< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu.
This is the book of generacioun of Adam, in the dai wher ynne God made man of nouyt. God made man to the ymage and licnesse of God;
2 Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.”
God formede hem male and female, and blesside hem, and clepide the name of hem Adam, in the day in which thei weren formed.
3 Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi.
Forsothe Adam lyuede an hundrid yeer and thretti, and gendride a sone to his ymage and liknesse, and clepide his name Seth.
4 Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And the daies of Adam after that he gendride Seth weren maad eiyte hundrid yeer, and he gendride sones and douytris.
5 Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa.
And al the tyme in which Adam lyuede was maad nyne hundrid yeer and thretti, and he was deed.
6 Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
Also Seth lyuede an hundrid and fyue yeer, and gendride Enos.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Seth lyuede aftir that he gendride Enos eiyte hundrid and seuen yeer, and gendride sones and douytris.
8 Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa.
And alle the daies of Seth weren maad nyne hundrid and twelue yeer, and he was deed.
9 Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Forsothe Enos lyuede nynti yeer, and gendride Caynan;
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
aftir whos birthe Enos lyuede eiyte hundrid and fiftene yeer, and gendride sones and douytris.
11 Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa.
And alle the daies of Enos weren maad nyne hundrid and fyue yeer, and he was deed.
12 Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
Also Caynan lyuyde seuenti yeer, and gendride Malalehel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Caynan lyuede after that he gendride Malalehel eiyte hundrid and fourti yeer, and gendride sones and douytris.
14 Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa.
And alle the dayes of Caynan weren maad nyn hundrid and ten yeer, and he was deed.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Forsothe Malalehel lyuede sixti yeer and fyue, and gendride Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Malalehel lyuede aftir that he gendride Jared eiyte hundrid and thretti yeer, and gendride sones and douytris.
17 Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa.
And alle the daies of Malalehel weren maad eiyte hundrid nynti and fyue yeer, and he was deed.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki.
And Jared lyuede an hundrid and two and sixti yeer, and gendride Enoth.
19 Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Jared lyuede aftir that he gendride Enoth eiyte hundrid yeer, and gendride sones and douytris.
20 Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa.
And alle the dayes of Jared weren maad nyn hundrid and twei and sexti yeer, and he was deed.
21 Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.
Forsothe Enoth lyuede fyue and sixti yeer, and gendride Matusalem.
22 Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Enoth yede with God; and Enoth lyuede after that he gendride Matusalem thre hundrid yeer, and gendride sones and douytris.
23 Enoki aliishi jumla ya miaka 365.
And alle the daies of Enoth weren maad thre hundride and fyue and sexti yeer.
24 Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua.
And Enoth yeed with God, and apperide not afterward, for God took hym awei.
25 Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki.
Also Matusalem lyuede an hundrid and `fourscoor yeer and seuene, and gendride Lameth.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Matusalem lyuede after that he gendride Lameth seuene hundrid and `fourscoor yeer and twei, and gendride sones and douytris.
27 Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa.
And alle the daies of Matusale weren maad nyn hundrid and nyn and sixti yeer, and he was deed.
28 Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
Forsothe Lameth lyuede an hundrid and `fourscoor yeer and two, and gendride a sone;
29 Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na Bwana.”
and clepide his name Noe, and seide, This man schal comforte vs of the werkis and traueilis of oure hondis, in the loond which the Lord curside.
30 Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike.
And Lameth lyuede after that he gendride Noe fyue hundrid `nynti and fyue yeer, and gendride sones and douytris.
31 Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa.
And alle the daies of Lameth weren maad seuene hundrid `thre scoor and seuentene yeer, and he was deed.
32 Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
Forsothe Noe whanne he was of fyue hundrid yeer gendride Sem, Cham, and Jafeth.

< Mwanzo 5 >