< Mithali 17 >

1 Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
MEJOR es un bocado seco, y en paz, que la casa de contienda llena de víctimas.
2 Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
El siervo prudente se enseñoreará del hijo que deshonra, y entre los hermanos partirá la herencia.
3 Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
El crisol para la plata, y la hornaza para el oro: mas Jehová prueba los corazones.
4 Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
El malo está atento al labio inicuo; [y] el mentiroso escucha á la lengua detractora.
5 Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
El que escarnece al pobre, afrenta á su Hacedor: y el que se alegra en la calamidad, no quedará sin castigo.
6 Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
Corona de los viejos son los hijos de los hijos; y la honra de los hijos, sus padres.
7 Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
No conviene al necio la altilocuencia: ¡cuánto menos al príncipe el labio mentiroso!
8 Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
Piedra preciosa es el cohecho en ojos de sus dueños: á donde quiera que se vuelve, da prosperidad.
9 Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
El que cubre la prevaricación, busca amistad: mas el que reitera la palabra, aparta al amigo.
10 Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
Aprovecha la reprensión en el entendido, más que si cien veces hiriese en el necio.
11 Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
El rebelde no busca sino mal; y mensajero cruel será contra él enviado.
12 Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
Mejor es se encuentre un hombre con una osa á la cual han robado sus cachorros, que con un fatuo en su necedad.
13 Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
El que da mal por bien, no se apartará el mal de su casa.
14 Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
El que comienza la pendencia es [como] quien suelta las aguas: deja pues la porfía, antes que se enmarañe.
15 Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
El que justifica al impío, y el que condena al justo, ambos á dos son abominación á Jehová.
16 Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
¿De qué sirve el precio en la mano del necio para comprar sabiduría, no teniendo entendimiento?
17 Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
En todo tiempo ama el amigo; y el hermano para la angustia es nacido.
18 Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
El hombre falto de entendimiento toca la mano, fiando á otro delante de su amigo.
19 Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
La prevaricación ama el que ama pleito; y el que alza su portada, quebrantamiento busca.
20 Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
El perverso de corazón nunca hallará bien: y el que revuelve con su lengua, caerá en mal.
21 Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
El que engendra al necio, para su tristeza [lo engendra]: y el padre del fatuo no se alegrará.
22 Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
El corazón alegre produce buena disposición: mas el espíritu triste seca los huesos.
23 Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
El impío toma dádiva del seno, para pervertir las sendas del derecho.
24 Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
En el rostro del entendido [aparece] la sabiduría: mas los ojos del necio [vagan] hasta el cabo de la tierra.
25 Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
El hijo necio es enojo á su padre, y amargura á la que lo engendró.
26 Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
Ciertamente no es bueno condenar al justo, ni herir á los príncipes que hacen lo recto.
27 Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
Detiene sus dichos el que tiene sabiduría: de prudente espíritu es el hombre entendido.
28 Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.
Aun el necio cuando calla, es contado por sabio: el que cierra sus labios es entendido.

< Mithali 17 >