< Mwanzo 39 >

1 Wakati huu Yosefu alikuwa amechukuliwa mpaka Misri. Mmisri aliyeitwa Potifa aliyekuwa mmojawapo wa maafisa wa Farao, mkuu wa ulinzi, akamnunua Yosefu kutoka kwa Waishmaeli waliomleta Misri.
Joseph was brought down to Egypt. Potiphar, an official of Pharaoh who was captain of the guard and an Egyptian, bought him from the Ishmaelites, who had brought him down there.
2 Bwana alikuwa pamoja na Yosefu, naye akastawi, Yosefu akaishi nyumbani kwa bwana wake Mmisri.
Yahweh was with Joseph and he became a prosperous man. He lived in the house of his Egyptian master.
3 Potifa alipoona kuwa Bwana alikuwa pamoja na Yosefu na kwamba Bwana alimfanikisha kwa kila kitu alichokifanya,
His master saw that Yahweh was with him and that Yahweh prospered everything that he did.
4 Yosefu alipata kibali machoni pa Potifa, akamfanya mhudumu wake. Potifa akamweka kuwa msimamizi wa nyumba yake, naye akamkabidhi kuwa mwangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho.
Joseph found favor in his sight. He served Potiphar. Potiphar made Joseph manager over his house, and everything that he possessed, he put under his care.
5 Kuanzia wakati huo Potifa alipomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nyumba na mali zake zote alizokuwa nazo, Bwana aliibariki nyumba ya Mmisri huyo kwa sababu ya Yosefu. Baraka ya Bwana ilikuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho Potifa, nyumbani na shambani.
It came about from the time that he made him manager over his house and over everything he possessed, that Yahweh blessed the Egyptian's house because of Joseph. The blessing of Yahweh was on everything that Potiphar had in the house and in the field.
6 Kwa hiyo Potifa akamwachia Yosefu uangalizi wa kila kitu alichokuwa nacho, Yosefu alipokuwa katika uongozi, Potifa hakuwa na sababu ya kujishughulisha na kitu chochote isipokuwa chakula alichokula. Yosefu alikuwa mwenye umbo zuri na sura ya kuvutia;
Potiphar put everything that he had under Joseph's care. He did not have to think about anything except the food that he ate. Now Joseph was handsome and attractive.
7 baada ya kitambo mke wa Potifa akamtamani Yosefu, akamwambia, “Njoo, ukutane nami kimwili!”
It came about after this that his master's wife lusted for Joseph. She said, “Sleep with me.”
8 Lakini Yosefu akakataa. Akamwambia yule mwanamke, “Mimi nikiwa katika uongozi, bwana wangu hahusiki na kitu chochote katika nyumba hii, kila kitu alicho nacho amenikabidhi.
But he refused and said to his master's wife, “Look, my master does not pay attention to what I do in the house, and he has put everything that he owns under my care.
9 Hapa nyumbani hakuna aliye mkuu kuliko mimi. Bwana wangu hakunizuilia kitu chochote isipokuwa wewe, kwa kuwa wewe ni mke wake. Nitawezaje basi kufanya uovu huu na kutenda dhambi dhidi ya Mungu?”
No one is greater in this house than I am. He has not kept back anything from me but you, because you are his wife. How then can I do this great wickedness and sin against God?”
10 Ingawa yule mwanamke aliendelea kumshawishi Yosefu siku baada ya siku, Yosefu alikataa kukutana naye kimwili wala kukaa karibu naye.
She spoke to Joseph day after day, but he refused to sleep with her or to be with her.
11 Siku moja Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi zake, wala hapakuwepo na mfanyakazi yeyote ndani ya nyumba.
It came about one day that he went into the house to do his work. None of the men of the house were there in the house.
12 Mke wa Potifa akashika vazi Yosefu alilokuwa amevaa, akamwambia, “Njoo tukutane kimwili!” Lakini Yosefu akaacha vazi lake mkononi mwa huyo mwanamke, akatoka nje ya nyumba akikimbia.
She caught him by his clothes and said, “Sleep with me.” He left his clothing in her hand, fled, and went outside.
13 Yule mwanamke alipoona kwamba Yosefu amemwachia vazi lake mkononi na kukimbilia nje ya nyumba,
It came about, when she saw that he had left his clothing in her hand and had fled outside,
14 akawaita watumishi wake wa nyumbani, akawaambia, “Tazameni! Huyu Mwebrania ameletwa hapa kutudhihaki! Aliingia hapa ndani ili akutane nami kimwili, lakini nikapiga kelele.
that she called to the men of her house and told them, “See, Potiphar has brought in a Hebrew to mock us. He came in to me to sleep with me, and I screamed.
15 Aliposikia kelele za kuomba msaada, akaacha vazi lake kando yangu akakimbilia nje.”
It came about when he heard me scream, that he left his clothing with me, fled, and went outside.”
16 Yule mwanamke akaliweka lile vazi karibu naye mpaka Potifa aliporudi nyumbani.
She set his clothing next to her until his master came home.
17 Ndipo akamweleza kisa hiki, akisema: “Yule mtumwa wa Kiebrania uliyetuletea alinijia ili kunidhihaki.
She told him this explanation, “The Hebrew servant whom you brought to us, came in to mock me.
18 Lakini mara nilipopiga kelele kuomba msaada, akaliacha vazi lake kando yangu akakimbia nje ya nyumba.”
It came about that when I screamed, he left his clothing with me and fled outside.”
19 Potifa aliposikia kisa hiki mkewe alichomweleza, akisema, “Hivi ndivyo mtumwa wako alivyonitenda.” Hasira ya Potifa ikawaka.
It came about that, when his master heard the explanation his wife told him, “This is what your servant did to me,” he became very angry.
20 Potifa akamchukua Yosefu na kumweka gerezani, mahali ambapo wahalifu wa mfalme walikuwa wamefungwa. Lakini wakati Yosefu alipokuwa huko gerezani,
Joseph's master took him and put him in prison, the place where the king's prisoners were confined. He was there in the prison.
21 Bwana alikuwa pamoja naye, akamhurumia na kumpa kibali mbele ya msimamizi wa gereza.
But Yahweh was with Joseph and showed covenant faithfulness to him. He gave him favor in the sight of the prison warden.
22 Kwa hiyo msimamizi wa gereza akamweka Yosefu awe mkuu wa wafungwa pamoja na kusimamia yote ambayo yalitendeka mle gerezani.
The prison warden gave into Joseph's hand all the prisoners who were in the prison. Whatever they did there, Joseph was in charge of it.
23 Msimamizi wa gereza hakujishughulisha tena na kitu chochote kilichokuwa chini ya uangalizi wa Yosefu, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja na Yosefu akimfanikisha kwa kila alichofanya.
The prison warden did not worry about anything that was in his hand, because Yahweh was with him. Whatever he did, Yahweh prospered.

< Mwanzo 39 >