< Waamuzi 16 >

1 Samsoni alikwenda Gaza na akamwona kahaba huko, naye akalala pamoja naye.
Or, Samson alla à Gaza, et il y vit une courtisane, et entra chez elle.
2 Watu wa Gaza wakaambiwa, “Samsoni amekuja hapa.” Watu wa Gaza wakazunguka mahali hapo kwa siri, wakamngoja usiku wote katika lango la jiji. Walikaa kimya usiku wote. Wakisema, “Hebu tusubiri mpaka mchana, na kisha tumwuue.”
Et on dit à ceux de Gaza: Samson est venu ici. Alors ils l'environnèrent, se tinrent en embuscade toute la nuit à la porte de la ville, et se tinrent tranquilles toute la nuit, en disant: Au point du jour, nous le tuerons.
3 Samsoni akalala kitandani mpaka usiku wa manane. Usiku wa manane akaamka na akashika mlango wa jiji na miimo yake miwili. Akavivuta kutoka nje, komeo na vyote, akaviweka kwenye mabega yake, akavichukua hadi juu ya kilima, mbele ya Hebroni.
Mais Samson demeura couché jusqu'à minuit; et vers minuit il se leva, saisit les battants de la porte de la ville et les deux poteaux, et, les ayant enlevés avec la barre, il les mit sur ses épaules, et les porta au sommet de la montagne qui est en face d'Hébron.
4 Baada ya hayo, Samsoni alimpenda mwanamke aliyeishi katika bonde la Soreki. Jina lake alikuwa Delila.
Après cela, il aima une femme dans la vallée de Sorek; elle se nommait Délila.
5 Wale wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakamwambia, “mdanganye Samsoni ili uone mahali zilipo nguvu zake kuu, na kwa namna gani tunaweza kumshinda, ili tumfunge na kumtesa. Fanya hili, na kila mmoja wetu atakupa vipande 1, 100 vya fedha.”
Et les princes des Philistins montèrent vers elle, et lui dirent: Flatte-le, et sache de lui en quoi consiste sa grande force, et comment nous pourrions le vaincre, afin que nous le liions pour le dompter; et nous te donnerons chacun mille et cent pièces d'argent.
6 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Tafadhali, niambie ni kwa jinsi gani wewe ni mwenye nguvu sana, na kwa namna gani mtu anaweza kukufunga, ili aweze kukudhibiti?”
Délila dit donc à Samson: Dis-moi, je te prie, d'où vient ta grande force, et avec quoi il faudrait te lier pour te dompter.
7 Samsoni akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba saba safi ambazo hazijakauka, nitakuwa dhaifu na kuwa kama mtu mwingine yeyote.”
Et Samson lui répondit: Si on me liait avec sept cordes fraîches, qui ne fussent point encore sèches, je deviendrais faible, et je serais comme un autre homme.
8 Basi wakuu wa Wafilisti wakamletea Delila kamba saba ambazo hazijakauka, naye akamfunga Samsoni.
Les princes des Philistins apportèrent à Délila sept cordes fraîches, qui n'étaient point encore sèches, et elle l'en lia.
9 Sasa alikuwa na watu waliojificha kwa siri, walikaa katika chumba chake cha ndani. Akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Lakini akazikata kamba kama uzi wakati unapogusa moto. Na hawakujifunza siri ya nguvu zake.
Or, des gens étaient en embuscade chez elle, dans une chambre; et elle lui dit: Les Philistins sont sur toi, Samson! Mais il rompit les cordes, comme se rompt un cordon d'étoupes lorsqu'il sent le feu; et le secret de sa force ne fut point connu.
10 Ndipo Delila akamwambia Samsoni, “Ndivyo ulivyonidanganya mimi na kuniambia uongo. Tafadhali, niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.”
Puis Délila dit à Samson: Voici, tu t'es moqué de moi, et tu m'as dit des mensonges. Je te prie, déclare-moi maintenant avec quoi il faut te lier.
11 Akamwambia, “Ikiwa watanifunga na kamba mpya ambayo haijawahi kutumika kwa kazi, nitakuwa dhaifu na kama mtu mwingine yeyote.”
Et il lui répondit: Si on me liait de grosses cordes neuves, dont on ne se serait jamais servi, je deviendrais faible, et je serais comme un autre homme.
12 Basi Delila alichukua kamba mpya akamfunga pamoja naye, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako Samsoni!” Watu waliokuwa wakisubiri walikuwa ndani ya chumba cha ndani. Lakini Samsoni akaondoa kamba kutoka mikono yake kama kilikuwa kipande cha uzi.
