< Yoshua 19 >

1 Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
ויצא הגורל השני לשמעון למטה בני שמעון למשפחותם ויהי נחלתם בתוך נחלת בני יהודה׃
2 Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
ויהי להם בנחלתם באר שבע ושבע ומולדה׃
3 Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
וחצר שועל ובלה ועצם׃
4 Eltoladi, Bethuli, Horma,
ואלתולד ובתול וחרמה׃
5 Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
וצקלג ובית המרכבות וחצר סוסה׃
6 Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
ובית לבאות ושרוחן ערים שלש עשרה וחצריהן׃
7 Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
עין רמון ועתר ועשן ערים ארבע וחצריהן׃
8 pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
וכל החצרים אשר סביבות הערים האלה עד בעלת באר ראמת נגב זאת נחלת מטה בני שמעון למשפחתם׃
9 Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
מחבל בני יהודה נחלת בני שמעון כי היה חלק בני יהודה רב מהם וינחלו בני שמעון בתוך נחלתם׃
10 Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
ויעל הגורל השלישי לבני זבולן למשפחתם ויהי גבול נחלתם עד שריד׃
11 Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
ועלה גבולם לימה ומרעלה ופגע בדבשת ופגע אל הנחל אשר על פני יקנעם׃
12 Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
ושב משריד קדמה מזרח השמש על גבול כסלת תבר ויצא אל הדברת ועלה יפיע׃
13 Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
ומשם עבר קדמה מזרחה גתה חפר עתה קצין ויצא רמון המתאר הנעה׃
14 Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
ונסב אתו הגבול מצפון חנתן והיו תצאתיו גי יפתח אל׃
15 Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
וקטת ונהלל ושמרון וידאלה ובית לחם ערים שתים עשרה וחצריהן׃
16 Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
זאת נחלת בני זבולן למשפחותם הערים האלה וחצריהן׃
17 Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
ליששכר יצא הגורל הרביעי לבני יששכר למשפחותם׃
18 Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
ויהי גבולם יזרעאלה והכסולת ושונם׃
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
וחפרים ושיאן ואנחרת׃
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
והרבית וקשיון ואבץ׃
21 Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
ורמת ועין גנים ועין חדה ובית פצץ׃
22 Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
ופגע הגבול בתבור ושחצומה ובית שמש והיו תצאות גבולם הירדן ערים שש עשרה וחצריהן׃
23 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
זאת נחלת מטה בני יששכר למשפחתם הערים וחצריהן׃
24 Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
ויצא הגורל החמישי למטה בני אשר למשפחותם׃
25 Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
ויהי גבולם חלקת וחלי ובטן ואכשף׃
26 Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
ואלמלך ועמעד ומשאל ופגע בכרמל הימה ובשיחור לבנת׃
27 Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
ושב מזרח השמש בית דגן ופגע בזבלון ובגי יפתח אל צפונה בית העמק ונעיאל ויצא אל כבול משמאל׃
28 Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
ועברן ורחב וחמון וקנה עד צידון רבה׃
29 Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
ושב הגבול הרמה ועד עיר מבצר צר ושב הגבול חסה ויהיו תצאתיו הימה מחבל אכזיבה׃
30 Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
ועמה ואפק ורחב ערים עשרים ושתים וחצריהן׃
31 Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
זאת נחלת מטה בני אשר למשפחתם הערים האלה וחצריהן׃
32 Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
לבני נפתלי יצא הגורל הששי לבני נפתלי למשפחתם׃
33 Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
ויהי גבולם מחלף מאלון בצעננים ואדמי הנקב ויבנאל עד לקום ויהי תצאתיו הירדן׃
34 Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
ושב הגבול ימה אזנות תבור ויצא משם חוקקה ופגע בזבלון מנגב ובאשר פגע מים וביהודה הירדן מזרח השמש׃
35 Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
וערי מבצר הצדים צר וחמת רקת וכנרת׃
36 Adama, Rama, Hazori,
ואדמה והרמה וחצור׃
37 Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
וקדש ואדרעי ועין חצור׃
38 Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
ויראון ומגדל אל חרם ובית ענת ובית שמש ערים תשע עשרה וחצריהן׃
39 Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
זאת נחלת מטה בני נפתלי למשפחתם הערים וחצריהן׃
40 Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
למטה בני דן למשפחתם יצא הגורל השביעי׃
41 Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
ויהי גבול נחלתם צרעה ואשתאול ועיר שמש׃
42 Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
ושעלבין ואילון ויתלה׃
43 Eloni, Timna, Ekroni,
ואילון ותמנתה ועקרון׃
44 Elteke, Gibethoni, Baalathi,
ואלתקה וגבתון ובעלת׃
45 Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
ויהד ובני ברק וגת רמון׃
46 Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
ומי הירקון והרקון עם הגבול מול יפו׃
47 (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
ויצא גבול בני דן מהם ויעלו בני דן וילחמו עם לשם וילכדו אותה ויכו אותה לפי חרב וירשו אותה וישבו בה ויקראו ללשם דן כשם דן אביהם׃
48 Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
זאת נחלת מטה בני דן למשפחתם הערים האלה וחצריהן׃
49 Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
ויכלו לנחל את הארץ לגבולתיה ויתנו בני ישראל נחלה ליהושע בן נון בתוכם׃
50 kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
על פי יהוה נתנו לו את העיר אשר שאל את תמנת סרח בהר אפרים ויבנה את העיר וישב בה׃
51 Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.
אלה הנחלת אשר נחלו אלעזר הכהן ויהושע בן נון וראשי האבות למטות בני ישראל בגורל בשלה לפני יהוה פתח אהל מועד ויכלו מחלק את הארץ׃

< Yoshua 19 >