< Mwanzo 5 >

1 Hii ni orodha ya vizazi vya Adamu. Katika siku ambayo Mungu alimuumba mtu, aliwaumba katika mfano wake mwenyewe.
Questo è il libro della posterità d’Adamo. Nel giorno che Dio creò l’uomo, lo fece a somiglianza di Dio;
2 Mwanaume na mwanamke aliwaumba. Akawabariki na akawaita Adam wakati walipoumbwa.
li creò maschio e femmina, li benedisse e dette loro il nome di “uomo”, nel giorno che furon creati.
3 Wakati Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, akamzaa mwana katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake, na akamuita jina lake Sethi.
Adamo visse centotrent’anni, generò un figliuolo, a sua somiglianza, conforme alla sua immagine, e gli pose nome Seth;
4 Baada ya Adamu kumzaa Sethi, aliishi miaka mia nane. Akawazaa wana wengi waume na wake.
e il tempo che Adamo visse, dopo ch’ebbe generato Seth, fu ottocento anni, e generò figliuoli e figliuole;
5 Adamu akaishi miaka 930 kisha akafariki.
e tutto il tempo che Adamo visse fu novecentotrenta anni; poi morì.
6 Wakati Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi.
E Seth visse centocinque anni, e generò Enosh.
7 Baada ya kumzaa Enoshi, akaishi miaka 807 na akawazaa wana wengi waume na wake.
E Seth, dopo ch’ebbe generato Enosh, visse ottocentosette anni, e generò figliuoli e figliuole;
8 Sethi akaishi miaka 912 kisha akafariki.
e tutto il tempo che Seth visse fu novecentododici anni; poi morì.
9 Wakati Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani.
Ed Enosh visse novant’anni, e generò Kenan.
10 Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
Ed Enosh, dopo ch’ebbe generato Kenan, visse ottocentoquindici anni, e generò figliuoli e figliuole;
11 Enoshi aliishi miaka 905 na kisha akafariki.
e tutto il tempo che Enosh visse fu novecentocinque anni; poi morì.
12 Wakati Kanani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli.
E Kenan visse settant’anni, e generò Mahalaleel.
13 Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
E Kenan, dopo ch’ebbe generato Mahalaleel, visse ottocentoquaranta anni, e generò figliuoli e figliuole;
14 Kenani aliishi miaka 910, na kisha akafariki.
e tutto il tempo che Kenan visse fu novecentodieci anni; poi morì.
15 Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, alimzaa Yaredi.
E Mahalaleel visse sessantacinque anni, e generò Jared.
16 Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830. Akazaa wana wengi wa ume na wake.
E Mahalaleel, dopo ch’ebbe generato Jared, visse ottocentotrenta anni, e generò figliuoli e figliuole;
17 Mahalaleli aliishi miaka 895 na kisha akafariki.
e tutto il tempo che Mahalaleel visse fu ottocento novantacinque anni; poi morì.
18 Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, alimzaa Henoko.
E Jared visse cento sessantadue anni, e generò Enoc.
19 Baada ya kumzaa Henoko, Yaredi aliishi miaka mianane. Akazaa wana wengi waume na wake.
E Jared, dopo ch’ebbe generato Enoc, visse ottocento anni, e generò figliuoli e figliuole;
20 Yaredi aliishi miaka 962 na kisha akafariki.
e tutto il tempo che Jared visse fu novecento sessantadue anni; poi morì.
21 Henoko alipokuwa ameishi miaka sitini na tano, akamzaa Methusela.
Ed Enoc visse sessantacinque anni, e generò Methushelah.
22 Henoko akaenenda na Mungu miaka miatatu baada ya kumzaa Methusela. Aliwazaa wana wengi wa ume na wake.
Ed Enoc, dopo ch’ebbe generato Methushelah, camminò con Dio trecento anni, e generò figliuoli e figliuole;
23 Henoko aliishi miaka 365.
e tutto il tempo che Enoc visse fu trecento sessantacinque anni.
24 Henoko alienenda na Mungu, na kisha alitoweka, kwa kuwa Mungu alimtwaa.
Ed Enoc camminò con Dio; poi disparve, perché Iddio lo prese.
25 Wakati Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, alimzaa Lameki.
E Methushelah visse cento ottantasette anni e generò Lamec.
26 Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782. Akawazaa wana wengi wa ume na wake.
E Methushelah, dopo ch’ebbe generato Lamec, visse settecento ottantadue anni, e generò figliuoli e figliuole;
27 Methusela aliishi miaka 969. Kisha akafariki.
e tutto il tempo che Methushelah visse fu novecento sessantanove anni; poi morì.
28 Wakati Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana.
E Lamec visse cento ottantadue anni, e generò un figliuolo;
29 Akamuita jina lake Nuhu, akisema, “Huyu ndiye atatupatia pumziko kutoka katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu, ambayo lazima tuifanye kwa sababu ya ardhi ambayo Yahwe ameilaani.”
e gli pose nome Noè, dicendo: “Questo ci consolerà della nostra opera e della fatica delle nostre mani cagionata dal suolo che l’Eterno ha maledetto”.
30 Lameki aliishi miaka 595 baada ya kumzaa baba wa Nuhu. Akazaa wanawengi wa ume na wake.
E Lamec, dopo ch’ebbe generato Noè, visse cinquecento novantacinque anni, e generò figliuoli e figliuole;
31 Lameki aliishi miaka 777. Kisha akafariki.
e tutto il tempo che Lamec visse fu settecento settantasette anni; poi morì.
32 Baada ya Nuhu kuishi miaka miatano, akamzaa Shemu, Hamu, na Yafethi.
E Noè, all’età di cinquecento anni, generò Sem, Cam e Jafet.

< Mwanzo 5 >