< Esta 10 >

1 Kisha Mfalme Ahusiero akaweka kodi juu ya nchi na maeneo ya bahari.
King Achashyerosh laid a tribute on the land, and on the islands of the sea.
2 Mafanikio yote na nguvu na ukuu wake, pamoja na wa Modekai ambao mfalme alimwinua, yameandikwa katika Kitabu cha Kumbukumbu ya wafalme wa Wamedi na Waajemi.
All the acts of his power and of his might, and the full account of the greatness of Mordecai, to which the king advanced him, aren't they written in the book of the chronicles of the kings of Media and Persia?
3 Modekai Muyahudi alikuwa wa pili kutoka kwa Mfalme Ahusiero. Alikuwa mkuu na maarufu miongoni mwa ndugu zake Wayahudi, kwa sababu alitetea mahitaji ya watu wake na haki za watu na akatetea amani kwa watu wote.
For Mordecai the Jew was next to King Achashyerosh, and great among the Jews, and accepted by the multitude of his brothers, seeking the good of his people, and speaking peace to all his descendants.

< Esta 10 >