Délila prit donc de grosses cordes neuves, et elle lia Samson; puis elle lui dit: Les Philistins sont sur toi, Samson! Or des gens étaient en embuscade dans une chambre. Mais il rompit comme un fil les grosses cordes qu'il avait aux bras.
13 Delila akamwambia Samsoni, “Mpaka sasa umenidanganya na kuniambia uongo. Niambie kwa namna gani unaweza kufungwa.” Samsoni akamwambia, 'Ikiwa utavifuma vifungo saba vya nywele zangu na kuvifunga kwenye kitambaa, kisha kufunga kwenye msumari, nitakuwa kama mtu mwingine yeyote.”
Puis Délila dit à Samson: Jusqu'à présent tu t'es moqué de moi, et tu m'as dit des mensonges. Déclare-moi avec quoi il faudrait te lier. Et il lui dit: Ce serait si tu tissais sept tresses de ma tête dans la chaîne de ton métier.
14 Alipokuwa amelala, Dalila akavifuma vifungo saba vya nywele zake akavifunga ndani ya kitambaa na kuzifunga kwenye msumari, akamwambia, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka kutoka usingizini akang'oa kitambaa na pini zilizokuwa zimefungwa.
Et elle les fixa par la cheville; et elle dit: Les Philistins sont sur toi, Samson! Mais il se réveilla de son sommeil, et arracha la cheville du métier avec le tissu.
15 Akamwambia, “Wawezaje kusema,” Unanipenda, wakati hushiriki siri zako na mimi? Umenidhihaki mara tatu hizi na hukukuambia ni kwa jinsi gani unazo nguvu nyingi.”
Alors elle lui dit: Comment peux-tu dire: Je t'aime! Puisque ton cœur n'est point avec moi? Tu t'es moqué de moi trois fois, et tu ne m'as point déclaré d'où vient ta grande force.
16 Kila siku alisisitiza kwa bidii na maneno yake, naye akamkemea sana kiasi kwamba alitamani kufa.
Et elle le pressait tous les jours par ses paroles, et le tourmentait, de sorte que son âme en était affligée jusqu'à la mort.
17 Basi Samsoni alimwambia kila kitu, akamwambia, “Wembe haujawahi kukata nywele juu ya kichwa changu, kwa maana nimekuwa Mnaziri kwa Mungu kutoka tumboni mwa mama yangu. Ikiwa kichwa changu kitanyolewa, basi nguvu zangu zitaniacha, nami nitakuwa dhaifu na kuwa kama kila mtu mwingine. '
Alors il lui ouvrit tout son cœur, et lui dit: Le rasoir n'a jamais passé sur ma tête; car je suis Nazarien de Dieu, dès le sein de ma mère. Si j'étais rasé, ma force m'abandonnerait, et je deviendrais faible, et je serais comme tout autre homme.
18 Delila alipoona kwamba amemwambia ukweli juu ya kila kitu, akawatuma na kuwaita watawala wa Wafilisti, akisema, “Njooni tena, kwa maana ameniambia kila kitu.” Ndipo wakuu wa Wafilisti wakamwendea, wakaleta fedha mkononi mwao.
Délila, voyant qu'il lui avait ouvert tout son cœur, envoya appeler les princes des Philistins, et leur fit dire: Montez cette fois; car il m'a ouvert tout son cœur. Les princes des Philistins montèrent donc vers elle, et apportèrent l'argent dans leurs mains.
19 Alimfanya alale katika magoti yake. Alimwita mtu avinyoe vifungo saba vya kichwa chake, naye akaanza kumshinda, kwa maana nguvu zake zilikuwa zimemwacha.
Et elle l'endormit sur ses genoux; et, ayant appelé un homme, elle lui fit raser sept tresses des cheveux de sa tête. Elle commença ainsi à le dompter, et sa force l'abandonna.
20 Alisema, “Wafilisti wako juu yako, Samsoni!” Aliamka nje ya usingizi wake akasema, “Nitatoka nje kama nyakati nyingine na kujiweka huru.” Lakini hakujua kwamba Bwana amemwacha.
Alors elle dit: Les Philistins sont sur toi, Samson! Et il s'éveilla de son sommeil, et dit: J'en sortirai comme les autres fois, et je me dégagerai de leurs mains. Mais il ne savait pas que l'Éternel s'était retiré de lui.
21 Wafilisti walimkamata na kumng'oa macho. Wakampeleka Gaza na kumfunga kwa shaba. Alikuwa akisaga ngano katika gerezani.
