< 2 Wafalme 23 >

1 Hivyo mfalme akawatuma wajumbe waliokuwa wamemzunguka wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu.
Da sendte Kongen Bud og lod alle Judas og Jerusalems Ældste kalde sammen hos sig.
2 Kisha mfalme akapanda hadi kwenye nyumba ya Yahwe, na watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu pamoja naye, na makuhani, manabii, na watu wote, kuanzia mdogo hadi mkubwa. Kisha akasoma katika masikioni kwao maneno yote ya kitabu cha agano ambalo lililokuwa limepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Derpå gik Kongen op i HERRENs Hus, fulgt af alle Judas Mænd og alle Jerusalems Indbyggere, Præsterne, Profeterne og hele Folket, små og store, og han forelæste dem alt, hvad der stod i Pagtsbogen, som var fundet i HERRENs Hus.
3 Mfalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yahwe, kutembea pamoja na Yahwe na kukumbuka maagizo yake, kanuni zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kuthibitisha maneno ya hili agano ambalo lililokuwa limeandikwa kwenye hiki kitabu. Hivyo watu wote wakakubaliana kusimama kwenye agano
Så tog Kongen Plads ved Søjlen og sluttede Pagt for HERRENs Åsyn om, at de skulde holde sig til HERREN og holde hans Bud, Vidnesbyrd og Anordninger af hele deres Hjerte og hele deres Sjæl, for at han kunde opfylde denne Pagts Ord, således som de var skrevet i denne Bog. Og alt Folket indgik Pagten.
4 Mfalme akamwamuru Hilkia yule kuhani mkuu, makuhani chini yake, na walinzi wa lango watoe kwenye hekalu vyombo vilivyokuwa vimetengenezwa kwa ajili ya Baali na Ashera, na kwa ajili ya nyota zote za mbinguni. Akivichoma moto Yerusalimu kwenye mashamba ya bonde la Kidroni na kubeba majivu yake kwenda Betheli.
Derpå bød Kongen Ypperstepræsten Hilkija og Andenpræsten og Dørvogterne at bringe alle de Ting, der var lavet til Ba'al, Asjera og hele Himmelens Hær, ud af HERRENs Helligdom, og han lod dem opbrænde uden for Jerusalem på Markerne ved Hedron, og Asken lod han bringe til Betel.
5 Akawaondoa makuhani waliokuwa wanaabudu miungu ambao wafalme wa Yuda waliwachagua ili kwa ajili ya kufukiza ubani katika mahali pa juu kwenye miji ya Yuda na sehemu zinazoizunguka Yerusalemu-wale waliokuwa wanchoma ubani kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote za mbinguni.
Og han afsatte Afgudspræsterne, som Judas Konger havde indsat, og som havde tændt Offerild på Højene i Judas Byer og Jerusalems Omegn, ligeledes dem, som havde tændt Offerild for Ba'al og for Solen, Månen, Stjernebillederne og hele Himmelens Hær.
6 Akaiondoa Ashera kutoka kwenye hekalu la Yahwe, nje ya Yerusalemu hata bonde la Kidroni na kuichoma hapo. Akaipiga kwenye mavumbi na kuiyatupa yale mavumbi kwenye makaburi ya watu wa kawaida.
Og han lod Asjerastøtten bringe fra HERRENs Hus uden for Jerusalem til Kedrons Dal og opbrænde der, og han lod den knuse til Støv og Støvet kaste hen, hvor Småfolk havde deres Grave.
7 Akavisafisha vyumba vya makahaba ambao walikuwa kwenye hekalu la Yahwe, ambako wanawake waliposhonea nguo kwa ajili ya Ashera
Han lod Mandsskøgernes Kamre i HERRENs Hus rive ned, dem i hvilke Kvinderne vævede Kjortler til Asjera.
8 Yosia akawaleta makuhani wote nje ya miji ya Yuda na kupanajisi mahali pa juu ambako makuhani walipokuwa wakichomea ubani, kutoka Geba hata Bersheba. Akapaharibu mahala pa juu kwenye malango ambayo yaliyokuwa ya kuingilia kwenda kwenye lango la Yoshua (liwali wa mji), upande wa kushoto wa lango la mji.
Han lod alle Præsterne hente fra Judas Byer og vanhelligede Offer: højene, hvor Præsterne havde tændt offerild, fra Geba til Be'er-sjeba. Og han lod Portofferhøjen rive ned, som var ved Indgangen til Byøversten Jehosjuas Port til venstre, når man går ind ad Byporten.
