< Ayubu 17 >

1 Roho yangu imemezwa, na siku zangu zimekwisha; kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.
My breath is corrupt: my dayes are cut off, and the graue is readie for me.
2 Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami; ni lazima daima jicho langu litazame kukasirisha kwao.
There are none but mockers with mee, and mine eye continueth in their bitternesse.
3 Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe; nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?
Lay downe nowe and put me in suretie for thee: who is hee, that will touch mine hand?
4 Kwa kuwa wewe Mungu umemeitunza mioyo yao kutoka katika ufahamu; kwa hiyo, wewe hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.
For thou hast hid their heart from vnderstanding: therefore shalt thou not set them vp on hie.
5 Yeye ambaye huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo, macho ya watoto wake yatashindwa kuona.
For the eyes of his children shall faile, that speaketh flattery to his friends.
6 Lakini amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu; wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.
Hee hath also made mee a byword of the people, and I am as a Tabret before them.
7 Jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni; sehemu zangu zote za mwili ni nyembamba kama vivuli.
Mine eye therefore is dimme for griefe, and all my strength is like a shadowe.
8 Watu wanyoofu watapendezwa na hiki; mtu asiye na hatia atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi ya watu wasiomcha Mungu.
The righteous shalbe astonied at this, and the innocent shalbe moued against ye hypocrite.
9 Mtu mwenye haki ataendelea katika njia yake; yeye ambaye ana mikono iliyo safi ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi.
But the righteous wil holde his way, and he whose hands are pure, shall increase his strength.
10 Lakini kama ilivyo kwenu ninyi nyote, njooni sasa; Mimi sitampata mtu mwenye hekima miongoni mwenu ninyi.
All you therefore turne you, and come nowe, and I shall not finde one wise among you.
11 Siku zangu zimepita; mipango yangu imenyamazishwa na hivyo ni matumaini ya moyo wangu.
My dayes are past, mine enterprises are broken, and the thoughts of mine heart
12 Watu hawa, wenye kukejeli, badili usiku kuwa mchana; mchana uko karibu kuwa giza.
Haue changed the nyght for the day, and the light that approched, for darkenesse.
13 Tangu mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu; tangu Mimi nimetandaza kiti changu katika giza; (Sheol h7585)
Though I hope, yet the graue shall bee mine house, and I shall make my bed in the darke. (Sheol h7585)
14 tangu Mimi nimesema na shimo 'Wewe ni baba yangu,' na kwa funza, 'Wewe ni mama yangu au dada yangu;
I shall say to corruption, Thou art my father, and to the worme, Thou art my mother and my sister.
15 liko wapi tena tumaini langu? Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?
Where is then now mine hope? or who shall consider the thing, that I hoped for?
16 Tumaini litakwenda pamoja na mimi katika milango ya Kuzimu wakati sisi tutakapokwenda katika mavumbi? (Sheol h7585)
They shall goe downe into the bottome of the pit: surely it shall lye together in the dust. (Sheol h7585)

< Ayubu 17 >