< Luka 2 >

1 Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
Now it came to pass, in those days, that there went forth a decree from Caesar Augustus, for all the inhabited earth to be enrolled:
2 (Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
this enrolment, first was made while Cyrenius was governor of Syria:
3 Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
and all were journeying to be enrolled, each one unto his own city.
4 Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
And Joseph also went up from Galilee, out of a city Nazareth, into Judaea, into the city of David which is called Bethlehem; because he was of the house and family of David:
5 Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
to enrol himself with Mary who was betrothed to him, she being with child.
6 Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
And it came to pass, while they were there, that the days were fulfilled for her to give birth;
7 naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
and she gave birth to her firstborn son, and wrapped him in swaddling clothes, and laid him in a manger, because there was no room for them in the inn.
8 Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
And there were, shepherds, in the same country, dwelling in the fields, and keeping the watches of the night over their flock.
9 Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
And, a messenger of the Lord, stood over them, and, a glory of the Lord, shone round about them; and they feared, a great fear.
10 Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
And the messenger said unto them—Be not afraid! For lo! I bring you good tidings of a great joy, the which shall be for all the people:
11 Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
That there hath been born unto you, this day, a saviour, —Who is Christ the Lord—in the city of David!
12 Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
And, this, to you is, a sign: Ye shall find a babe, wrapped in swaddling clothes, and lying in a manger.
13 Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
And, suddenly, there came to be, with the messenger, the throng of the heavenly host, praising God, and saying—
14 “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
Glory, in the highest, unto God! And, on earth, peace, among men of goodwill.
15 Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
And it came to pass, when the messengers had departed from them into heaven, that, the shepherds, began to say one to another—Let us go through forthwith as far as to Bethlehem, and see this thing which hath come to pass, which the Lord hath made known to us.
16 Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
And they came, with haste, and found both Mary and Joseph, and the babe lying in the manger.
17 Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
Now, when they beheld, they made known concerning the thing which had been told them as to this child.
18 Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
And, all who heard, marvelled concerning the things which had been told by the shepherds unto them;
19 Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
but, Mary, was closely observing, all, these things, putting them together in her heart.
20 Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
And the shepherds returned, giving glory and singing praise unto God, over all things which they had heard and seen, according as it had been told unto them.
21 Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
And, when eight days were fulfilled for circumcising him, then was his name called, Jesus, —which it was called by the messenger, before he was conceived in the womb.
22 Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
And, when the days of their purification, according to the law of Moses, were fulfilled, they took him up into Jerusalem, to present [him] unto the Lord, —
23 (kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
according as it is written in the law of the Lord—Every male that is a firstborn, Holy unto the Lord, shall be called,
24 na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
and to give a sacrifice, according to that which is said in the law of the Lord—A pair of turtle-doves, or two young pigeons.
25 Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
And lo! there was, a man, in Jerusalem, whose name, was Symeon; and, this man, was righteous and devout, awaiting the consolation of Israel, and Holy Spirit was upon him;
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
and it had been intimated to him by the Holy Spirit, that he should not see death, before he had seen the Christ of the Lord.
27 Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
And he came, in the Spirit, into the temple; and, when the parents brought in the child Jesus, that they might do according to that which was customary by the law concerning it,
28 ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
even he, welcomed it into his arms, and blessed God, and said—
29 “Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
Now, dost thou dismiss thy servant, O Sovereign, according to thy declaration—in peace;
30 Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
Because mine eyes have seen thy salvation,
31 ulioweka tayari machoni pa watu wote,
Which thou hast prepared in face of all the peoples:
32 nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
A light for the unveiling of nations, and the glory of thy people Israel.
33 Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
And his father and mother were marvelling over the things which were being spoken concerning him.
34 Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
And Symeon blessed them, and said unto Mary his mother—Lo! this one, is being set for the falling and rising of many in Israel, and for a sign to be spoken against;
35 ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
And, thou! through thy very soul, shall pass a sword, that, reasonings, may be revealed, out of many hearts.
36 Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
And there was one Anna, a prophetess, daughter of Phanuel, of the tribe of Asher; —the same, advanced in many days; having lived with a husband seven years from her virginity,
37 Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
and, she, had been a widow for as long as eighty-four years, —who left not the temple, with fastings and supplications, rendering divine service night and day; —
38 Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
and, in that very hour, coming near, she began to give thanks unto God, and to speak concerning him unto all who were waiting for the redemption of Jerusalem.
39 Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
And, when they had finished all things that were according to the law of the Lord, they returned into Galilee, into their own city, Nazareth.
40 Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
And, the child, went on growing, and waxing strong, becoming filled with wisdom; and, the favour of God, was upon it.
41 Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
And his parents used to journey yearly into Jerusalem, at the feast of the passover.
42 Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
And, when he became twelve years, and they went up, according to the custom of the feast,
43 Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
and completed the days, and then were returning, the boy Jesus remained behind in Jerusalem, —and his parents noticed it not;
44 Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
but, supposing him to be in the company, went a day’s journey, and then began to seek for him among their kinsfolk and acquaintances,
45 Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
and, not finding him, returned unto Jerusalem, seeking him.
46 Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
And it came to pass, that, after three days, they found him in the temple, sitting amidst the teachers, —both hearkening unto them, and questioning them.
47 Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
Now all who heard him were beside themselves, because of his understanding and his answers.
48 Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
And, when they behold him, they were astounded, and his mother said unto him—Child! why, hast thou dealt with us, thus? Lo! thy father and I, in anguish, were seeking thee.
49 Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
And he said unto them—Why was it that ye were seeking me? Perceived ye not, that, in the courts of my Father, I must needs be?
50 Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
And, they, understood not the thing which he spake to them.
51 Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
And he went down with them, and came to Nazareth, and was submitting himself unto them. And, his mother, was closely observing all these things in her heart.
52 Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
And, Jesus, went on advancing in wisdom, and in stature, and in favour with God and men.

< Luka 2 >