9 Ingawa makuhani wa mahali pa juu hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye madhabahu ya Yahwe katika Yerusalemu, wakala mikate isiyotiwa chachu miongoni mwa ndugu zao.
Dog fik Præsterne ved Højene ikke Adgang til HERRENs Alter i Jerusalem, men de måtte spise usyret Brød blandt deres Brødre.
10 Yosia akainajisi Tofethi, ambayo ipo kwenye bonde la Ben Hinomu, ili kwamba mtu yeyote asimuweke mtoto wake wa kiume au binti yake kwenye moto kama sadaka kwa Molaki.
Han vanhelligede Ildstedet i Hinnoms Søns Dal, så at ingen mere kunde lade sin Søn eller Datter gå igennem Ilden for Molok.
11 Akawachukua farasi ambao wafalme wa Yuda waliokuwa wametolewa kwa ajili ya jua. Walikuwa kwenye eneo la lango la uingilia kwenye hekalu la Yahwe, karibu na chumba cha Nathani Meleki, msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme. Yosia akayachoma yale magari ya farasi ya jua
Han fjernede de Heste, Judas Konger havde opstillet for Solen ved Indgangen til HERRENs Hus hen imod Hofmanden Netan Me'leks Kammer i Parvarim, og Solens Vogne lod han opbrænde.
12 Yosia mfalme akayaharibu madhabahu yaliyokuwa kwenye dari ya juu ya chumba cha Ahazi, ambacho wafalme wa Yuda walikitengeneza, na madhabahu ambayo Manase aliyatengeneza kwenye behewa mbili za nyumba ya Yahwe. Yosia akazivunga vipande vipande na kuvitupa kwenye bonde la Kidroni.
Altrene, som Judas Konger havde rejst på Taget (Akaz's Tagbygning), og Altrene, som Manasse havde rejst i begge Forgårdene til HERRENs Hus, lod Kongen nebdryde og knuse på Stedet, og Støvet lod han kaste, hen i Kedrons Dal.
13 Mfalme akapaangamiza mahali pa juu magharibi mwa Yerusalemu, kusini mwa mlima wa uharibifu ambapo Sulemani mfalme wa Israeli alipajenga kwa ajili ya Ashtorithi, chukizo la Wamoabu; sanamu za karaha za Wasidoni; kwa Kemoshi, sanamu za karaha wa Moabu; na kwa Moleki, sanamu wa karaha wa watu wa Amoni.
Og Offerhøjene østen for Jerusalem på Sydsiden af Fordærvelsens Bjerg, som Kong Salomo af Israel havde bygget for Astarte; Zidoniernes væmmelige Gud, Kemosj, Moabiternes væmmelige Gud, og Milkom, Ammoniternes vederstyggelige Gud, vanhelligede Kongen.
14 Akazivunja nguzo za jiwe kuwa vipande vipande na kuziangusha chini nguzo za Ashera na kuzijaza zile sehemu kwa mifupa ya watu.
Han lod Stenstøtterne nedbryde og Asjerastøtterne omhugge og Pladsen fylde med Menneskeknogler.
15 Yosia pia akaiteketeza kabisa madhabahu iliyokuwa Betheli na mahali pa juu ambako Yeroboamu mwana wa Nebati (ambaye aliwafanya Waisraeli kuasi) aliijenga. Pia aliichoma moto ile madhabahu na mahali pa juu na kupapiga hadi pakawa vumbi. Pia akaichoma moto nguzo ya Ashera.
Også Alteret i Betel, den Offerhøj, som Jeroboam, Nebats Søn havde rejst han der forledte Israel til Synd, også det Alter tillige med Offerhøjen lod han nedbryde; Stenene lod han nedrive og knuse til Støv, og Asjerastøtten lod han opbrænde.
16 Yosia alipotazama kwenye lile eneo, akagundua kwamba yale makaburi yalikuwa juu ya mlima. Akawatuma watu kuichukua mifupa kutoka kwenye yale makaburi; kisha akaichoma kwenye madhabahu, akainajisi. Hii ilitokana na neno la Yahwe ambalo mtu wa Mungu aliliongea, yule mtu aliyekuwa ameongea haya mambo kabla.
