< Isaya 66 >

1 Hili ndilo asemalo Bwana, “Mbingu ni kiti changu cha enzi, nayo dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu. Iko wapi nyumba mtakayoijenga kwa ajili yangu? Mahali pangu pa kupumzikia patakuwa wapi?
Thus says the Lord: Heaven is my throne, and the earth is my footstool. What is this house that you would build for me? And what is this place of my rest?
2 Je, mkono wangu haukufanya vitu hivi vyote, hivyo vikapata kuwepo?” asema Bwana. “Mtu huyu ndiye ninayemthamini: yeye ambaye ni mnyenyekevu na mwenye roho yenye toba, atetemekaye asikiapo neno langu.
My hand has made all these things, and all these things have been made, says the Lord. But upon whom will I look with favor, except upon a poor little one, who is contrite in spirit, and who trembles at my words?
3 Lakini yeyote atoaye dhabihu ya fahali ni kama yeye auaye mtu, na yeyote atoaye sadaka ya mwana-kondoo, ni kama yule avunjaye shingo ya mbwa. Yeyote atoaye sadaka ya nafaka, ni kama yule aletaye damu ya nguruwe, na yeyote afukizaye uvumba wa kumbukumbu, ni kama yule aabuduye sanamu. Wamejichagulia njia zao wenyewe, nazo nafsi zao zinafurahia machukizo yao.
Whoever immolates an ox, it is as if he slaughters a man. Whoever sacrifices a sheep, it is as if he is smashing the head of a dog. Whoever offers an oblation, it is as if he is offering swine’s blood. Whoever makes remembrance with incense, it is as if he is blessing an idol. All these things, they have chosen according to their own ways, and their soul has taken delight in their own abominations.
4 Hivyo, mimi pia nitawachagulia mapigo makali, nami nitaleta juu yao kile wanachokiogopa. Kwa maana nilipoita, hakuna yeyote aliyejibu, niliposema, hakuna yeyote aliyesikiliza. Walifanya maovu machoni pangu na kuchagua lile linalonichukiza.”
Therefore, I also will choose their illusions, and I will lead over them the things that they feared. For I called, and there was no one who would respond. I have spoken, and they have not listened. And they have done evil in my eyes; and what I did not will, they have chosen.
5 Sikieni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa neno lake: “Ndugu zenu wanaowachukia ninyi na kuwatenga ninyi kwa sababu ya Jina langu, wamesema, ‘Bwana na atukuzwe, ili tupate kuona furaha yenu!’ Hata sasa wataaibika.
Listen to the word of the Lord, you who tremble at his word. Your brothers, who hate you and who cast you out because of my name, have said: “Let the Lord be glorified, and we will see by your rejoicing.” But they themselves will be confounded.
6 Sikieni hizo ghasia kutoka mjini, sikieni hizo kelele kutoka hekaluni! Ni sauti ya Bwana ikiwalipa adui zake yote wanayostahili.
A voice of the people from the city! A voice from the temple! The voice of the Lord repaying retribution to his enemies!
7 “Kabla hajasikia utungu, alizaa; kabla hajapata maumivu, alizaa mtoto mwanaume.
Before she was in labor, she gave birth. Before her time arrived for delivery, she gave birth to a male child.
8 Ni nani amepata kusikia jambo kama hili? Ni nani amepata kuona mambo kama haya? Je, nchi yaweza kuzaliwa kwa siku moja, au taifa laweza kutokea mara? Mara Sayuni alipoona utungu, alizaa watoto wake.
Who has ever heard of such a thing? And who has seen anything like this? Will the earth give birth in one day? Or will a nation be born all at once? For Zion has been in labor, and she has given birth to her sons.
9 Je, nilete mwana hadi wakati wa kuzaliwa na nisizalishe?” asema Bwana. “Je, nifunge tumbo la uzazi wakati mimi ndiye nizalishaye?” asema Mungu wako.
Will I, who causes others to give birth, not also give birth myself, says the Lord? Will I, who bestows generation upon others, be barren myself, says the Lord your God?
10 “Shangilieni pamoja na Yerusalemu na mfurahi kwa ajili yake, ninyi nyote mnaompenda, shangilieni kwa nguvu pamoja naye, ninyi nyote mnaoomboleza juu yake.
Rejoice with Jerusalem, and exult in her, all you who love her! Rejoice greatly with her, all you who mourn over her!
11 Kwa kuwa mtanyonya na kutosheka katika faraja ya matiti yake; mtakunywa sana, na kuufurahia wingi wa mafuriko ya ustawi wake.”
So may you nurse and be filled, from the breasts of her consolations. So may you receive milk and overflow with delights, from every portion of her glory.
12 Kwa kuwa hili ndilo asemalo Bwana: “Nitamwongezea amani kama mto, nao utajiri wa mataifa kama kijito kifurikacho; utanyonya na kuchukuliwa mikononi mwake na kubembelezwa magotini pake.
