< Isaya 28 >

1 Ole kwa lile taji la maua, kiburi cha walevi wa Efraimu, kwa ua linalosinyaa, uzuri wa utukufu wake, uliowekwa kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba: kwa ule mji, kiburi cha wale walioshushwa na mvinyo!
Biada koronie pychy, pijakom Efraima, których wspaniała ozdoba jest więdnącym kwiatem rosnącym na szczycie urodzajnych dolin odurzonych winem!
2 Tazama, Bwana anaye mmoja aliye na uwezo na nguvu. Kama dhoruba ya mvua ya mawe na upepo uharibuo, kama mvua inyeshayo kwa nguvu na mafuriko yashukayo, atakiangusha chini kwa nguvu.
Oto ktoś od Pana, mocny i silny, jak burza gradowa, jak niszcząca nawałnica, jak ulewa gwałtownych rwących wód, rzuci [ją] na ziemię swoją ręką.
3 Lile taji la maua, kiburi cha walevi cha Efraimu, kitakanyagwa chini ya nyayo.
Zostanie zdeptana nogami korona pychy, pijacy Efraima.
4 Lile ua linalosinyaa, uzuri wa utukufu wake, uliowekwa kwenye kichwa cha bonde lenye rutuba, litakuwa kama tini iliyoiva kabla ya mavuno: mara mtu aionapo, huichuma na kuila.
A wspaniała ozdoba, która jest na szczycie urodzajnej doliny, będzie więdnącym kwiatem jak przed latem wczesny owoc; kto go tylko zobaczy, weźmie do ręki i zje.
5 Katika siku ile, Bwana Mwenye Nguvu Zote atakuwa taji la utukufu, taji zuri la maua kwa mabaki ya watu wake.
W tym dniu PAN zastępów będzie koroną chwały i diademem ozdoby dla resztki swojego ludu;
6 Atakuwa roho ya haki kwa yeye aketiye katika kiti cha hukumu, chanzo cha nguvu kwa wale wazuiao vita langoni.
Duchem sądu dla zasiadającego w sądzie i mocą dla tych, którzy odpierają atak aż do bramy.
7 Hawa pia wanapepesuka kwa sababu ya mvinyo, wanayumbayumba kwa sababu ya kileo: Makuhani na manabii wanapepesuka kwa sababu ya kileo, wanachanganyikiwa kwa sababu ya mvinyo; wanapepesuka wanapoona maono, wanajikwaa wanapotoa maamuzi.
Ale również ci od wina błądzą i od mocnego napoju zataczają się. Kapłan i prorok błądzą od mocnego napoju, utonęli w winie, zataczają się od mocnego napoju, błądzą w widzeniach, potykają się w sądzie.
8 Meza zote zimejawa na matapishi wala hakuna sehemu hata ndogo isiyokuwa na uchafu.
Wszystkie ich stoły bowiem są pełne wymiotów i plugastwa, tak że nie ma [czystego] miejsca.
9 “Yeye anajaribu kumfundisha nani? Yeye anamwelezea nani ujumbe wake? Je, ni kwa watoto walioachishwa kunyonya? Je, ni wale ambao ndipo tu wametolewa matitini?
Kogo ma uczyć poznania? Komu ma wyjaśnić naukę? Czyż odstawionym od mleka i odłożonym od piersi?
10 Kwa maana ni: Amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni; hapa kidogo, kule kidogo.”
Ponieważ podaje się przykazanie za przykazaniem, przykazanie za przykazaniem, przepis za przepisem, przepis za przepisem, trochę tu, trochę tam.
11 Sawa kabisa, kwa midomo migeni na kwa lugha ngeni, Mungu atasema na watu hawa,
Bo wargami jąkających się i obcym językiem będę mówił do tego ludu.
12 wale ambao aliwaambia, “Hapa ni mahali pa kupumzika, waliochoka na wapumzike,” na, “Hapa ni mahali pa mapumziko,” lakini hawakutaka kusikiliza.
A gdy im powiedział: To jest odpoczynek, dajcie odpocząć spracowanemu; to jest wytchnienie. Ale oni nie chcieli słuchać.
13 Hivyo basi, neno la Bwana kwao litakuwa: Amri juu ya amri, amri juu ya amri, kanuni juu ya kanuni, kanuni juu ya kanuni, hapa kidogo, kule kidogo: ili waende na kuanguka chali, wakijeruhiwa, wakinaswa na kukamatwa.
I słowo PANA będzie im: przykazanie za przykazaniem, przykazanie za przykazaniem, przepis za przepisem, przepis za przepisem, trochę tu, trochę tam, po to, aby szli, padli na wznak i rozbili się, aby zostali uwikłani i pojmani.
14 Kwa hiyo sikieni neno la Bwana, enyi watu wenye dharau mnaotawala watu hawa wa Yerusalemu.
Dlatego słuchajcie słowa PANA, wy, mężowie szyderczy, panujący nad tym ludem, który jest w Jerozolimie.
