< Hosea 1 >

1 Hili ni neno la Bwana lililofika kwa Hosea mwana wa Beeri siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na katika siku za Yeroboamu mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli.
The Lord’s message to Hosea son of Beeri during the reigns of Kings Uzziah, Jotham, Ahaz, and Hezekiah of Judah and during the reign of King Jeroboam, son of Joash of Israel.
2 Wakati Bwana alipozungumza kwanza kupitia Hosea, akamwambia, “Nenda ukajitwalie mke ambaye ni kahaba. Atakuwa na watoto ambao ni matokeo ya ukahaba wake. Kwa maana nchi inafanya uzinzi mkubwa kwa kumwacha Bwana.”
When the Lord began to speak through Hosea, he said to him: “Go marry an unfaithful woman who will bear you children by her adultery, for like an adulterous wife the land is unfaithful to the Lord.”
3 Basi Hosea akaenda akamwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba, akazaa mtoti mwanamume.
So he married Gomer, the daughter of Dibliam, and when she conceived and bore him a son,
4 Bwana akamwambia Hosea, Mwite jina lake Yezreeli. Kwa maana kwa muda mfupi nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa sababu ya kumwaga damu huko Yezreeli; nami nitamaliza ufalme wa nyumba ya Israeli.
the Lord said: “Call him ‘Jezreel,’ for in a little while I will punish the dynasty of Jehu for the blood shed at the valley of Jezreel, I will cause the kingdom of Israel to cease.
5 Itatokea siku ile nitakapovunja upinde wa Israeli katika bonde la Yezreeli.
On that day, I will break Israel’s bows and arrows in the valley of Jezreel.”
6 Gomeri akachukua mimba tena akamzaa binti. Ndipo Bwana akamwambia Hosea, “Mwite jina lake Lo Ruhama; kwa maana sitawahurumia tena nyumba ya Israeli, nisije nikawasamehe kwa njia yoyote.
When she conceived again and bore a daughter, the Lord said to Hosea: “Call her Lo-Ruhamah – ‘No-Compassion’ for I will no longer have compassion on Israel, certainly not spare them.
7 Hata hivyo nitawahurumia nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa mwenyewe, Bwana, Mungu wao. Sitawaokoa kwa upinde, upanga, vita, farasi, au wapanda farasi. '
But on Judah I will have compassion, I will deliver them by the Lord their God, but I will not deliver them by bow nor by sword, nor by battle nor by horses nor by horsemen.”
8 Baada ya Gomeri kumwachisha Lo Ruhama, alipata mimba na kuzaa mtoto mwingine mwanamume.
After she had weaned No-Compassion, and when she conceived and bore a son, he said:
9 Ndipo Bwana akasema, “Mwite jina la Lo Ami; kwa kuwa ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.”
“Call him Lo-Ammi – ‘Not-My-People’ for you, Israel, are not my people, and I indeed am not your God.”
10 Hata hivyo idadi ya watu wa Israeli itakuwa kama mchanga wa bahari, ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa. Itakuwa pale ambapo waliambiwa, “Ninyi si watu wangu,” wataambiwa, “Ninyi ni watu wa Mungu aliye hai.”
Yet the number of the Israelites will be as the sand of the sea, which cannot be measured or counted, and where they were told, “You are not my people,” they will be called, “children of the living God.”
11 Watu wa Yuda na watu wa Israeli watakusanyika pamoja. Wao wataweka kiongozi mmoja wao wenyewe, na watatoka kutoka nchi, kwa maana itakuwa siku ya Yezreeli kuu.
The Judeans and the Israelites will join together again, will appoint for themselves one leader, will return to their own land. Great will be the day of Jezreel!

< Hosea 1 >