< Zaburi 12 >

1 Msaada, Yahweh, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; nao waaminifu wametokomea.
Help, LORD; for the godly man ceases; for the faithful fail from among the children of men.
2 Kila mmoja anasema kwa jirani yake maneno matupu; kila mmoja anaongea kwa midomo yenye sifa za uongo na maneno ya udanganyifu.
They speak vanity every one with his neighbor: with flattering lips and with a double heart do they speak.
3 Yahweh, katilia mbali midomo yenye sifa za uongo, kila ulimi unanena kwa nguvu mambo makubwa.
The LORD shall cut off all flattering lips, and the tongue that speaks proud things:
4 Hawa ni wale ambao wamesema, “Kwa ndimi zetu tutashinda. Wakati midomo yetu itakapo ongea, ni nani atakaye kuwa mtawala juu yetu?”
Who have said, With our tongue will we prevail; our lips are our own: who is lord over us?
5 “Kwa sababu ya vurugu zilizopo kinyume na maskini, na kwa sababu ya kuugua kwao wahitaji, Nitainuka,” asema Yahwe. “Nitawaletea usalama wanao hitaji.”
For the oppression of the poor, for the sighing of the needy, now will I arise, says the LORD; I will set him in safety from him that puffs at him.
6 Maneno ya Yahwe ni masafi, kama fedha iliyo safishwa katika tanuru duniani, iliyo ng'arishwa mara saba zaidi.
The words of the LORD are pure words: as silver tried in a furnace of earth, purified seven times.
7 Wewe ni Yahwe! Unaye watunza. Una wahifadhi wacha Mungu kutoka katika hiki kizazi cha waovu na hata milele.
You shall keep them, O LORD, you shall preserve them from this generation for ever.
8 Waovu hutembea kila pande pale uovu unapoinuliwa kati ya wanadamu.
The wicked walk on every side, when the vilest men are exalted.

< Zaburi 12 >