< Mwanzo 4 >

1 Adamu akakutana kimwili na mkewe Eva, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Eva akasema, “Kwa msaada wa Bwana nimemzaa mwanaume.”
The man knew Eve [Life] his wife. She conceived, and gave birth to Cain [Acquisition], and said, “I have gotten a man with Adonai’s help.”
2 Baadaye akamzaa Abeli ndugu yake. Basi Abeli akawa mfugaji, na Kaini akawa mkulima.
Again she gave birth, to Cain [Acquisition]’s brother Abel [Vanity, Mourning]. Abel [Vanity, Mourning] was a keeper of sheep, but Cain [Acquisition] was a tiller of the ground.
3 Baada ya muda Kaini akaleta baadhi ya mazao ya shamba kama sadaka kwa Bwana.
As time passed, Cain [Acquisition] brought an offering to Adonai from the fruit of the ground.
4 Lakini Abeli akaleta fungu nono kutoka baadhi ya wazaliwa wa kwanza wa mifugo yake. Bwana akamkubali Abeli pamoja na sadaka yake,
Abel [Vanity, Mourning] also brought some of the firstborn of his flock and of its fat. Adonai respected Abel [Vanity, Mourning] and his offering,
5 lakini Mungu hakumkubali Kaini pamoja na sadaka yake. Kwa hiyo Kaini akakasirika sana, uso wake ukawa na huzuni.
but he didn’t respect Cain [Acquisition] and his offering. Cain [Acquisition] was very angry, and the expression on his face fell.
6 Kisha Bwana akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika? Kwa nini uso wako una huzuni?
Adonai said to Cain [Acquisition], “Why are you angry? Why has the expression of your face fallen?
7 Ukifanya lililo sawa, je, hutakubalika? Lakini usipofanya lililo sawa, dhambi inakuvizia mlangoni mwako, inakutamani wewe, lakini inakupasa uishinde.”
If you do well, won’t it be lifted up? If you don’t do well, sin crouches at the door. Its desire is for you, but you are to rule over it.”
8 Basi Kaini akamwambia ndugu yake Abeli, “Twende shambani.” Walipokuwa shambani, Kaini akamshambulia Abeli ndugu yake, akamuua.
Cain [Acquisition] said to Abel [Vanity, Mourning], his brother, “Let’s go into the field.” While they were in the field, Cain [Acquisition] rose up against Abel [Vanity, Mourning], his brother, and murdered him.
9 Kisha Bwana akamuuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Akamjibu, “Sijui, je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?”
Adonai said to Cain [Acquisition], “Where is Abel [Vanity, Mourning], your brother?” He said, “I don’t know. Am I my brother’s keeper?”
10 Bwana akasema, “Umefanya nini? Sikiliza! Damu ya ndugu yako inanililia mimi kutoka ardhini.
Adonai said, “What have you done? The voice of your brother’s blood cries to me from the ground.
11 Sasa umelaaniwa na umehamishwa kutoka ardhi, ambayo imefungua kinywa chake na kupokea damu ya ndugu yako kutoka mkononi mwako.
Now you are cursed because of the ground, which has opened its mouth to receive your brother’s blood from your hand.
12 Utakapoilima ardhi, haitakupa tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga duniani asiye na utulivu.”
From now on, when you till the ground, it won’t yield its strength to you. You will be a fugitive and a wanderer in the earth.”
13 Kaini akamwambia Bwana, “Adhabu yangu ni zaidi ya niwezavyo kustahimili.
Cain [Acquisition] said to Adonai, “My punishment is greater than I can bear.
14 Leo unanifukuza kutoka nchi, nami nitafichwa mbali na uwepo wako. Nitakuwa mtu wa kutangatanga asiyetulia duniani na yeyote anionaye ataniua.”
Behold, you have divorced and driven me out today from the surface of the ground. I will be hidden from your face, and I will be a fugitive and a wanderer in the earth. Whoever finds me will kill me.”
15 Lakini Bwana akamwambia, “La sivyo, ikiwa mtu yeyote atamuua Kaini atalipizwa kisasi mara saba zaidi.” Kisha Bwana akamwekea Kaini alama ili mtu yeyote ambaye angemwona asimuue.
Adonai said to him, “Therefore whoever slays Cain [Acquisition], vengeance will be taken on him sevenfold.” Adonai appointed a sign for Cain [Acquisition], so that anyone finding him would not strike him.
16 Kwa hiyo Kaini akaondoka mbele za Bwana akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, iliyoko mashariki ya Edeni.
Cain [Acquisition] left Adonai’s presence, and lived in the land of Nod, east of Eden [Delight].
17 Kaini akakutana kimwili na mkewe, naye akapata mimba na akamzaa Enoki. Wakati huo Kaini alikuwa anajenga mji, akauita Enoki jina la mtoto wake.
Cain [Acquisition] knew his wife. She conceived, and gave birth to Enoch. He built a city, and called the name of the city, after the name of his son, Enoch.
18 Enoki akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli, Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, na Methushaeli akamzaa Lameki.
To Enoch was born Irad. Irad became the father of Mehujael. Mehujael became the father of Methushael. Methushael became the father of Lamech.
19 Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada, na mwingine Sila.
Lamech took two wives: the name of the first one was Adah, and the name of the second one was Zillah.
20 Ada akamzaa Yabali ambaye ni baba wa wale walioishi katika mahema na kufuga wanyama.
Adah gave birth to Jabal, who was the father of those who dwell in tents and have livestock.
21 Kaka yake aliitwa Yubali, aliyekuwa baba wa wote wapigao zeze na filimbi.
His brother’s name was Jubal, who was the father of all who handle the harp and pipe.
22 Pia Sila alikuwa na mtoto wa kiume aliyeitwa Tubali-Kaini ambaye alifua vifaa vya aina mbalimbali vya shaba na chuma. Naama alikuwa dada wa Tubali-Kaini.
Zillah also gave birth to Tubal Cain [Acquisition], the forger of every cutting instrument of bronze and iron. Tubal Cain [Acquisition]’s sister was Naamah.
23 Lameki akawaambia wake zake, “Ada na Sila nisikilizeni mimi; wake wa Lameki sikieni maneno yangu. Nimemuua mtu kwa kunijeruhi, kijana mdogo kwa kuniumiza.
Lamech said to his wives, “Adah and Zillah, sh'ma ·hear obey· my voice. You wives of Lamech, listen to my speech, for I have slain a man for wounding me, a young man for bruising me.
24 Kama Kaini atalipizwa kisasi mara saba, basi Lameki itakuwa mara sabini na saba.”
If Cain [Acquisition] will be avenged seven times, truly Lamech seventy-seven times.”
25 Adamu akakutana kimwili na mke wake tena, akamzaa mwana, akamwita Sethi, akisema, “Mungu amenijalia mwana mwingine badala ya Abeli, kwa kuwa Kaini alimuua.”
Adam [Human, Red earth] knew his wife again. She gave birth to a son, and named him Seth [Appointed], saying, “for God has given me another child instead of Abel [Vanity, Mourning], for Cain [Acquisition] killed him.”
26 Naye Sethi akamzaa mwana, akamwita Enoshi. Wakati huo watu wakaanza kuliitia jina la Bwana.
A son was also born to Seth [Appointed], and he named him Enosh. At that time men began to call on Adonai’s name.

< Mwanzo 4 >