< Mathayo 12 >

1 Wakati huo Yesu alipitia kwenye mashamba ya nafaka siku ya Sabato. Wanafunzi wake walikuwa na njaa, nao wakaanza kuvunja masuke ya nafaka na kuyala.
At that time Jesus went on the Sabbath day through the grainfields. His disciples were hungry and began to pluck heads of grain and eat them.
2 Lakini Mafarisayo walipoona jambo hili, wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato.”
But when the Pharisees saw that, they said to Jesus, “See, your disciples do what is unlawful to do on the Sabbath.”
3 Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na njaa?
But Jesus said to them, “Have you never read what David did, when he was hungry, and the men who were with him?
4 Aliingia katika nyumba ya Mungu, akala mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake, jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya, isipokuwa makuhani peke yao.
He went into the house of God and ate the bread of the presence, which was unlawful for him to eat and unlawful for those who were with him, but lawful only for the priests.
5 Au hamjasoma katika Sheria kwamba siku ya Sabato makuhani huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini hawahesabiwi kuwa na hatia?
Have you not read in the law that on the Sabbath the priests in the temple profane the Sabbath but are guiltless?
6 Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.
But I say to you that one greater than the temple is here.
7 Kama mngekuwa mmejua maana ya maneno haya, ‘Nataka rehema, wala si dhabihu,’ msingewalaumu watu wasio na hatia,
If you had known what this meant, 'I desire mercy and not sacrifice,' you would not have condemned the guiltless.
8 kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”
For the Son of Man is Lord of the Sabbath.”
9 Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao,
Then Jesus left from there and went into their synagogue.
10 na huko alikuwepo mtu aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya kumshtaki Yesu, wakamuuliza, “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?”
Behold, there was a man who had a withered hand. The Pharisees asked Jesus, saying, “Is it lawful to heal on the Sabbath?” so that they might accuse him of sinning.
11 Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato hatamtoa?
Jesus said to them, “What man would there be among you, who, if he had just one sheep, and if this sheep fell into a deep hole on the Sabbath, would not grasp hold of it and lift it out?
12 Mtu ana thamani kubwa kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”
How much more valuable, then, is a man than a sheep! Therefore it is lawful to do good on the Sabbath.”
13 Ndipo akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa ukawa mzima kama ule mwingine.
Then Jesus said to the man, “Stretch out your hand.” He stretched it out, and it was restored to health, just like the other hand.
14 Lakini Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri baya juu ya Yesu jinsi watakavyoweza kumuua.
But the Pharisees went out and plotted against him. They were seeking how they might put him to death.
15 Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao, akaondoka mahali hapo. Watu wengi wakamfuata, naye akawaponya wagonjwa wao wote,
As Jesus perceived this, he withdrew from there. Many people followed him, and he healed them all.
16 akiwakataza wasiseme yeye ni nani.
He commanded them not to make him known to others,
17 Hii ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya kusema:
that it might come true, what had been said through Isaiah the prophet, saying,
18 “Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, mpendwa wangu, ninayependezwa naye. Nitaweka Roho wangu juu yake, naye atatangaza haki kwa mataifa.
“See, my servant whom I have chosen; my beloved one, in whom my soul is well pleased. I will put my Spirit upon him, and he will proclaim justice to the Gentiles.
19 Hatagombana wala hatapiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani.
He will not strive nor cry aloud; neither will anyone hear his voice in the streets.
20 Mwanzi uliopondeka hatauvunja, na utambi unaofuka moshi hatauzima, mpaka atakapoifanya haki ishinde.
He will not break any bruised reed; he will not quench any smoking flax, until he leads justice to victory,
21 Katika Jina lake mataifa wataweka tumaini lao.”
and in his name the Gentiles will have certain hope.”
22 Kisha wakamletea mtu aliyekuwa amepagawa na pepo mchafu, na alikuwa kipofu na bubu. Yesu akamponya, hata akaweza kusema na kuona.
Then someone blind and mute, possessed by a demon, was brought to Jesus. He healed him, with the result that the mute man spoke and saw.
23 Watu wote wakashangaa na kusema, “Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa Daudi?”
All the crowds were amazed and said, “Can this man be the Son of David?”
24 Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu kwa uwezo wa Beelzebuli, mkuu wa pepo wachafu.”
But when the Pharisees heard of this miracle, they said, “This man does not cast out demons except by Beelzebul, the prince of the demons.”
25 Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, hivyo akawaambia, “Kila ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila mji au watu wa nyumba moja waliogawanyika dhidi yao wenyewe hawawezi kusimama.
But Jesus knew their thoughts and said to them, “Every kingdom divided against itself is made desolate, and every city or house divided against itself will not stand.
26 Kama Shetani akimtoa Shetani, atakuwa amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme wake utawezaje kusimama?
If Satan drives out Satan, he is divided against himself. How then will his kingdom stand?
