna watu wanaowachanganya na wanaotaka kuipotosha Injili ya Kristo.
Which is not, another, only there are, some, that are troubling you, and wishing to change the glad-message of the Christ.
8 Lakini hata ikiwa sisi au malaika atokaye mbinguni akihubiri Injili nyingine tofauti na ile tuliyowahubiria sisi, basi mtu huyo alaaniwe milele!
But, even if, we, or, a messenger out of heaven, announce a glad-message [unto you] aside from that which we announced unto you, accursed, let him be!
9 Kama vile tulivyokwisha kusema kabla, sasa nasema tena, ikiwa mtu yeyote atawahubiria Injili kinyume na ile mliyoipokea na alaaniwe milele!
As we have said before, even now, again, I say: If anyone is announcing unto you a glad-message aside from that which ye accepted, accursed, let him be!
10 Je, sasa mimi ninatafuta kukubaliwa na wanadamu au kukubaliwa na Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa bado najaribu kuwapendeza wanadamu, nisingekuwa mtumishi wa Kristo.
For am I, even now, persuading, men, or God? Or am I seeking to please, men? If I had been still pleasing, men, Christ’s servant, had I not been!
11 Ndugu zangu, nataka mjue kwamba Injili niliyowahubiria haikutokana na wanadamu.
For I make known unto you, brethren, as to the glad-message which was announced by me, that it is not after man;
12 Kwa maana mimi sikuipokea hiyo Injili kutoka kwa mwanadamu, wala sikufundishwa na mtu, bali niliipata kwa ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo.
For neither, from man, did I accept it, nor was taught [it], —but through a revealing of Jesus Christ.
13 Ninyi mmekwisha kusikia juu ya maisha yangu ya zamani nilipokuwa katika dini ya Kiyahudi, jinsi nilivyolitesa kanisa la Mungu kwa nguvu na kujaribu kuliangamiza.
For ye have heard, as to my own manner of life, at one time, in Judaism, how that, exceedingly, was I persecuting the assembly of God, and laying it waste,
14 Nami niliendelea sana katika dini ya Kiyahudi kuliko Wayahudi wengi wa rika yangu maana nilijitahidi sana katika desturi za baba zangu.
And was making advancement, in Judaism, above many contemporaries in my nation, being, surpassingly zealous, of my paternal instructions.
15 Lakini ilipompendeza Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu na kuniita kwa neema yake,
But, when God, who set me apart from my mother’s womb and called me through his favour, was well-pleased
16 alimdhihirisha Mwanawe kwangu, ili nipate kumhubiri miongoni mwa watu wa Mataifa. Mimi sikushauriana na mwanadamu yeyote,
to reveal his Son in me, that I might announce the glad-message regarding him among the nations, straightway, I conferred not with flesh and blood,
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kuwaona hao waliokuwa mitume kabla yangu, bali nilikwenda mara moja Arabuni na kisha nikarudi Dameski.
Neither went I up unto Jerusalem unto them who, before me, were apostles, —but I went away into Arabia, and again returned unto Damascus.
18 Kisha baada ya miaka mitatu nilipanda kwenda Yerusalemu kuonana na Kefa na nilikaa naye siku kumi na tano.
Then, after three years, went I up unto Jerusalem, to become acquainted with Cephas, and tarried with him fifteen days;
19 Lakini sikumwona mtume mwingine yeyote isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana.
But, other of the apostles, saw I none, save James the brother of the Lord: —
20 Nawahakikishia mbele za Mungu kuwa ninayowaandikia si uongo.
Now, as touching the things which I am writing to you, lo! before God, I am not guilty of falsehood: —
21 Baadaye nilikwenda sehemu za Syria na Kilikia.
After that, I went into the regions of Syria and Cilicia,
22 Lakini mimi binafsi sikujulikana kwa makanisa ya huko Uyahudi yaliyo katika Kristo.
And was still unknown, by face, unto the assemblies of Judaea which were in Christ, —
23 Wao walisikia habari tu kwamba, “Mtu yule ambaye hapo kwanza alikuwa akitutesa sasa anahubiri imani ile ile aliyokuwa akijaribu kuiangamiza.”
Only they were hearing—He that was persecuting us formerly, now, is announcing the glad-message of the faith which he formerly laid waste;
24 Nao wakamtukuza Mungu kwa sababu yangu.
And they were glorifying, God, in me.

< Wagalatia 1 >