< Nehemia 4 >

1 Sanbalati alipoposikia tulikuwa tukijenga ukuta, akaghadhabika ndani yake, naye akakasirika sana, akawacheka Wayahudi.
But when Sanballat heard that we builded the wall, then was he wroth and sore grieued, and mocked the Iewes,
2 Mbele ya ndugu zake na jeshi la Samaria, akasema, “Wayahudi dhaifu hawa wanafanya nini? Je, watajifanyia mji wenyewe? Je, watatoa dhabihu? Je, wataimaliza kazi siku moja? Je! Watawaletea mawe kutoka kwenye kifusi baada ya kuchomwa moto?
And sayde before his brethren and the armie of Samaria, thus he sayde, What doe these weake Iewes? wil they fortifie them selues? wil they sacrifice? will they finish it in a day? will they make the stones whole againe out of the heapes of dust, seeing they are burnt?
3 Tobia Mwamoni alikuwa pamoja naye, naye akasema, 'Ikiwa tu mbweha angepanda juu ya hichi wanachokijenga, angeubomoa ukuta huo wa mawe.”
And Tobiah the Ammonite was beside him, and said, Although they buylde, yet if a foxe goe vp, he shall euen breake downe their stonie wall.
4 Tusikilize, Mungu wetu, kwa maana sisi tunatukanwa. Rudisha malalamiko yao juu ya vichwa vyao wenyewe na kuwapa wapate kutekwa katika nchi ambapo wao ni wafungwa.
Heare, O our God (for we are despised) and turne their shame vpon their owne head, and giue them vnto a pray in the lande of their captiuitie,
5 Usiufunike uovu wao, wala usiondoe dhambi zao mbele yako; kwa sababu wamewachukiza wanaojenga.
And couer not their iniquitie, neither let their sinne be put out in thy presence: for they haue prouoked vs before the builders.
6 Kwa hiyo tulijenga ukuta na ukuta wote uliunganishwa kwa nusu ya urefu wake, kwa kuwa watu walikuwa na hamu ya kufanya kazi
So we built the wall, and all the wall was ioyned vnto the halfe thereof, and the heart of the people was to worke.
7 Lakini Sanbalati, Tobia, Waarabu, Waamoni, na Waashdodi waliposikia kwamba kazi ya ukarabati wa kuta za Yerusalemu ilikuwa ikiendelea, na kwamba sehemu zilizovunjika katika ukuta zilikuwa zimefungwa, ghadhabu kubwa ikawaka ndani yao.
But when Sanballat, and Tobiah, and the Arabians, and the Ammonites, and the Ashdodims heard that the walles of Ierusalem were repayred, (for the breaches began to be stopped) then they were very wroth,
8 Wote walifanya shauri pamoja, na walikuja kupigana dhidi ya Yerusalemu na kusababisha machafuko ndani yake.
And conspired all together to come and to fight against Ierusalem, and to hinder them.
9 Lakini tuliomba kwa Mungu wetu na kuweka walinzi kama ulinzi dhidi yao mchana na usiku kwa sababu ya tishio lao.
The we prayed vnto our God, and set watchmen by them, day and night, because of them.
10 Kisha watu wa Yuda wakasema, “Nguvu ya wale wanaobeba mizigo inashindwa. Kuna kifusi kikubwa, na hatuwezi kujenga ukuta.”
And Iudah said, The strength of the bearers is weakened, and there is much earth, so that we are not able to build the wall.
11 Na adui zetu wakasema,” Wala hawatajua au kuona mpaka tutakapokuja kati yao na kuwaua, na kuisimamisha kazi.”
Also our aduersaries had sayde, They shall not knowe, neither see, till we come into the middes of them and slay them, and cause the worke to cease.
12 Wakati huo Wayahudi waliokuwa wakiishi karibu nao walitoka pande zote na kuzungumza nasi mara kumi, wakituonya juu ya mipango waliyofanya dhidi yetu.
But when the Iewes (which dwelt beside them) came, they told vs ten times, From all places whence ye shall returne, they wil be vpon vs.
