< Warumi 1 >

1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
Paul, a servant of Jesus Christ, a called apostle, separated unto the glad-message of God—
2 Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
Which he promised beforehand, through his prophets, in holy scriptures—
3 yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
Concerning his Son, —who came to be of the seed of David, according to flesh,
4 na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
Who was distinguished as the Son of God—by power, according to a Holy Spirit, through means of a resurrection of the dead, —Jesus Christ our Lord;
5 Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
Through whom we have received favour and apostleship, for obedience of faith among all the nations, in behalf of his name,
6 Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
Among whom are, ye also, called of Jesus Christ:
7 Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
Unto all that are in Rome, beloved of God, called saints, favour unto you, and peace, from God our Father and Lord Jesus Christ.
8 Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
First, indeed, I give thanks unto my God, through Jesus Christ, concerning you all, because your faith is being announced throughout the whole world.
9 Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
For God is, my witness, —unto whom I am rendering divine service in my spirit, in the glad message of his Son, —how incessantly, I am making mention of you
10 katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
At all times in my prayers, —making supplication—if, by some means, even now, at any time, I may have a way opened, in the will of God, to come unto you;
11 Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
For I am longing to see you, that I may impart some spiritual gift unto you, to the end ye may be established, —
12 au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
That is to say—there may be a mutual encouragement among you, each by the other’s faith, both yours and mine.
13 Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
I do not wish however that ye should be ignorant, brethren, that, many times, have I purposed to come unto you, but have been hindered, until the present, —in order that, some fruit, I might have among you also, even as among the other nations,
14 Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
Both to Greeks and to Barbarians, both to wise and to unwise, a debtor, I am:
15 Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
Thus, the eagerness on my part—unto you also who are in Rome, to announce the joyful message.
16 Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
For I am not ashamed of the joyful message; for it is God’s power unto salvation, to every one that believeth, both to Jew [first] and to Greek;
17 Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
For, a righteousness of God, is therein revealed, —by faith unto faith: even as it is written—But, he that is righteous, by faith, shall live.
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
For there is being revealed an anger of God from heaven—against all ungodliness and unrighteousness of men who, the truth, in unrighteousness, do hold down; —
19 kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
Inasmuch as, what may be known of God, is manifest among them, for, God, unto them, hath made it manifest, —
20 Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios g126)
For, the unseen things of him, from a world’s creation, by the things made, being perceived, are clearly seen, even his eternal power and divinity, —to the end they should be without excuse; (aïdios g126)
21 Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
Inasmuch as, having come to know God, not, as God, did they glorify him, or give him thanks, but were made fruitless in their reasonings, and darkened was their undiscerning heart,
22 Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
Professing to be wise, they were made foolish,
23 na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
And, exchanged the glory of the incorruptible God, for the likeness of an image of a corruptible man, and of birds and fourfooted beasts and reptiles:
24 Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
Wherefore God gave them up in the covetings of their hearts unto impurity, so as to be dishonouring their bodies among them, —
25 Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn g165)
Who, indeed, exchanged away the truth of God for the falsehood, and rendered worship and service unto the creature rather than unto the Creator, —who is blessed unto the ages. Amen! (aiōn g165)
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
For this cause, God gave them up unto dishonourable passions; for, even their females, exchanged away the natural use into that which is against nature, —
27 Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
In like manner also, even the males, leaving the natural use of the female, flamed out in their eager desire one for another, males with males, the indecency, effecting, —and, the necessary recompence of their error, within themselves, duly receiving; —
28 Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
And, even as they did not approve to be holding, God, in acknowledgment, God gave them up unto a disapproved mind to be doing the things that are not becoming,
29 Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
Filled with all unrighteousness, wickedness, greed, baseness, full of envy, murder, strife, deceit, evil disposition,
30 wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
Whisperers, detractors, haters of God, insolent, arrogant, vain boasters, inventors of vices, unto parents unyielding,
31 wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
Without discernment, regardless of covenants, without natural affection, unmerciful: —
32 Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
Who, indeed, having acknowledged the righteous sentence of God, —that, they who such things as these do practise, are worthy of death, not only, the same things, are doing, but are even delighting together with them who are practising [them].

< Warumi 1 >