Da Josias vendte sig om og fik Øje på Gravene på Bjerget, sendte han Folk hen og lod dem tage Benene ud af Gravene og opbrænde dem på Alteret for, at vanhellige det efter HERRENs Ord, som den Guds Mand udråbte, da han kundgjorde disse Ting,
17 Kisha akasema, “Ni ukumbusho wa nani ule ninao uona?” Mtu wa ule mji akamwambia, “Lile ni kaburi la mtu wa Mungu ambaye alikuja kutoka Yuda na kuongea kuhusu haya mambo ambayo ameyafanya dhidi ya madhabahu ya Betheli.”
Så sagde han: "Hvad er det for et Gravmæle, jeg ser der?" Byens Folk svarede ham: "Det er den Guds Mands Grav, der kom fra Juda og kundgjorde det, du nu har gjort med Alteret i Betel."
18 Hivyo Yosia akasema, “Mwacheni. Mtu asihamishe mifupa yake.” Hivyo wakaacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya nabii ambaye alikuja kutoka Samaria.
Da sagde han: "Lad ham ligge i Ro, ingen må flytte hans Ben!" Så lod de både hans og Profeten fra Samarias Ben fred.
19 Kisha Yosia akahamisha nyumba zote za mahali pa juu ambazo zilikuwa katika mji wa Samaria, ambazo wafalme wa Israeli walizokuwa wamezitengeneza, na ambazo zilizokuwa zimemgadhabisha Yahwe kwa hasira.
Også alle Offerhusene på Højene i Samarias Byer, som Israels Konger havde opført for at krænke HERREN, lod Josias fjerne, og han handlede med dem ganske som han havde gjort i Betel;
20 Aliwafanyia kile ambacho kilikuwa kimefanyika katika Betheli. Aliwachinja makuhani wote wa mahali pa juu ya madhabahu na aliichoma mifupa ya watu juu yao. Kisha akarudi Yerusalemu.
og han lod alle Højenes Præster, som var der ved Altrene, dræbe, og han opbrændte Menneskeknogler på Altrene. Så vendte han tilbage til Jerusalem.
21 Kisha mfalme akawaamuru watu wote, akisema, “Itunzeni Pasaka ya Yahwe Mungu wenu, kama ilivyoandikwa kwenye hiki kitabu cha agano.”
Derefter gav Kongen alt Folket, den Befaling: "Hold Påske for HERREN eders Gud, som der er foreskrevet her i Pagtsbogen!"
22 Hiyo Pasaka haijawahi kufanyika tangu siku za waamuzi ambao waliiongoza Israeli, wala katika siku zote za wafalme wa Israeli au Yuda.
Thi slig en Påske var ikke nogen Sinde blevet holdt i Israels og Judas Kongers Tid, ikke siden Dommerne dømte Israel;
23 Lakini katika mwaka wa kumi na nane wa Mfalme Yosia hii Pasaka ya Yahwe ilisheherekewa katika Yerusalemu.
men først i Kong Josias's attende Regeringsår blev en sådan Påske fejret for HERREN i Jerusalem.
24 Yosia pia akawafukuza wale ambao waliokuwa wameongea na wafu au na roho. Pia aliifukuza miungu ya sananmu, sanamu, na vitu vyote ambavyo ni chukizo vilivyokuwa vinaonekana katika nchi ya Yuda na katika Yerusalemu, hivyo kwa kuthibitisha yale maneno ya sheria ambayo iliyokuwa imeandikwa kwenye kitabu cha Hilkia yule kuhani aliyekuwa amepatikana kwenye nyumba ya Yahwe.
Også Dødemanerne og Sandsigerne, Husguderne, Afgudsbillederne og alle de væmmelige Guder, der var at se i Judas Land og Jerusalem, udryddede Josias for at opfylde Lovens Ord, der stod skrevet i den Bog, Præsten Hilkija havde fundet i HERRENs Hus.
25 Kabla ya Yosia, hapakuwa na mfalme kama yeye, aliyekuwa amemwelekea yahwe kwa moyo wake wote, roho yake yote, na nguvu zake zote, ambaye alifuata sheria zote za Musa. Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye.
Der havde ikke før været nogen Konge, der som han af hele sit Hjerte og hele sin Sjæl og al sin Kraft omvendte sig til HERREN og fulgte hele Mose Lov; og heller ikke efter ham opstod hans Lige.
26 Walakini, Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya Yuda kwa waabudu wapagani wote pamoja ambao Manase aliokuwa amemgadhibisha.
Alligevel lagde HERRENs mægtige Vredesglød sig ikke, thi hans Vrede var blusset op mod Juda over alle de Krænkelser, Manasse havde tilføjet ham.
