< Yeremia 8 >

1 “‘Wakati huo, asema Bwana, mifupa ya wafalme na maafisa wa Yuda, mifupa ya makuhani na manabii, na mifupa ya watu wa Yerusalemu itaondolewa kutoka makaburi yao.
W tym czasie, mówi PAN, wydobędą z ich grobów kości królów Judy, kości ich książąt, kości kapłanów, kości proroków i kości mieszkańców Jerozolimy;
2 Itawekwa wazi kwa jua, na mwezi, na nyota zote za mbingu, ambazo walizipenda na kuzitumikia, na ambazo wamezifuata kutafuta ushauri na kuziabudu. Hawatakusanywa pamoja au kuzikwa, lakini watakuwa kama mavi yaliyotapakaa juu ya ardhi.
I rozrzucą je przed słońcem, przed księżycem i przed całym zastępem nieba, które oni kochali, którym służyli, za którymi szli, których szukali i którym oddawali pokłon. Nie będą zebrane ani pogrzebane, [lecz] staną się nawozem na powierzchni ziemi.
3 Popote nitakapowafukuzia, mabaki wote wa kizazi hiki kiovu watatamani kufa kuliko kuishi, asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.’
I cała reszta ocalałych z tego przewrotnego rodu będzie wybierać [raczej] śmierć niż życie we wszystkich miejscach, gdzie zostali, kiedy ich wygnałem, mówi PAN zastępów.
4 “Waambie, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: “‘Je, watu wanapoanguka hawainuki? Je, mtu anapopotea harudi?
Dlatego powiesz do nich: Tak mówi PAN: Czy nie powstaje ten, który upadł? Czy nie zawraca ten, który zbłądził?
5 Kwa nini basi watu hawa walipotea? Kwa nini Yerusalemu inapotea kila mara? Wanangʼangʼania udanganyifu na wanakataa kurudi.
Czemu więc odwrócił się ten lud Jerozolimy wiecznym odstępstwem? Trzymają się kłamstwa, nie chcą wrócić.
6 Nimewasikiliza kwa makini, lakini hawataki kusema lililo sawa. Hakuna anayetubia makosa yake akisema, “Nimefanya nini?” Kila mmoja hufuata njia yake mwenyewe kama farasi anayekwenda vitani.
Uważałem i słyszałem: nie mówią właściwie, nikt nie żałuje swej niegodziwości, mówiąc: Cóż uczyniłem? Każdy biegnie swoją drogą, jak koń pędzący do bitwy.
7 Hata korongo aliyeko angani anayajua majira yake yaliyoamriwa, nao njiwa, mbayuwayu na koikoi hufuata majira yao ya kurudi. Lakini watu wangu hawajui Bwana anachotaka kwao.
Nawet bocian na niebiosach zna swoje ustalone pory; synogarlica, żuraw i jaskółka przestrzegają czasu swego przylotu. Lecz mój lud nie zna sądu PANA.
8 “‘Mwawezaje kusema, “Sisi tuna busara kwa sababu tunayo sheria ya Bwana,” wakati ambapo kwa hakika kalamu ya uongo ya waandishi imeandika kwa udanganyifu?
Jakże [możecie] mówić: My jesteśmy mądrzy, a prawo PANA [jest] przy nas? Oto zaprawdę na próżno uczynił je; daremne jest pióro pisarzy.
9 Wenye hekima wataaibika, watafadhaika na kunaswa. Kwa kuwa wamelikataa neno la Bwana, hiyo hekima waliyo nayo ni ya namna gani?
Mędrcy się zawstydzili. Są przestraszeni i pojmani. Oto odrzucają słowo PANA, jaką więc mają mądrość?
10 Kwa hiyo nitawapa watu wengine wake zao, na mashamba yao kwa wamiliki wengine. Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa, wote wana tamaa ya kupata zaidi; manabii na makuhani wanafanana, wote wanafanya udanganyifu.
Dlatego ich żony dam innym, ich pola tym, którzy ich zdobędą, bo od najmniejszego aż do największego – wszyscy są oddani chciwości, od proroka aż do kapłana – wszyscy działają podstępnie.