13 Kwa hiyo nikaweka watu katika sehemu za chini za ukuta katika sehemu zilizo wazi. Niliweka kila familia wenye upanga, mikuki, na upinde.
Therefore set I in the lower places behind the wall vpon the toppes of the stones, and placed the people by their families, with their swordes, their speares and their bowes.
14 Nikatazama, nikasimama, nikawaambia wakuu, na watawala, na watu wengine, “Msiogope. mkumbukeni Bwana, ambaye ni mkuu na wa kushangaza. Wapiganie ndugu zenu, wana zenu, binti zenu, wake zenu na nyumba zenu.
Then I behelde, and rose vp, and said vnto the Princes, and to the rulers, and to the rest of the people, Be not afrayde of them: remember the great Lord, and fearefull, and fight for your brethren, your sonnes, and your daughters, your wiues, and your houses.
15 Ilipokuwa wakati adui zetu waliposikia kwamba mipango yao ilikuwa inayojulikana kwetu, na Mungu alikuwa amebatilisha mipango yao, sote tulirudi ukutani, kila mmoja kwa kazi yake.
And when our enemies heard that it was knowen vnto vs, then God brought their counsell to nought, and we turned all againe to the wall, euery one vnto his worke.
16 Kwa hiyo tangu wakati huo nusu ya watumishi wangu walifanya kazi tu juu ya kujenga ukuta, na nusu yao wakaishika mikuki, ngao, pinde, na kuvaa silaha, wakati viongozi walisimama nyuma ya watu wote wa Yuda.
And from that day, halfe of the yong men did the labour, and the other halfe part of them helde the speares, and shieldes, and bowes, and habergins: and the rulers stoode behinde all the house of Iudah.
17 Na hivyo wafanyakazi haohao ambao walikuwa wakijenga ukuta na kubeba mizigo walikuwa pia wakilinda nafasi zao. Kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono mwingine alikuwa na silaha yake.
They that buylded on the wall, and they that bare burdens, and they that laded, did the worke with one hand, and with the other helde the sworde.
18 Kila mjenzi alivaa upanga wake ubavuni mwake na ndivyo alivyojenga. Yule aliyepiga tarumbeta akakaa karibu nami.
For euery one of the buylders had his sworde girded on his loynes, and so buylded: and he that blewe the trumpet, was beside me.
19 Niliwaambia wakuu na viongozi na watu wengine, “Kazi ni nzuri na ya kina, na tumejitenga kwenye ukuta, mbali na mtu mwingine.
Then saide I vnto the Princes, and to the rulers, and to the rest of the people, The worke is great and large, and we are separated vpon the wall, one farre from another.
20 Lazima mkimbilie mahali ambapo mtasikia sauti ya tarumbeta na kusanyika huko. Mungu wetu atatupigania.”
In what place therefore ye heare the sound of the trumpet, resort ye thither vnto vs: our God shall fight for vs.
21 Kwa hiyo tulifanya kazi hiyo. Nusu yao walikuwa wakichukua mikuki kutoka kupambazuka asubuhi hadi kutokea kwa nyota.
So we laboured in the worke, and halfe of them helde the speares, from the appearing of the morning, till the starres came foorth.
22 Nikawaambia watu wakati huo, “Kila mtu na mtumishi wake waende usiku katikati ya Yerusalemu, ili wawe walinzi wakati wa usiku na mfanyakazi wakati huo.”
And at the same time said I vnto the people, Let euery one with his seruant lodge within Ierusalem, that they may be a watch for vs in the night, and labour in the day.
23 Basi si mimi, wala ndugu zangu, wala watumishi wangu, wala watu wa walinzi waliokuwa wananifuata, hakuna hata mmoja wetu aliyebadili nguo zake, na kila mmoja wetu alichukua silaha yake, hata kama angeenda kwa ajili ya kuteka maji.
So neither I, nor my brethren, nor my seruants, nor the men of the warde, (which followed me) none of vs did put off our clothes, saue euery one put them off for washing.

< Nehemia 4 >