27 Hivyo Yahwe akasema, “Pia nitaiondoa Yuda usoni kwangu, kama nilivyoiondoa Israeli, na nitautupilia mbali huu mji ambao nilio uchagua, Yerusalemu, na ile nyumba ambayo niliyokuwa nimesema, 'Jina langu litakuwa humo.”'
Og HERREN sagde: "Også Juda vil jeg fjerne fra mit Åsyn, ligesom jeg fjernede Israel, og jeg vil forkaste Jerusalem, denne min udvalgte By, og det Hus, om hvilket jeg har sagt: Mit Navn skal være der!"
28 Kama kwa mambo mengine yanayo muhusu Yosia, kila kitu alichofanya, je vimeandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
Hvad der ellers er at fortælle om Josias, alt, hvad han udførte, står jo optegnet i Judas Kongers Krønike.
29 Katika siku zake, Farao Neko, mfalme wa Misri, alienda kupigana dhidi ya mfalme wa Ashuru huko mto Frati. Mfalme Yosia akaenda kuonana na Neco katika mapigano, na Neko akamuua huko Megido.
I hans Dage drog Ægypterkongen Parao Neko op til Eufratfloden imod Assyrerkongen. Kong Josias rykkede imod ham, men Neko fældede ham ved Megiddo, straks han så ham.
30 Watumishi wa Yosia wakambeba kwenye gari la farasi akiwa amekufa kutoka Migido, kumleta Yerusalemu, na kumzika katika kaburi lake mwenyewe. Kisha watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtia mafuta, na kumfanya kuwa mfalme katika mahali pake.
Og hans Folk førte ham død bort fra Megiddo, bragte ham til Jerusalem og jordede ham i hans Grav. Men Folket fra Landet tog Joahaz, Josias's Søn, og salvede og hyldede ham til Bonge i hans Faders Sted.
31 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na tatu alipoanza kutawala, na alitawala miezi mitatu katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Hamutali; alikuwa binti wa Yeremia wa Libana.
Joahaz var tre og tyve År gammel, da han blev Konge, og han herskede tre Måneder i Jerusalem. Hans Moder hed Hamutal og var en Datter af Jirmeja fra, Libna.
32 Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama kila kitu ambacho babu zake walichokifanya.
Han gjorde, hvad der var ondt i HERRENs Øjne, ganske som hans Fædre.
33 Farao Neko akamfunga gerezani huko Ribla katika nchi ya Hamathi, hivyo asiweze kutawala katika Yerusalemu. Kisha Neko akaitoza Yuda talanta mia moja za fedha na talanta moja ya dhahabu.
Men Farao Neko lod ham fængsle i Ribla i Hamats Land og gjorde dermed Ende på hans Herredømme i Jerusalem og lagde en Skat af hundrede Talenter Sølv og ti Talenter Guld på Landet.
34 Farao Neko akamfanya Eliakimu mwana wa Yosia mfalme katika mahali pa Yosia baba yake, na kubadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Lakini akamchukua mfalme Yehoahazi kwenda Misri, na Yehoahazi akafia huko.
Derpå gjorde Farao Neko Eljakim, Josias's Søn, til Konge i hans Fader Josias's Sted, og han ændrede hans Navn til Jojakim; Joahaz derimod tog han med til Ægypten, og der døde han.
35 Yehoyakimu akalipa fedha na dhahabu kwa Farao. Ili akutane na amri ya Farao, Yehoyakimu akaitoza nchi na kulazimisha kila mtu miongoni mwa watu wa nchi wamlipe fedha na dhahabu kulingana na makadirio yao.
Sølvet og Guldet udredede Jojakim til Farao; men for. at kunne udrede Pengeneefter Faraos Befaling satte han Landet i Skat; efter som hver især var sat i Skat, inddrev han Sølvet og Guldet for at give Farao Neko det.
36 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala, na alitawala miaka kumi na moja katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa akiitwa Zebida; alikuwa binti wa Pedaia wa Ruma.
Jojakim var fem og tyve År gammel, da han blev Konge, og han herskede elleve År i Jerusalem. Hans Moder hed Zebida og var en Datter af Pedaja fra Ruma.
37 Yehoyakimu akafanya yale yaliyo maovu usoni kwa Yahwe, kama waliyoyafanya babu zake.
Han gjorde, hvad der var ondt i HERRENs Øjne, ganske som hans Fædre.

< 2 Wafalme 23 >