11 Wanafunga majeraha ya watu wangu bila uangalifu. Wanasema, “Amani, amani,” wakati hakuna amani.
I leczą rany córki mego ludu [tylko] powierzchownie, mówiąc: Pokój, pokój! Ale nie ma pokoju.
12 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yao inayochukiza mno? Hapana, hawana aibu hata kidogo, hawajui hata kuona haya. Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka, watashushwa chini watakapoadhibiwa, asema Bwana.
Czy zawstydzili się, że popełnili obrzydliwość? Bynajmniej, wcale się nie zawstydzili ani nie potrafili rumienić. Dlatego upadną wśród tych, co mają upaść. W czasie gdy ich nawiedzę, upadną, mówi PAN.
13 “‘Nitayaondoa mavuno yao, asema Bwana. Hapatakuwepo zabibu kwenye mzabibu. Hapatakuwepo na tini kwenye mtini, majani yake yatanyauka. Kile nilichowapa watanyangʼanywa.’”
Doszczętnie ich wykorzenię, mówi PAN. Nie będzie winogron na winorośli ani żadnych fig na drzewie figowym, nawet liść opadnie, a to, co im dałem, zostanie im zabrane.
14 “Kwa nini tunaketi hapa? Kusanyikeni pamoja! Tukimbilie kwenye miji yenye maboma, tukaangamie huko! Kwa kuwa Bwana, Mungu wetu ametuhukumu kuangamia, na kutupa maji yenye sumu tunywe, kwa sababu tumemtenda dhambi.
Czemu [tu] siedzimy? Zbierzcie się, wejdźmy do miast warownych i tam będziemy milczeć. PAN bowiem, nasz Bóg, każe nam milczeć i daje nam do picia wodę żółci, gdyż zgrzeszyliśmy przeciwko PANU.
15 Tulitegemea amani, lakini hakuna jema lililokuja, tulitegemea wakati wa kupona, lakini kulikuwa hofu tu.
Oczekiwaliśmy pokoju, ale nic dobrego [nie przyszło]; czasu uzdrowienia – a oto strach.
16 Mkoromo wa farasi za adui umesikika kuanzia Dani, kwa mlio wa madume yao ya farasi, nchi yote inatetemeka. Wamekuja kuangamiza nchi na vyote vilivyomo, mji na wote waishio ndani yake.”
Od Dan słychać parskanie jego koni, na odgłos rżenia jego mocarzy zadrżała cała ziemia. Nadciągają, aby pożreć ziemię i wszystko, co jest na niej, miasto i jego mieszkańców.
17 “Tazama, nitatuma nyoka wenye sumu kali katikati yenu, fira ambao hawawezi kulogwa, nao watawauma,” asema Bwana.
Oto bowiem poślę na was najbardziej jadowite węże, których nie można zaklinać, i będą was kąsać, mówi PAN.
18 Ee Mfariji wangu katika huzuni, moyo wangu umezimia ndani yangu.
Moje serce, które miało mnie posilać w smutku, mdleje we mnie.
19 Sikia kilio cha watu wangu kutoka nchi ya mbali: “Je, Bwana hayuko Sayuni? Je, Mfalme wake hayuko tena huko?” “Kwa nini wamenikasirisha kwa vinyago vyao, kwa sanamu zao za kigeni zisizofaa?”
Oto głos krzyku córki mego ludu z dalekiej ziemi: Czy nie ma PANA na Syjonie? Czy nie ma na nim jego króla? Czemu pobudzili mnie do gniewu swoimi bożkami i obcymi próżnościami? – [odpowiada PAN].
20 “Mavuno yamepita, kiangazi kimekwisha, nasi hatujaokolewa.”
Przeminęło żniwo, skończyło się lato, a my nie jesteśmy wybawieni.
21 Kwa kuwa watu wangu wamepondwa, nami nimepondeka pia; ninaomboleza, nayo hofu kuu imenishika.
Z powodu rany córki mojego ludu jestem ranny, pogrążony w żałobie, ogarnęło mnie przerażenie.
22 Je, hakuna zeri ya kuponya katika Gileadi? Je, hakuna tabibu huko? Kwa nini basi hakuna uponyaji wa majeraha ya watu wangu?
Czy nie ma balsamu w Gileadzie? Czy nie ma tam lekarza? Czemu więc nie jest uleczona córka mojego ludu?

< Yeremia 8 >