15 Ninyi mnajisifu, “Tumefanya agano na mauti, tumefanya mapatano na kuzimu. Wakati pigo lifurikalo litakapopita, haliwezi kutugusa sisi, kwa kuwa tumefanya uongo kuwa kimbilio letu na miungu ya uongo kuwa mahali petu pa kujificha.” (Sheol h7585)
Ponieważ mówicie: Zawarliśmy przymierze ze śmiercią i z piekłem mamy układ; gdy przejdzie bicz gwałtowny, nie dosięgnie nas, gdyż kłamstwo uczyniliśmy naszą ucieczką i skryliśmy się za fałszem; (Sheol h7585)
16 Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo: “Tazama, ninaweka jiwe katika Sayuni, jiwe lililojaribiwa, jiwe la pembeni la thamani kwa ajili ya msingi thabiti. Yeye atumainiye kamwe hatatiwa hofu.
Dlatego tak powiedział Pan BÓG: Oto kładę jako grunt na Syjonie kamień, kamień wypróbowany, węgielny, drogocenny, utwierdzony fundament. Kto uwierzy, nie pospieszy się.
17 Nitaifanya haki kuwa kamba ya kupimia na uadilifu kuwa timazi; mvua ya mawe itafagia kimbilio lenu, huo uongo, nayo maji yatafurikia mahali penu pa kujificha.
A wykonam sąd według sznura, a sprawiedliwość według pionu. I grad zmiecie schronienie kłamstw, a wody zaleją kryjówkę.
18 Agano lenu na kifo litabatilishwa, patano lenu na kuzimu halitasimama. Wakati pigo lifurikalo litakapowakumba, litawaangusha chini. (Sheol h7585)
Wasze przymierze ze śmiercią zostanie zerwane, a wasz układ z piekłem nie ostoi się; gdy ten bicz gwałtowny przejdzie, zostaniecie przez niego zdeptani. (Sheol h7585)
19 Kila mara lijapo litawachukua, asubuhi baada ya asubuhi, wakati wa mchana na wakati wa usiku, litawakumba tangu mwanzo hadi mwisho.” Kuuelewa ujumbe huu utaleta hofu tupu.
Jak tylko zacznie przechodzić, pochwyci was, bo każdego poranka będzie przechodzić, dniem i nocą. Sam tylko postrach zaprowadzi was do zrozumienia tego, co słyszeliście;
20 Kitanda ni kifupi mno kujinyoosha juu yake, nguo ya kujifunikia ni nyembamba mno mtu hawezi kujifunikia.
Bo łóżko będzie za krótkie, aby się na nim rozciągnąć, przykrycie zbyt wąskie, by się nim owinąć.
21 Bwana atainuka kama alivyofanya kwenye Mlima Perasimu, ataghadhibika kama alivyofanya katika Bonde la Gibeoni: ili kufanya kazi yake, kazi yake ya ajabu, ili kutimiza kazi yake, kazi yake ngeni.
PAN bowiem powstanie jak na górze Perazym i rozgniewa się jak w dolinie Gibeon, aby dokonać swego dzieła, swego niezwykłego dzieła, aby dokończyć swoje zadanie, swoje niezwykłe zadanie.
22 Sasa acheni dharau zenu, la sivyo minyororo yenu itakuwa mizito zaidi. Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, ameniambia habari za maangamizi yaliyoamriwa dhidi ya nchi yote.
Teraz więc nie naśmiewajcie się, aby wasze węzły nie zacisnęły się mocniej, gdyż słyszałem od Pana, BOGA zastępów, że postanowione jest zniszczenie na całej ziemi.
23 Sikilizeni msikie sauti yangu, tegeni masikio na msikie niyasemayo.
Nadstawcie uszu, posłuchajcie mego głosu; bądźcie uważni, słuchajcie mojej mowy.
24 Wakati mkulima alimapo ili apande, je, hulima siku zote? Je, huendelea kubomoa ardhi na kusawazisha udongo?
Czyż oracz codziennie orze, aby siać? [Czy] robi bruzdy i bronuje swoją rolę?
25 Akiisha kusawazisha shamba, je, hatapanyi mbegu za bizari na kutawanya jira? Je, hapandi ngano katika sehemu yake, shayiri katika eneo lake, na nafaka nyingine katika shamba lake?
Czyż gdy wyrówna jej powierzchnię, nie rozsiewa czarnuszki, nie rozsiewa kminu i nie obsiewa pszenicą wyborną, jęczmieniem przednim i orkiszem w odpowiednich miejscach?
26 Mungu wake humwelekeza na kumfundisha njia iliyo sahihi.
Jego Bóg uczy go roztropności i poucza go.
27 Iliki haipurwi kwa nyundo, wala gurudumu la gari halivingirishwi juu ya jira; iliki hupurwa kwa fimbo, na jira kwa ufito.
Czarnuszki bowiem nie młóci się saniami młockarskimi ani nie przetacza się koła wozu po kminku; ale kijem wybija się czarnuszkę, a kminek – laską.
28 Nafaka lazima isagwe ili kutengeneza mkate, kwa hiyo mtu haendelei kuipura daima. Ingawa huendesha magurudumu ya gari lake la kupuria juu yake, farasi wake hawasagi.
Pszenicę młóci się, ale nie bez końca, i nie pociera jej kołem wozu ani jej nie kruszy zaprzęgiem.
29 Haya yote pia hutoka kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote, mwenye mashauri ya ajabu, na anayepita wote kwa hekima.
I to także pochodzi od PANA zastępów, który jest cudowny w radzie i wielki w działaniu.

< Isaya 28 >