< Zaburi 98 >

1 Zaburi. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, kwa maana ametenda mambo ya ajabu; kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu umemfanyia wokovu.
מזמור שירו ליהוה שיר חדש כי נפלאות עשה הושיעה לו ימינו וזרוע קדשו׃
2 Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.
הודיע יהוה ישועתו לעיני הגוים גלה צדקתו׃
3 Ameukumbuka upendo wake na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli; miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.
זכר חסדו ואמונתו לבית ישראל ראו כל אפסי ארץ את ישועת אלהינו׃
4 Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote, ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;
הריעו ליהוה כל הארץ פצחו ורננו וזמרו׃
5 mwimbieni Bwana kwa kinubi, kwa kinubi na sauti za kuimba,
זמרו ליהוה בכנור בכנור וקול זמרה׃
6 kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume: shangilieni kwa furaha mbele za Bwana, aliye Mfalme.
בחצצרות וקול שופר הריעו לפני המלך יהוה׃
7 Bahari na ivume na kila kiliomo ndani yake, dunia na wote wakaao ndani yake.
ירעם הים ומלאו תבל וישבי בה׃
8 Mito na ipige makofi, milima na iimbe pamoja kwa furaha,
נהרות ימחאו כף יחד הרים ירננו׃
9 vyote na viimbe mbele za Bwana, kwa maana yuaja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia kwa haki na mataifa kwa haki.
לפני יהוה כי בא לשפט הארץ ישפט תבל בצדק ועמים במישרים׃

< Zaburi 98 >