For thus says the Lord: Behold, I will turn a river of peace toward her, with an inundating torrent: the glory of the Gentiles, from which you will nurse. You will be carried at the breasts, and they will caress you upon the knees.
13 Kama mama anavyomfariji mtoto wake, ndivyo nitakavyokufariji wewe, nawe utafarijiwa huko Yerusalemu.”
In the manner of one whom a mother caresses, so will I console you. And you will be consoled in Jerusalem.
14 Wakati mtakapoona jambo hili, mioyo yenu itashangilia, nanyi mtastawi kama majani; mkono wa Bwana utajulikana kwa watumishi wake, bali ghadhabu yake kali itaonyeshwa kwa adui zake.
You will see, and your heart will be glad, and your bones will flourish like a plant, and the hand of the Lord will be known to his servants, and he will be angry with his enemies.
15 Tazama, Bwana anakuja na moto, magari yake ya vita ni kama upepo wa kisulisuli, atateremsha hasira yake kwa ghadhabu kali, na karipio lake pamoja na miali ya moto.
For behold, the Lord will arrive with fire, and his four-horse chariots will be like a whirlwind: to render his wrath with indignation, and his rebuke with flames of fire.
16 Kwa maana kwa moto na kwa upanga wake Bwana atatekeleza hukumu juu ya watu wote, nao wengi watakuwa ni wale waliouawa na Bwana.
For the Lord will divide with fire, and with his sword among all flesh, and those slain by the Lord will be many.
17 “Watu wote wanaojiweka wakfu na kujitakasa wenyewe ili kwenda bustanini, wakimfuata aliye katikati ya wale ambao hula nyama za nguruwe na panya pamoja na vitu vingine vilivyo machukizo, watafikia mwisho wao pamoja,” asema Bwana.
Those who were sanctified, who thought themselves to be clean in the gardens behind the inner gate, who were eating swine’s flesh, and the abomination, and the mouse: they will be consumed all at once, says the Lord.
18 “Nami, kwa sababu ya matendo yao na mawazo yao, niko karibu kuja na kukusanya mataifa yote na lugha zote, nao watakuja na kuuona utukufu wangu.
But I know their works and their thoughts. I am arriving, so that I may gather them together with all nations and languages. And they will approach, and they will see my glory.
19 “Nitaweka ishara katikati yao, nami nitapeleka baadhi ya hao walionusurika kwa mataifa, hadi Tarshishi, kwa Puli na Waludi (wanaojulikana kama wapiga upinde), kwa Tubali na Uyunani, hadi visiwa vya mbali ambavyo havijasikia juu ya sifa zangu au kuuona utukufu wangu. Watatangaza utukufu wangu miongoni mwa mataifa.
And I will set a sign among them. And I will send some of those who will have been saved to the Gentiles in the sea, to Africa, and to those who draw the bow in Lydia, to Italy and Greece, to islands far away, to those who have not heard of me, and to those who have not seen my glory. And they will announce my glory to the Gentiles.
20 Nao watawaleta ndugu zenu wote, kutoka mataifa yote, mpaka kwenye mlima wangu mtakatifu katika Yerusalemu kama sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, katika magari ya vita na magari makubwa, juu ya nyumbu na ngamia,” asema Bwana. “Watawaleta, kama Waisraeli waletavyo sadaka zao za nafaka, katika Hekalu la Bwana, katika vyombo safi kwa kufuata desturi za ibada.
And they will lead all of your brothers from all of the Gentiles as a gift to the Lord, on horses, and in four-horse chariots, and on stretchers, and on mules, and in coaches, to my holy mountain Jerusalem, says the Lord, in the same manner that the sons of Israel would carry an offering in a pure vessel into the house of the Lord.
21 Nami nitachagua baadhi yao pia wawe makuhani na Walawi,” asema Bwana.
And I will take from them to be priests and Levites, says the Lord.
22 “Kama vile mbingu mpya na nchi mpya ninazozifanya zitakavyodumu mbele zangu,” asema Bwana, “ndivyo jina lenu na wazao wenu watakavyodumu.
For in like manner as the new heavens and the new earth, which I will cause to stand before me, says the Lord, so will your offspring and your name stand.
23 Kutoka Mwezi Mpya hata mwingine, na kutoka Sabato hadi nyingine, wanadamu wote watakuja na kusujudu mbele zangu,” asema Bwana.
And there will be month after month, and Sabbath after Sabbath. And all flesh will approach, so as to adore before my face, says the Lord.
24 “Nao watatoka nje na kuona maiti za wale walioniasi mimi. Funza wao hawatakufa, wala moto wao hautazimika, nao watakuwa kitu cha kuchukiza sana kwa wanadamu wote.”
And they will go out, and they will view the carcasses of the men who have transgressed against me. Their worm will not die, and their fire will not be extinguished. And they will be a sight to all flesh even unto revulsion.

< Isaya 66 >