Les Philistins le saisirent donc, et lui crevèrent les yeux. Ils le firent descendre à Gaza, et le lièrent de deux chaînes d'airain; et il tournait la meule dans la prison.
22 Lakini nywele juu ya kichwa chake zilianza kukua tena baada ya kunyolewa.
Cependant les cheveux de sa tête recommencèrent à croître, depuis qu'il avait été rasé.
23 Watawala wa Wafilisti walikusanyika ili kutoa dhabihu kubwa kwa Dagoni mungu wao, na kufurahi. Walisema, “mungu wetu amemshinda Samsoni, adui yetu, na kumtia katika ufahamu wetu.”
Or, les princes des Philistins s'assemblèrent pour offrir un grand sacrifice à Dagon, leur dieu, et pour se réjouir. Et ils dirent: Notre dieu a livré entre nos mains Samson, notre ennemi.
24 Watu walipomwona, walimsifu mungu wao, kwa sababu walisema, “mungu wetu ameshinda adui yetu na kutupa sisi - mharibifu wa nchi yetu, ambaye aliwaua wengi wetu.”
Et quand le peuple le vit, ils célébrèrent leur dieu, en disant: Notre dieu a livré entre nos mains notre ennemi, le destructeur de notre pays, et celui qui en a tant tué d'entre nous.
25 Walipokuwa wakisherehekea, wakasema, 'Mwite Samsoni, aje kutufurahisha.' Walimwita Samsoni nje ya jela na akawafanya wacheke. Walimsimamisha katikati ya nguzo.
Or, comme ils avaient le cœur joyeux, ils dirent: Faites venir Samson, et qu'il nous divertisse. Ils appelèrent donc Samson et le tirèrent de la prison, et il jouait devant eux; et ils le firent tenir entre les piliers.
26 Samsoni akamwambia yule kijana ambaye alikuwa ameshika mkono wake, 'Niruhusu nishike nguzo zilizoshikilia nyumba hii, ili nipate kuegemea.”
Alors Samson dit au garçon qui le tenait par la main: Place-moi, et fais-moi toucher les piliers qui soutiennent la maison, afin que je m'y appuie.
27 Sasa nyumba ilikuwa imejaa wanaume na wanawake. Watawala wote wa Wafilisti walikuwa huko. Juu ya paa kulikuwa na wanaume na wanawake elfu tatu, ambao walikuwa wakiangalia wakati Samsoni alipokuwa akiwafurahisha.
Or, la maison était pleine d'hommes et de femmes, et tous les princes des Philistins y étaient; il y avait même sur la plate-forme près de trois mille personnes, hommes et femmes, qui regardaient Samson jouer.
28 Samsoni akamwita Bwana, akasema, “Bwana MUNGU, nipe nia! Tafadhali niimarishe mara moja tu, Mungu, ili nipate kulipiza kisasi kwa Wafilisti kwa kuchukua macho yangu mawili.
Alors Samson invoqua l'Éternel, et dit: Seigneur Éternel, je te prie, souviens-toi de moi! ô Dieu, je te prie, fortifie-moi seulement cette fois, et que je me venge des Philistins pour la perte de mes deux yeux!
29 Samsoni aliweka nguzo mbili katikati ambzo zinashikilia nyumba hiyo, naye akaegemea juu yake, nguzo moja kwa mkono wake wa kuume, na mwingine kwa kushoto kwake.
Et Samson embrassa les deux piliers du milieu, sur lesquels la maison reposait, et il s'appuya contre eux; l'un était à sa droite et l'autre à sa gauche.
30 Samsoni akasema, “Na nife pamoja na Wafilisti!” Alipanda kwa nguvu zake na jengo likaanguka juu ya watawala na juu ya watu wote waliokuwa ndani yake. Hivyo waliouawa wakati alikufa walikuwa zaidi ya wale waliouawa wakati wa maisha yake.
Et il dit: Que je meure avec les Philistins! Puis il s'étendit de toute sa force, et la maison tomba sur les princes et sur tout le peuple qui y était. Et il fit mourir beaucoup plus de gens dans sa mort, qu'il n'en avait fait mourir pendant sa vie.
31 Kisha ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakashuka. Wakamchukua, wakamrudisha na kumzika kati ya Sora na Eshtaoli katika mahali pa kuzikwa Manoa, baba yake. Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini.
Ensuite ses frères et toute la maison de son père descendirent, et l'emportèrent; et, étant remontés, ils l'ensevelirent entre Tsora et Eshthaol, dans le tombeau de Manoah son père. Il avait jugé Israël pendant vingt ans.

< Waamuzi 16 >