< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Praise you the LORD. I will praise the LORD with my whole heart, in the assembly of the upright, and in the congregation.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The works of the LORD are great, sought out of all them that have pleasure therein.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work is honorable and glorious: and his righteousness endures for ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He has made his wonderful works to be remembered: the LORD is gracious and full of compassion.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He has given meat to them that fear him: he will ever be mindful of his covenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He has showed his people the power of his works, that he may give them the heritage of the heathen.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands are verity and judgment; all his commandments are sure.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They stand fast for ever and ever, and are done in truth and uprightness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He sent redemption to his people: he has commanded his covenant for ever: holy and reverend is his name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the LORD is the beginning of wisdom: a good understanding have all they that do his commandments: his praise endures for ever.

< Zaburi 111 >