< 1 Wakorintho 11 >

1 Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
Be imitators of me, even as I also am of Christ.
2 Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
Now I praise you, that you remember me in all things, and hold firm the traditions, even as I delivered them to you.
3 Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
But I would have you know that the head of every man is Christ, and the head of the woman is the man, and the head of Christ is God.
4 Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
Every man praying or prophesying, having his head covered, dishonors his head.
5 Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
But every woman praying or prophesying with her head unveiled dishonors her head. For it is one and the same thing as if she were shaved.
6 Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
For if a woman is not covered, let her also be shorn. But if it is shameful for a woman to be shorn or shaved, let her be covered.
7 Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
For a man indeed ought not to have his head covered, because he is the image and glory of God, but the woman is the glory of the man.
8 Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
For man is not from woman, but woman from man;
9 Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
for neither was man created for the woman, but woman for the man.
10 Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
For this cause the woman ought to have authority on her head, because of the angels.
11 Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
Nevertheless, neither is the woman independent of the man, nor the man independent of the woman, in the Lord.
12 Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
For as woman came from man, so a man also comes through a woman; but all things are from God.
13 Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
Judge for yourselves. Is it appropriate that a woman pray to God unveiled?
14 Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
Doesn't even nature itself teach you that if a man has long hair, it is a dishonor to him?
15 lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
But if a woman has long hair, it is a glory to her, for her hair is given to her for a covering.
16 Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
But if anyone seems to be contentious, we have no such custom, neither do God's churches.
17 Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
But in giving you this command, I do not praise you, that you come together not for the better but for the worse.
18 Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
For first of all, when you come together in the church, I hear that divisions exist among you, and I partly believe it.
19 maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
For there also must be factions among you, that those who are approved may be revealed among you.
20 Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
When therefore you assemble yourselves together, it is not the Lord's supper that you eat.
21 Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
For in your eating each one takes his own supper first. One is hungry, and another is drunk.
22 Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
What, do you not have houses to eat and to drink in? Or do you despise God's church, and put them to shame who do not have? What should I tell you? Should I praise you? In this I do not praise you.
23 Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
For I received from the Lord that which also I delivered to you, that the Lord Jesus on the night in which he was betrayed took bread.
24 akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: “Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
When he had given thanks, he broke it, and said, "This is my body, which is for you. Do this in memory of me."
25 Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: “Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka.”
In the same way he also took the cup, after the meal, saying, "This cup is the new covenant in my blood. Do this, as often as you drink, in memory of me."
26 Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
For as often as you eat this bread and drink this cup, you proclaim the Lord's death until he comes.
27 Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
Therefore whoever eats this bread or drinks the Lord's cup in a manner unworthy will be guilty of the body and the blood of the Lord.
28 Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
But let a person examine himself, and so let him eat of the bread, and drink of the cup.
29 maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
For he who eats and drinks eats and drinks judgment to himself, if he does not discern the body.
30 Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
For this cause many among you are weak and sickly, and not a few sleep.
31 Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
For if we discerned ourselves, we would not be judged.
32 Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
But when we are judged, we are punished by the Lord, that we may not be condemned with the world.
33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
Therefore, my brothers, when you come together to eat, wait one for another.
34 Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.
But if anyone is hungry, let him eat at home, lest your coming together be for judgment. The rest I will set in order whenever I come.

< 1 Wakorintho 11 >