27 Nami kama natoa pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, watu wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo wa nani? Hivyo basi, wao ndio watakaowahukumu.
And if I drive out demons by Beelzebul, by whom do your sons drive them out? For this reason they will be your judges.
28 Lakini kama mimi ninatoa pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu.
But if I drive out demons by the Spirit of God, then the kingdom of God has come upon you.
29 “Au tena, mtu awezaje kuingia katika nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Akishamfunga, ndipo hakika anaweza kuteka nyara mali zake.
How can anyone enter the house of the strong man and steal his belongings without tying up the strong man first? Then he will steal his belongings from his house.
30 “Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume nami, na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami, hutawanya.
The one who is not with me is against me, and the one who does not gather with me scatters.
31 Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Therefore I say to you, every sin and blasphemy will be forgiven men, but the blasphemy against the Spirit will not be forgiven.
32 Mtu yeyote atakayesema neno dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au katika ulimwengu ujao. (aiōn g165)
Whoever speaks any word against the Son of Man, that will be forgiven him. But whoever speaks against the Holy Spirit, that will not be forgiven him, neither in this world, nor in that which is to come. (aiōn g165)
33 “Ufanye mti kuwa mzuri, nayo matunda yake yatakuwa mazuri. Au ufanye mti kuwa mbaya, na matunda yake yatakuwa mabaya. Kwa maana mti hutambulika kwa matunda yake.
Make a tree good and its fruit good, or make the tree bad and its fruit bad, for a tree is recognized by its fruit.
34 Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale yaliyoujaza moyo wake.
You offspring of vipers, since you are evil, how can you say good things? For out of the abundance of the heart his mouth speaks.
35 Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka hazina ya mambo mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka hazina ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
The good man from the good treasure of his heart produces what is good, and the evil man from the evil treasure of his heart produces what is evil.
36 Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo maana walilonena.
I say to you that in the day of judgment people will give an account for every idle word they will have said.
37 Kwa maana kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.”
For by your words you will be justified, and by your words you will be condemned.”
38 Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka kuona ishara kutoka kwako.”
Then certain scribes and Pharisees answered Jesus and said, “Teacher, we wish to see a sign from you.”
39 Lakini yeye akawajibu, “Kizazi kiovu na cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ile ishara ya nabii Yona.
But Jesus answered and said to them, “An evil and adulterous generation seeks for a sign. But no sign will be given to it except the sign of Jonah the prophet.
40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumikwa siku tatu, usiku na mchana, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, usiku na mchana.
For as Jonah was three days and three nights in the stomach of the big fish, so will the Son of Man be three days and three nights in the heart of the earth.
41 Siku ya hukumu watu wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na kukihukumu; kwa maana wao walitubu waliposikia mahubiri ya Yona. Na tazama, hapa yupo yeye aliye mkuu kuliko Yona.
The men of Nineveh will stand up at the judgment with this generation of people and will condemn it. For they repented at the preaching of Jonah, and see, someone greater than Jonah is here.
42 Malkia wa Kusini atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu kizazi hiki. Kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni. Na hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.”
The Queen of the South will rise up at the judgment with the men of this generation and condemn them. She came from the ends of the earth to hear the wisdom of Solomon, and see, someone greater than Solomon is here.
43 “Pepo mchafu amtokapo mtu, hutangatanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta mahali pa kupumzika, lakini hapati.
When an unclean spirit has gone away from a man, it passes through waterless places and looks for rest, but does not find it.
44 Ndipo husema, ‘Nitarudi kwenye nyumba yangu nilikotoka.’ Naye arudipo huikuta ile nyumba ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
Then it says, 'I will return to my house from which I came.' Having returned, it finds that house swept out and put in order.
45 Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu wengine saba wabaya kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo. Nayo hali ya mwisho ya yule mtu huwa ni mbaya kuliko ile ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu.”
Then it goes and takes along with it seven other spirits more evil than itself, and they all come in to live there. Then the final condition of that man becomes worse than the first. It will be just like that with this evil generation.”
46 Wakati alikuwa angali anazungumza na makutano, mama yake na ndugu zake wakasimama nje wakitaka kuongea naye.
While Jesus was still speaking to the crowds, behold, his mother and his brothers stood outside, seeking to speak to him.
47 Ndipo mtu mmoja akamwambia, “Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kuongea na wewe.”
Someone said to him, “Look, your mother and your brothers stand outside, seeking to speak to you.”
48 Lakini yeye akamjibu na kumwambia yule mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni nani?”
But Jesus answered and said to him who told him, “Who is my mother and who are my brothers?”
49 Akawanyooshea mkono wanafunzi wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama yangu na ndugu zangu!
Then he stretched out his hand toward his disciples and said, “See, here are my mother and my brothers!
50 Kwa maana yeyote afanyaye mapenzi ya Baba yangu wa mbinguni, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”
For whoever does the will of my Father who is in heaven, that person is my brother, and sister, and mother.”

< Mathayo 12 >